Elections 2015 Mlinzi wa kura na mwizi wa kura ni nani anavunja amani?

Elections 2015 Mlinzi wa kura na mwizi wa kura ni nani anavunja amani?

Madenge Origino

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2010
Posts
1,847
Reaction score
1,095
UKAWA wao wanadai linda kura yako ukishapiga. Ila CCM, polisi na NEC wao hawataki watu walinde kura. Huko nyuma CCM walishatamka kupitia Nape ya kwamba "ushindi ni ushindi tu hata kwa goli la mkono"! Sasa hebu tujadilane baina ya mlinzi na mwizi wa kura ni nani anaweza kuvuruga amani ya nchi hii?
 
Mlinzi wa kura wa chama tayari yupo ndani kwenye kituo huo wizi utafanyika saa ngapi?

Hivi kwa akili zako kama lengo ni kuiba kura NEC inayo simamia uchaguzi nchi nzima, yenye idadi ya watu kamili waliojiandikisha, wao ndio wa kwanza kupata data ya watu waliojitokeza na shortfalls za uchaguzi; kama ni kuchakachua kwanini waangaike na sehemu ambazo kuna watu wengi wakati wana system wanayo manage wao, wanasimamia uchaguzi sehemu zingine hata wagombea wa majimbo hawawezi kwenda piga kambi let alone viongozi wa UKAWA.

Kama kulinda unalinda vipi zaidi ya kuwa na msimamizi ndani na kujua procedures zikoje, kukaa nje ya vituo unahesabu vipi kura wakati hesabu zinapigiwa ndani ya ukumbi.

Safari hii kwakweli watu somo wasipolipata sisi raia wapenda amani tunapenda kuona polisi wakiwashikisha adabu hawa vijana wasiotaka kutii amri za sheria kwa malengo ya kuleta fujo ambazo viongozi wao wana hubiri kutwa kwanza democratic indicators zote tayari zishaonyesha Magufuli for president na UKAWA wamejichimbia kaburi wao wenyewe.
 
Kuna madaraja ya wizi. Mawakala wanaweza kudhibiti wezi ambao mara nyingi wanakuwa ndani ya chumba cha kuhesabia kura.
Kuna majambazi ya kura haya mara nyngi yanakuwa nje ya kituo. Hapa ndo kuna shughuli pevu. Umeme kuzmwa, kuanzisha fujo ndani ya kituo na polisi kuja na kuwatoaa mawakala ambao wanaona ni kikwazo n.k.

Naomba pia tujiulize, kwa nini ccm na serikali yake wanang'ang'ania wapigakura wasirinde kura zao? Kwa nini jeshi la polisi hilohilo linahamasisha ULINZI SHIRIKISHI?

Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani kama mna uwezo wa kudhibiti mwendo kasi barabarani kwa nini huwa mnawauliza abiria juu ya mwendokasi wa gari walilomo? Ttena mmebandika namba zenu kwenye mabasi.

Ushauri wangu ni kwamba ulinzi na usalama wa taifa hili ni wajibu wa kila Mtanzania kwa hiyo Jeshi la Polisi lishirikiane na wapiga kura kulinda kura na siyo kushirikiana na wapiga kura kutengeneza mazingira yanayotoa nafasi kwa wezi wa kura.
 
halafu CCM hawana aibu wanapiga kelele watu waondolewe wakati watu wanatuhumu kuwa wezi hodari wa kura....kweli CCM wameshawaona watz ni wajinga haswa....
 
Kauli mbiu ya UKAWA ni "Mwizi ni mpaka athibitishwe na Mahakama"!
 
ccm wao ndio wafunja amani kwa kauli yoa, yaani wanaandaa ushindi wa wazi wa bao la mkono
 
Kuna jamaa moja jana nilimsikia kwenye ule mdahalo wa akina polepole akisema kuwa kama utabaki eneo la kupigia kura ukilinda kura utavujna amani!

Swali! Kama mlinzi ndo anakuwa mvunjifu wa amani , je, polisi, JWTZ, na makampuni mengi ya ulinzi ya kazi gani?

CCM waache kiini macho, kura zetu tutalinda ss na wao waende nyumbani kwasababu zao zitalindwa na NEC na Polisi
 
Kazi kubwa ni kulinda wezi ndani na nje wenye lengo kununua mawakala, kuforge matokeo, kufanya fujo ili kuwatimua MAWAKALA maeneo ya kituo!!

Lazima kura zilindwe hadi zihesabiwe, MAWAKALA waweke saini, Matokeo yabandikwe kwenye mbao ya matangazo!!
 
Mlinzi wa kura wa chama tayari yupo ndani kwenye kituo huo wizi utafanyika saa ngapi?

Hivi kwa akili zako kama lengo ni kuiba kura NEC inayo simamia uchaguzi nchi nzima, yenye idadi ya watu kamili waliojiandikisha, wao ndio wa kwanza kupata data ya watu waliojitokeza na shortfalls za uchaguzi; kama ni kuchakachua kwanini waangaike na sehemu ambazo kuna watu wengi wakati wana system wanayo manage wao, wanasimamia uchaguzi sehemu zingine hata wagombea wa majimbo hawawezi kwenda piga kambi let alone viongozi wa UKAWA.

Kama kulinda unalinda vipi zaidi ya kuwa na msimamizi ndani na kujua procedures zikoje, kukaa nje ya vituo unahesabu vipi kura wakati hesabu zinapigiwa ndani ya ukumbi.

Safari hii kwakweli watu somo wasipolipata sisi raia wapenda amani tunapenda kuona polisi wakiwashikisha adabu hawa vijana wasiotaka kutii amri za sheria kwa malengo ya kuleta fujo ambazo viongozi wao wana hubiri kutwa kwanza democratic indicators zote tayari zishaonyesha Magufuli for president na UKAWA wamejichimbia kaburi wao wenyewe.




Linapokuja suali la kulinda kura ni kwamba wahusika tayari wamekosa imani na system nzimainayohusika na kusimamia uchaguzi huu yaani NEC na Polisi. Hapo nitakufafanulia pengine itakusaidia kuujua ukweli!
NEC na watendaji wake si huru na hata wewe unalijua hilo!
Tume yote ya uchaguzi pamoja na wasimamizi wote wa uchaguzi wanachaguliwa na Mwenyekiti wenu wa CCM. Huu ni uchaguzi wa vyama vingi Tanzania na sio uchaguzi ya wagombea wa CCM tu! Labda nikukumbushe tu kwa mfano mara tu baada ya kumalizika kwa zoezi la kurejesha fomu za kuomba kugombea ubunge kwa tume ya uchaguzi basi wasimamizi wa uchaguzizaidi ya tisa waliwapa ushindi wagombea ubunge waCCM ushindi wa bila ya kupingwa! Yaani walitaka kupiga bao la mkono mchana kweupe! Kama ingekuwa uchaguzi ni mchezo wa mpira wa miguu basi ni kwamba Refa na washika vibendera wote ni wa upande mmoja!

Hao Polisi ndio hata kipofu anaona ya kwamba wao ni CCM zealots(wanamaskani)! Polisi ni kama wamehasiwa kuwachukulia hatua wanaCCM wanapovuruga amani. IGP na makamishana wote wa polisi wanachaguliwa na Mwenyekiti wenu wa CCM. Sawa ndio katiba inavyosema lakini sheria ni msumeno jamani. Hivi katika uchaguzi huu basi wanaofanya fujo ni wanachama na wagombea wa upinzani tu? Ebu nikukumbushe tena katika uchaguzi wenu wa maoni tu basi tumewashudia kuanzia wagombea ngazi zote - urais, ubunge na udiwani- wakipigana ngumi hadharani pamoja na kugawa rushwa nje nje! Kuna ushahidi na uthibitisho wa picha na video za kina Ndugai, Kamala na yule aliotaka kugombea urais kupitia chama chenu wakipigana ama kupigwa hadharani. Hatukusikia Polisi kuchukua hatua yoyote. Hio rushwa kwenye CCM ndio hata sitaki kuitaizungumzia maana inajulika wazi ya kwamba CCM ni chama cha Rushwa .Wagombea ubunge wa upinzani Msigwa, Masha, Ester Bulaya, Lema na wengine wengi tu tayari wamepelekwa mahabusu. Hapo naona kabakia huyo Lowasa tu kupelekwa mahabusu!

Hapo nimekupa picha tu ya kwamba System nzima inayohusika na uchaguzi huu imeegemea upande wenu wa CCM. Ingelikuwa ni pambano la mpira baina ya Simba na Yanga basi ni sawa na mfano huu: Pambano linachezwa Jangwani, Refa ni mwenyekiti wa klabu ya Yanga, washika vibendera ni makamo mwenyekiti wa Klabu ya Yanga na katibu mkuu wake. Hata wale ball boys hapo jangwani basi ni Polisi. Simba imebakiwa na watazamaji tu! Sasa jee unatarajia matokeo gani hapo. Kwa picha hio ni kwamba UKAWA ni lazima walinde kura zao lasivyo watapigwa mabao!
 
Linapokuja suali la kulinda kura ni kwamba wahusika tayari wamekosa imani na system nzimainayohusika na kusimamia uchaguzi huu yaani NEC na Polisi. Hapo nitakufafanulia pengine itakusaidia kuujua ukweli!
NEC na watendaji wake si huru na hata wewe unalijua hilo!
Tume yote ya uchaguzi pamoja na wasimamizi wote wa uchaguzi wanachaguliwa na Mwenyekiti wenu wa CCM. Huu ni uchaguzi wa vyama vingi Tanzania na sio uchaguzi ya wagombea wa CCM tu! Labda nikukumbushe tu kwa mfano mara tu baada ya kumalizika kwa zoezi la kurejesha fomu za kuomba kugombea ubunge kwa tume ya uchaguzi basi wasimamizi wa uchaguzizaidi ya tisa waliwapa ushindi wagombea ubunge waCCM ushindi wa bila ya kupingwa! Yaani walitaka kupiga bao la mkono mchana kweupe! Kama ingekuwa uchaguzi ni mchezo wa mpira wa miguu basi ni kwamba Refa na washika vibendera wote ni wa upande mmoja!

Hao Polisi ndio hata kipofu anaona ya kwamba wao ni CCM zealots(wanamaskani)! Polisi ni kama wamehasiwa kuwachukulia hatua wanaCCM wanapovuruga amani. IGP na makamishana wote wa polisi wanachaguliwa na Mwenyekiti wenu wa CCM. Sawa ndio katiba inavyosema lakini sheria ni msumeno jamani. Hivi katika uchaguzi huu basi wanaofanya fujo ni wanachama na wagombea wa upinzani tu? Ebu nikukumbushe tena katika uchaguzi wenu wa maoni tu basi tumewashudia kuanzia wagombea ngazi zote - urais, ubunge na udiwani- wakipigana ngumi hadharani pamoja na kugawa rushwa nje nje! Kuna ushahidi na uthibitisho wa picha na video za kina Ndugai, Kamala na yule aliotaka kugombea urais kupitia chama chenu wakipigana ama kupigwa hadharani. Hatukusikia Polisi kuchukua hatua yoyote. Hio rushwa kwenye CCM ndio hata sitaki kuitaizungumzia maana inajulika wazi ya kwamba CCM ni chama cha Rushwa .Wagombea ubunge wa upinzani Msigwa, Masha, Ester Bulaya, Lema na wengine wengi tu tayari wamepelekwa mahabusu. Hapo naona kabakia huyo Lowasa tu kupelekwa mahabusu!

Hapo nimekupa picha tu ya kwamba System nzima inayohusika na uchaguzi huu imeegemea upande wenu wa CCM. Ingelikuwa ni pambano la mpira baina ya Simba na Yanga basi ni sawa na mfano huu: Pambano linachezwa Jangwani, Refa ni mwenyekiti wa klabu ya Yanga, washika vibendera ni makamo mwenyekiti wa Klabu ya Yanga na katibu mkuu wake. Hata wale ball boys hapo jangwani basi ni Polisi. Simba imebakiwa na watazamaji tu! Sasa jee unatarajia matokeo gani hapo. Kwa picha hio ni kwamba UKAWA ni lazima walinde kura zao lasivyo watapigwa mabao!

Hivi haya mawazo huwa mnayatoa wapi, tatizo lenu ni ushabiki sana uwe basi unatafuta credible source za upande ili uweze changanya na zako au angalia vipindi vya maana star TV jumanne or jumatatu ni siku ya kujadili sheria mbali mbali za nchi kuna wataalum wanakuja kutolea ufafanuzi mambo kadhaa yanayotokea kwenye jamii na kutoa msaada wa mawazo ni elimu ya bure kabisa.

Last week hilo swala lilitolewa ufafanuzi na mmoja wa afisa wa NEC kuna sheria ambazo zinataka watu waandike majina yao kamili au kuweka picha sijui yenye rangi blue ni vitu vingine ambavyo ni tosh; yes kuna mawakala waliokuwa wakipokea form za uchaguzi walizikataa kwa sababu ni kweli form zingine azikuandikwa sahihi au azikufuata masharti yanavyotaka.

Hatua ya pili form zikitoka hapo ndio zinaingia ofisi za NEC na wao ndio watafsiri wa sheria ya uchaguzi walipoona hakuna sababu za msingi wahusika waliitwa na kutakiwa kujaza form vizuri na kuendelea na campaign zao kwa hivyo kilichofanywa na watendaji hakina mkono wa NEC ata chembe tena wao ndio waliwarudishia watu nafasi zao walizotaka kudhulumiwa huko kwenye kurudisha form.

Pili kuteua watu hakuna uhakika wa kuwa ndio sababu za kuiba kura, vyama vya siasa vinajua kanuni na procedure za kupiga kura na kufanya uhakiki huko kama kuna lawama ntaelewa lakini kuteuliwa kwa watu hakuna uhalisia wa kuibiwa kwa kura, yaani kwanza NEC ndio inatumia muda kuwapa somo wagombea wa upinzani kuhusu haki zao sio kwamba wazijue kupitia kwenye vyama; viongozi wako busy kulamba miguu ya Lowassa.

Ulichoandika ni akili za UKAWA tu ndio zinaweza fikiria vitu ambavyo havipo.
 
UKAWA wao wanadai linda kura yako ukishapiga. Ila CCM, polisi na NEC wao hawataki watu walinde kura. Huko nyuma CCM walishatamka kupitia Nape ya kwamba "ushindi ni ushindi tu hata kwa goli la mkono"! Sasa hebu tujadilane baina ya mlinzi na mwizi wa kura ni nani anaweza kuvuruga amani ya nchi hii?

Kuna HAJA GANI sasa ya kuwa na MAWAKALA Kama kila mtu atapiga na kulinda kura??
 
Viongozi wanaotoa lawama kwa Tume ni kama hamnazo vichwani mwao! Mwaka huu mwanzoni, viongozi wote wa vyama walikutana na JK kule Dodoma na kuja na azimio kuwa, endapo kura ya maoni haitawezekana kufanyika kutokana na kutokamilika kwa daftari la kudumu, basi Muswada Maalum uandikwe na upelekwe Bungeni kwa ajili ya Mabadiliko ya Katiba ya sasa ili kuwe na vifungu vya TUME HURU, MGOMBEA BINAFSI na MATOKEO YA URAIS KUPINGWA MAHAKAMANI! Viongozi wote wa upinzani Bungeni pamoja na wabunge wao hawakupaaza sauti baada ya kushindikana kura ya Maoni. Badala yake wao walikuwa wanachekelea kile kiinua mgongo cha milioni 230 kila mmoja! Suala MUHIMU la kuongeza vipengere vile vilivyokubaliwa waliliacha lipotee! Sasa ndiyo wanashituka eti Tume siyo huru wakati walizembea wenyewe! Wabunge wa CCM wasingelikumbushia suala hili kwa kuwa lilikuwa halina manufaa kwao! Hivyo, Upinzani wamejitengenezea wenyewe bao la mkono kupitia Tume ambayo wanadai siyo Huru!
 
Nimesikia hoja za upande wa tume ya taifa na hoja za baadhi ya watu hasa upande wa ccm na kuwashngaa sana. Hivi kama watu watapiga kura na kwenda umbali unaokubalika (100m na 200m) na sijui kwa nini waliamua 300m uchaguzi serikali za mitaa) kuna hathari gari? Wasichojua nini? Maana tunajua

1) Baadhi ya wakurugenzi wako tayari kutangaza matokeo kinyume wakisingizia asiyerizika aende mahakamani...yalitokea 2010 Karagwe/Mwanza....
2) Polisi wanaweza kuingia na masanduku ktk vituo vya kupigia kura au wagombea....yalitokea 2010 Musoma
3) Mawakara kuchukuliwa fedha nyingi vituoni zianzowachanganya akili

Wananchi wakilinda kura zao ktk mazingira hayo yatajwa hapo juu shid iko wapi? Mtawaaminsha vipi kuwa hamtaiba/kutangaza matokeo tofauti?

UKAWA mkilala ccm haitalala!
 
Back
Top Bottom