py thon
JF-Expert Member
- Sep 11, 2016
- 2,476
- 4,448
Leo Mwasa kaitisha press na kulizungumzia sakata la Mchezaji wa Azam Gadiel Michael na Yanga kuna kauli Mkwasa kasema ni rahisi kwa mchezaji wa Azam kwenda simba kuliko yanga.
1.Mkwasa naomba nikukumbushe ndugu yangu huenda uliteleza umesema takriban wachezaji 4 wametoka Azam na kwenda simba bila shida yeyote ila nataka nikukumbushe Mkwasa wachezaji waliosajiliwa simba kutoka Azam ni makombo "wachezaji waliotemwa kikosini" mfano ni Bocco alitemwa na alikuwa mchezaji huru hivyo ilikuwa ni choice yake aende wapi pia kwa kesi ya Manula na Kapombe ni hivyo hivyo walitemwa.
2.Lakini kwa kesi ya Gadiel Michael ni tofauti Azam wanamhitaji bado sababu ya umri wake mdogo na kiwango na pia yupo ndani ya mkataba.Lakini mchezaji ameonyesha nia ya kuondoka anashindikiza kuondoka sasa hapa mlipaswa mkae meza moja na Azam na mlipe ada ya uhamisho Lakini wewe Mkwasa ulifanya ndivyo sivyo mlimsainisha Gadiel ambaye yupo kwenye mkataba na Azam bila ya waajiri wake kujua yani hapa mngekuwa ulaya basi klabu na mchezaji wote mngepewa adhabu kali sana .juzi nilikuwa namsikiliza Gadiel Michael akihojiwa efm alilalamika sana na kulia lia sana kuwa Azam wanamfanyia mtima nyongo lakini Gadiel unafahamu fika upo ndani ya mkataba kwanini usaini yanga bila ya Azam kujua au bila ya Azam na yanga kuongea ?
Twende ulaya kidogo nadhani sote tumeshuhudia saga ya Neymar aliyekuwa anataka kwenda Psg lakini alikuwa ndani ya mkataba na Barca na siku ya kuripoti kambini aliripoti na kufanya mazoezi na kucheza michezo ya pre season huku akifuatilia uhamisho wake na kusubiria PSG na Barca wakubaliane na walipe ada ya uhamisho 222M ili auvunje mkataba aende PSG baada ya PSG kulipa 222M Neymar alienda kujiunga na kusaini mkataba wake PSG
Lakini ndugu yangu Gadiel kinyemela umeenda kusaini yanga ilhali una mkataba Azam halafu unaanza kulia lia unawekewa mtima Nyonga
Na Mkwasa umeteleza kusema tumemsainisha Gadiel ila tulivyotajiwa bei tumeshindwa
Leo hii klabu ya Morocco imetoa kitita cha 120,000 kumsainisha Msuva aliyekuwa kwenye mkataba yanga na nyie toeni pesa kwa Azam mvunje mkataba ,kesi ya akina Bocco walikuwa wachezaji huru .
Gadiel juzi nilimuonea huruma alivyokuwa analalamika ila kwasasa inabidi uwe mpole na Mkwasa utamsainishaje mchezaji bila ya kufuatilia kwa kina
1.Mkwasa naomba nikukumbushe ndugu yangu huenda uliteleza umesema takriban wachezaji 4 wametoka Azam na kwenda simba bila shida yeyote ila nataka nikukumbushe Mkwasa wachezaji waliosajiliwa simba kutoka Azam ni makombo "wachezaji waliotemwa kikosini" mfano ni Bocco alitemwa na alikuwa mchezaji huru hivyo ilikuwa ni choice yake aende wapi pia kwa kesi ya Manula na Kapombe ni hivyo hivyo walitemwa.
2.Lakini kwa kesi ya Gadiel Michael ni tofauti Azam wanamhitaji bado sababu ya umri wake mdogo na kiwango na pia yupo ndani ya mkataba.Lakini mchezaji ameonyesha nia ya kuondoka anashindikiza kuondoka sasa hapa mlipaswa mkae meza moja na Azam na mlipe ada ya uhamisho Lakini wewe Mkwasa ulifanya ndivyo sivyo mlimsainisha Gadiel ambaye yupo kwenye mkataba na Azam bila ya waajiri wake kujua yani hapa mngekuwa ulaya basi klabu na mchezaji wote mngepewa adhabu kali sana .juzi nilikuwa namsikiliza Gadiel Michael akihojiwa efm alilalamika sana na kulia lia sana kuwa Azam wanamfanyia mtima nyongo lakini Gadiel unafahamu fika upo ndani ya mkataba kwanini usaini yanga bila ya Azam kujua au bila ya Azam na yanga kuongea ?
Twende ulaya kidogo nadhani sote tumeshuhudia saga ya Neymar aliyekuwa anataka kwenda Psg lakini alikuwa ndani ya mkataba na Barca na siku ya kuripoti kambini aliripoti na kufanya mazoezi na kucheza michezo ya pre season huku akifuatilia uhamisho wake na kusubiria PSG na Barca wakubaliane na walipe ada ya uhamisho 222M ili auvunje mkataba aende PSG baada ya PSG kulipa 222M Neymar alienda kujiunga na kusaini mkataba wake PSG
Lakini ndugu yangu Gadiel kinyemela umeenda kusaini yanga ilhali una mkataba Azam halafu unaanza kulia lia unawekewa mtima Nyonga
Na Mkwasa umeteleza kusema tumemsainisha Gadiel ila tulivyotajiwa bei tumeshindwa
Leo hii klabu ya Morocco imetoa kitita cha 120,000 kumsainisha Msuva aliyekuwa kwenye mkataba yanga na nyie toeni pesa kwa Azam mvunje mkataba ,kesi ya akina Bocco walikuwa wachezaji huru .
Gadiel juzi nilimuonea huruma alivyokuwa analalamika ila kwasasa inabidi uwe mpole na Mkwasa utamsainishaje mchezaji bila ya kufuatilia kwa kina