Mliowahi kuwa na kesi polisi au kwenda mahakamani na mkavijua vifungu hii kesi ipo kundi lipi?

Mliowahi kuwa na kesi polisi au kwenda mahakamani na mkavijua vifungu hii kesi ipo kundi lipi?

mr pipa

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2021
Posts
3,074
Reaction score
6,472
Shemeji yangu alichukua mkataba wa pikipiki dada yake akamdhamini baada ya muda miezi sita ikatokea ajari ikapelekea kifo cha abiria pikipiki ikakamatwa kituoni shemeji yangu, ambae ndiye aliepewa mkataba wa chombo akamtaarifu boss mwenye chombo

Bosi mwenye chombo akakaa kimya dereva akaamua kufuatilia chombo polisi wakaamwambia chombo hakiwezi toka mpaka mazishi yaishe, basi muda ukapita boss mwenye chombo kuona kimya akaanza fuatilia kimya kimya, mwisho akatoa rushwa wakakiachia.

Baadae akarudi kwa mdhamini wa dereva wake na kumwambia atoe hela ambaye ametolea polisi mdhamini kwa woga kwa kuwa bosi alimtisha akamlipia mdogo wake pesa ambayo ni laki mbili, bosi mwenye chombo alivyopata akakaa kimya kwa muda

Baada kupita miez mitatu akamfuata tena mdhamin akidai amlipe hela ya matengenezo milion moja mdhamin akasema kwa sasa sina, likawa kosa akaenda kwa mwenye kiti kesi haijakaa sawa akambeba mdhamin polisi, haijakaa sawa akapewa karatasi aandike barua mwisho wa kulipa sasa muda umepita hivi imekaaje?
 
Mdhamini anahusika vipi wakati muhusika/mdhaminiwa yupo ?

Kama damage imetokana na ajali mdhamini na mdhaminiwa inawahusu nini ?


Mwambien aende mahakamani achaneni na polisi.


Msitoe maelezo yoyote popote mwambien aende mahakamani Wala msiogope
 
Mdhamini amedhamini yale yaliyopo kwenye mkataba. Karudie mkataba wa dereva una kipengere hicho anachodemand. Na kama kipo ni katika mazingira gani ? Yaani matengenezo ya pkpk ni ya dereva au mmiliki? Matengenezo ya namna gani ya service na mayengenezo ndogondogo au matengenrzo makubwa ? Na ikitokeaje ? Akisababisha dereva kwa uzembe ? Ajali haina mwenyewe. By the way mdhaminiwa yupo mdhamini anaweza kuhusika ikiwa aliyedhaminiwa hayupo.
 
Mdhamini anahusika vipi wakati muhusika/mdhaminiwa yupo ?

Kama damage imetokana na ajali mdhamini na mdhaminiwa inawahusu nini ?


Mwambien aende mahakamani achaneni na polisi.


Msitoe maelezo yoyote popote mwambien aende mahakamani Wala msiogope
sawa mkuu asante kwa ushauli
 
Mdhamini amedhamini yale yaliyopo kwenye mkataba. Karudie mkataba wa dereva una kipengere hicho anachodemand. Na kama kipo ni katika mazingira gani ? Yaani matengenezo ya pkpk ni ya dereva au mmiliki? Matengenezo ya namna gani ya service na mayengenezo ndogondogo au matengenrzo makubwa ? Na ikitokeaje ? Akisababisha dereva kwa uzembe ? Ajali haina mwenyewe. By the way mdhaminiwa yupo mdhamini anaweza kuhusika ikiwa aliyedhaminiwa hayupo.
ndio nilicho shangaa chombo anacho mwenye chombo na mwenye chombo baada ya ajari kampa mtu mwingine na sio dereva wa kwanza kinaingiza pesa ila mdhamin kaambiwa atoe pesa ya matengenezo
 
Na umbea wako

Haya twambie mkataba unasemaje endapo chombo kikipata ajali au terms zote zamkataba zinasemaje
 
Mosi
Mdhaminiwa yupo kwanini mdhamini abughuziwe?

Pili
Chombo kilikua hakina bima? Si akakomae na bima

Mwisho
Au ndio ile mamikataba ya kihuni tunayoandikiana uswahilini?
Kwamba chombo ikiibiwa analipa mdhamini, chombo ikipata ajali anagharamikia mdhamini?...... uhuni huu

NB
Mwambieni awapeleke mahakamani
Msikubali kumaliza kesi polisi wala kwa mjumbe.... HAMNA KESI HAPO
 
Back
Top Bottom