Mlio na mpango wa kununua Gari Mistubishi FUSO single kwa ajili ya biashara usijaribu.

Mlio na mpango wa kununua Gari Mistubishi FUSO single kwa ajili ya biashara usijaribu.

Ziroseventytwo

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
8,581
Reaction score
15,618
Katikati ya miaka 2000, ilikuwa 2006 Tuliingia ubia mimi na jamaa yangu tukanunua gari aina ya Mitsubishi Fuso fighter 17. Gari tuliiagiza kwa kumtuma mtu tuliyemwamini. Kwa wakati ule tulimpa Us$ 9700, alituambia kuwa hizo zilitosha kwa kila kitu.kuanzia kununua, kusafirisha, ukaguzi nk. Baada ya miezi kama m4 gari ikafika. Tukaanza kazi ya kuitoa pale bandarini. Tukalipa kodi, ushuru na tozo nyingine kibao pale bandarini hatimae tukalitoa.

Baada ya wiki tukafanya mpango tukaenda kuweka body pale Tabata dumple. Kazi ikaisha na baada ya process zote gari ikasimama ikiwa na thamani ya 24ml. Tukaenda bima tukakata comprehensive 12% ya thamani ya gari ambayo tuliishusha mpaka 15m na kulipa kama 1.8ml.

Tukaanza kazi. Tukapambana kufa kupona, usiku mchana. Kumbuka tulitoa kila m1 13ml. Sikuwahi kuishika ile 13ml mpaka tulipoamua kuja kuuza gari miaka mi4 baadae. Tukauza ile gari kwa 16ml baada ya kuanza kusumbua.

Nachotaka kusema hapa ni nini.

Wakati sisi tunanunua gari thamani yake ilikuwa 24m. Kwa sasa ukilitaka na ukapitia process nilizotaja hapo huu ni 50-55ml

Wakati ule tyres zilikuwa wastani wa Tsh 150-170k kwa sasa ni 370-400k

Mafuta diesel lita ilikuwa 850 wakati sasa ni 2000. Rim ilikuwa 25k kwa sasa ni 150k. Mzigo wa spring ulikuwa ni kati ya 50k-60 kwa sasa huwezi pata chini ya 250k
Ukiangali gharamaza uendeshaji wa gari zimepanda zaidi ya mara 2. Kwa uzoefu wangu gharama za kusafirisha mzigo toka eneo moja kwenda lingine pesa iliyoongezeka ni kama elfu 2000. Sisi tulikuwa tukitokea labda kibaigwa tulikuwa tunatoza wastani wa shs 500000 kwa tani 10. Kwa sasa ni wastani wa shs 700000 kwa tani 10.

Ushauri.
Kama unataka biashara ya gari aina ya fuso iwe tandam. Hiyo inabeba wastani wa tani16 kwa ingine ile ile ya single. Mafuta ya kutoka dom mpaka dsm tofauti ni lts10. Traffic ukiwapa 5000 hata yule wa single naye anatoa 5000 pia. Kila unachofanya kwa single ndio unachofanya kwa tandam. Tofauti ni zile tyres 4 zinazoongezeka. Uzoefu unaonyesha mwenye single ndio anaongoza kwa kumaliza tairi kuliko wa tandam.
 
Maelezo yako hayana Hoja Za Msngi
Mfano Gari aina hiyo hiyo ukiipaki pale Buguruni chama wapo Madreva wanalipa sh.300,000 Kwa wiki ambayo kwa mwaka ni sawa na sh.15.6Ml
Na gari hizi ikiwa ndo kwanza Mpya inaweza kuchukua miaka mpaka mitatu kuanza kusumbua
 
Maelezo yako hayana Hoja Za Msngi
Mfano Gari aina hiyo hiyo ukiipaki pale Buguruni chama wapo Madreva wanalipa sh.300,000 Kwa wiki ambayo kwa mwaka ni sawa na sh.15.6Ml
Na gari hizi ikiwa ndo kwanza Mpya inaweza kuchukua miaka mpaka mitatu kuanza kusumbua
Hoja yako ww ya msingi iko wapi?
 
Fuso ya tani nne nyie mnabebesha tani 10, gari ikichoka mapema mnasema kuwa gari kimeo kumbe nyie mnaibebesha mzigo zaidi ya mara mbili ya ule mzigo ambao mjapani aliukadiria wakati anatengeneza gari!
Hii kitu ndo inaua gari nyingi hapa bongo ata zisizokua za mizigo.
Unakuta gari ya watu nane wamepanda watu 12 na mizigo mizito, mwisho wa siku gari inakua over loaded injini inazidiwa nguvu na kila kitu kinaharibika.
In short wabongo hatujui kutunza vitu vidumu
 
Unakuta gari ya watu nane wamepanda watu 12 na mizigo mizito
😀😀😀

Umenivunja mbavu.
Siku moja nasafiri nimefika mdaula, kuna majamaa wakubwa kama Le Mutuz wakanisimamisha niwaboost walikuwa na Kivitz kimezimika. Baada ya kuwaboost gari yao ikawaka nikashangaa yale mapande ya watu yako manne yote yakaingia kwenye kile kivitz! Kikabonyeaa mpaka nikabaki mdomo wazi!
 
Katikati ya miaka 2000, ilikuwa 2006 Tuliingia ubia mimi na jamaa yangu tukanunua gari aina ya Mitsubishi Fuso fighter 17. Gari tuliiagiza kwa kumtuma mtu tuliyemwamini. Kwa wakati ule tulimpa Us$ 9700, alituambia kuwa hizo zilitosha kwa kila kitu.kuanzia kununua, kusafirisha, ukaguzi nk. Baada ya miezi kama m4 gari ikafika. Tukaanza kazi ya kuitoa pale bandarini. Tukalipa kodi, ushuru na tozo nyingine kibao pale bandarini hatimae tukalitoa.

Baada ya wiki tukafanya mpango tukaenda kuweka body pale Tabata dumple. Kazi ikaisha na baada ya process zote gari ikasimama ikiwa na thamani ya 24ml. Tukaenda bima tukakata comprehensive 12% ya thamani ya gari ambayo tuliishusha mpaka 15m na kulipa kama 1.8ml.

Tukaanza kazi. Tukapambana kufa kupona, usiku mchana. Kumbuka tulitoa kila m1 13ml. Sikuwahi kuishika ile 13ml mpaka tulipoamua kuja kuuza gari miaka mi4 baadae. Tukauza ile gari kwa 16ml baada ya kuanza kusumbua.

Nachotaka kusema hapa ni nini.

Wakati sisi tunanunua gari thamani yake ilikuwa 24m. Kwa sasa ukilitaka na ukapitia process nilizotaja hapo huu ni 50-55ml

Wakati ule tyres zilikuwa wastani wa Tsh 150-170k kwa sasa ni 370-400k

Mafuta diesel lita ilikuwa 850 wakati sasa ni 2000. Rim ilikuwa 25k kwa sasa ni 150k. Mzigo wa spring ulikuwa ni kati ya 50k-60 kwa sasa huwezi pata chini ya 250k
Ukiangali gharamaza uendeshaji wa gari zimepanda zaidi ya mara 2. Kwa uzoefu wangu gharama za kusafirisha mzigo toka eneo moja kwenda lingine pesa iliyoongezeka ni kama elfu 2000. Sisi tulikuwa tukitokea labda kibaigwa tulikuwa tunatoza wastani wa shs 500000 kwa tani 10. Kwa sasa ni wastani wa shs 700000 kwa tani 10.

Ushauri.
Kama unataka biashara ya gari aina ya fuso iwe tandam. Hiyo inabeba wastani wa tani16 kwa ingine ile ile ya single. Mafuta ya kutoka dom mpaka dsm tofauti ni lts10. Traffic ukiwapa 5000 hata yule wa single naye anatoa 5000 pia. Kila unachofanya kwa single ndio unachofanya kwa tandam. Tofauti ni zile tyres 4 zinazoongezeka. Uzoefu unaonyesha mwenye single ndio anaongoza kwa kumaliza tairi kuliko wa tandam.
Pole kwa yaliyo wakuta. Analysis yako ina dosari kidogo. Presentation yako ingeonekana na mashiko kama ungelinganisha pia ulikuwa unapata nini kwa kubeba mzigo kwenda sehemu, na na-sasa unapata nini, Usiangalie wakati ule tari na vipuri ilikuwa bei gani.
Hakuna kitu kisichokuwa na challenge. Usifanye biashara kwa hisia zako, jaribu kufanya upembuzi yakinifu. Jiridhishe baada ya ku-analyse risks zinazotamani biashara yako.
 
Maelezo yako hayana Hoja Za Msngi
Mfano Gari aina hiyo hiyo ukiipaki pale Buguruni chama wapo Madreva wanalipa sh.300,000 Kwa wiki ambayo kwa mwaka ni sawa na sh.15.6Ml
Na gari hizi ikiwa ndo kwanza Mpya inaweza kuchukua miaka mpaka mitatu kuanza kusumbua

Mkuu hujui chochote kuhusu gari haswa hizi za mizigo. Hicho unachosema hapo kipo kinadharia sana.
 
Back
Top Bottom