Mlio na Mtazamo wangu kama huu kwa 'Kariakoo Derby' ya jana tarehe 30 April, 2022 tujuane tafadhali....

Mlio na Mtazamo wangu kama huu kwa 'Kariakoo Derby' ya jana tarehe 30 April, 2022 tujuane tafadhali....

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
1. Kujiona ( Kujimwambafai ) kabla ya Mchezo kuanza kwa Mshambuliaji Hatari wa Yanga SC Fiston Mayele kulichangia Kumharibu / Kumharibia Kisaikolojia kwani Kitendo kile ni kama vile kiliwapa Kengele Mabeki wa Simba SC waongeze juhudi maradufu katika Kumdhibiti hadi akashindwa Kufurukuta.

2. Upumbavu, Utoto, Ushamba na Nidhamu mbovu ya Winga Mshambuliaji wa Simba SC Bernard Morrison kulichangia kwa 85% kumtoa katika Mchezo na hata Kuikosesha Simba SC Ushindi kwani endapo angekuwa na Maadili ya Kimchezo na kuamua kweli Kucheza Mpira jana angekuwa ni Tishio zaidi na hata Kuwafunga Yanga SC ingewezekana.

3. Kwa mara ya Kwanza Pongezi ziende kwa TFF na Bodi ya Ligi kwa Kumchagua Mwamuzi ( Refa ) Kayoko na Wasaidizi wake Wote kwani walichezesha vyema, kwa Ustadi na Uweledi mkubwa na hakika Wanastahili hata Tuzo kwa Kazi iliyotukuka.

4. Beki wa pembeni Kibwana Shomary ameonyesha kuwa ni Hazina si tu kwa Yanga SC yake bali hata kwa Taifa ( Tanzania ) kwa Uwezo mkubwa alionao ambao hauendani kabisa na Umri wake Mdogo.

5. Beki wa Simba SC Henock Inonga Baka ametoa Darasa tosha kwa Mabeki wote wa Tanzania na wale ambao wana Kazi ya Kumzuia Mshambuliaji Hatari wa Yanga SC Fiston Mayele kuwa watumie sana Akili na siyo Nguvu halafu Wajiamini muda wote.

6. Makocha wa Yanga SC na Simba SC wametnibitisha kuwa uwepo Wao kama Makocha katika hivi Vilabu Vikubwa nchini si wa Makosa au wa bahati mbaya. Pongezi Kwao Wote.

7. Jana Watanzania, Afrika na hata dunia imeshuhudia Derby ya Kibabe kweli na Wametufurahisha Watazamaji wote.

Aksanteni sana Yanga SC na Simba SC.
 
Namba 2 nakubali 100%

Naamini yule Morisson atakuwa anavuta bangi.
 
Kingine Mbinu Ya Kupaki Basi Sometimes Inasaidia .Zile Dk 20 za Mwisho anazozielezea Kaze kuwa Ziliwapa Wakati Mgumu...Kupaki Basi kulisaidia.
 
Enzi zile za kina Zamoyoni Mogela,Peter Tino ,Juma Mkambi,Said Mrisho ,Ally Mchumila,Justine Simfukwe,Thuweni Ally,George Kulagwa(Best) tungeona mashuti ya kumwaga mchezoni..

Wachezaji wote wa pande mbili wajifunze hili,kupiga mashuti.
 
Kitu pekee Cha kushukuru kwa Simba ni Nabii hakuwa benchi!! Kaze yule ni mbovu na afadhali hata Zahera.
 
Enzi zile za kina Zamoyoni Mogela,Peter Tino ,Juma Mkambi,Said Mrisho ,Ally Mchumila,Justine Simfukwe,Thuweni Ally,George Kulagwa(Best) tungeona mashuti ya kumwaga mchezoni..

Wachezaji wote wa pande mbili wajifunze hili,kupiga mashuti.
Aisee siku hizi hakuna washambuliaji kabisa wanaopiga mashuti sijui huko kwenye viwanja vya mazoezi sijui wanafundishwa nini. Mbaya zaidi hata wapigaji wazuri wa faulu nje ya 18 kwenye hizi timu mbili ni kama hakuna kabisa. Sikuona kabisa makipa wakinyooshwa mbavu. Wanashindwa kujifunza hata kwa Orlando jinsi Manula alivyonyooshwa mbavu mfululizo?
 
Aisee siku hizi hakuna washambuliaji kabisa wanaopiga mashuti sijui huko kwenye viwanja vya mazoezi sijui wanafundishwa nini. Mbaya zaidi hata wapigaji wazuri wa faulu nje ya 18 kwenye hizi timu mbili ni kama hakuna kabisa. Sikuona kabisa makipa wakinyooshwa mbavu. Wanashindwa kujifunza hata kwa Orlando jinsi Manula alivyonyooshwa mbavu mfululizo?
We unajua Mpira nimekubali yaani dk 90 hakuna mashuti ya maana.

Zikija penati nazo ni shida wapiga penati tia maji tia maji.

Timu bora lazima ikamilike kila idara ,unafikiri tungekuwa na wapiga penati wazuri siku ya Orlando SA tungetoboa..Manura anajitahidi kuzitoa wachezaji wengine wanapoteza....

Hatua kama ile lazima wachezaji wawe Serious hiyo ndiyo maana halisi ya timu kukamilika.
 
Back
Top Bottom