Nyumba ya mlevi mmoja nje kuna shimo kubwa la maji bila mfuniko.
Siku moja karudi usiku kalewa tooooop, mambo yakawa hivi:
*MUME*: Fungua mlango!
*MKE*: Leo sifungui! Nimechoshwa na ulevi wako.
*MUME*: kama hufungui najitupa kwenye hili shimo nife kabisa.
*MKE*. Kufa huna faida yoyote duniani!
*MUME* kachukua jiwe kubwa kalitupa kwenye shimo chubwi!
MKE kajifunga kanga, kafungua mlango. Ghafla mume kaingia ndani na kumfungia mke nje.
*MKE*: Nifungulie la sivyo nitapiga kelele majirani waje.
*MUME*: Piga kelele na wakija uwambie unakotoka wapi usiku huu na khanga moja.
*_Walevi huwa hawataki ujinga sometimes_*?