Mmarekani adai kufanyiwa ufisadi

kwa bongo mambo mengi ya ajabu hata mtu huwezi kushangaa tena.

hata hivyo katika hili najiuliza "hawa wenzetu hawakawii kwenda
kwenye balozi zao wanapokumbwa na dhahali kama hizi, huyu alipitia
huko?"
 

Yaani nipo pamoja na wewe...pale airport dar...wakati narudi last time nilikuwa na masanduku 5,carry one moja na laptop nimebeba..kuna this guy alikuwa i think ndiyo anafungua masanduku ya watu na kuangalia kuna nini...nikamwangalia nikasema i knwo this guy nimesoma naye IFM...At the time sijui anaangalia nini so niko kwenye foleni nasubiria my time...nilivyofika nikamsalimia hi hakunijibu kanilia kobisi bwana....basi nasukuma masandukua yangu kumbe akafungua sanduku langu la kwanza nikamuuliza whats up mbona unafungua my sanduku bila idnini yangu akasema we have to check nikamuuliza check what?....akasema all these shoes ni biashara nikamwambia hakuna kitu cha biashara ...and for the record nina exempt nikamtolea akanitolea macho akafunga sanduku langu alafu naanz akumsikia aisee vipi za siku nyingi umeptea ndiyo unarudi kimoja au...nikasema kumbe this dude ananikumbuka ila mwanzoni alinilia kobisi la nguvu kujifanya hanijui sasa nina excempt unanikumbuka?....ikawa dhamu yangu sasa kumkaushia......

Then nikaambiw anina bahati sana...maana lazimaningeingizwa mjini...ila uzuri wakati najibishana naye my friends wanaofanya pale airport walikuwa wameshakuja and my dad akawa ameshasogea alijua naingizwa mjini.....maana aliona navyojibishana naye....
 

Fundi anakimbilia umande na kung'ang'ania sopusopu za majuu.
 

Nakuunga mkono. Mbaya zaidi malalamiko haya yatakuwepo 5, 10, 15 years ahead. Watu wapo pale , wanalipwa mshahara na kila siku wanaenda kazini. Vitu vingine vidogo sana, usafi tu wa maliwato unawashinda !! Ningekuwa bosi wa mkuu wa uwanja, angepiga deki bathrooms zote kwa mwezi mzima. Nina uhakika usalama na usafi wa mazingira ni moja ya descriptions za kazi yake.
 
Fundi Mchundo hata eapoti hajui ikoje.

Tubaki kwenye hoja iliyo mbele yetu na tusiingize yaliyotupata. Huyu bwana ametuambia ame-check in mzigo wake Amsterdam, kufika Dar es Salaam, haupo. Kwa nini aamini kuwa umeibiwa Dar tu? Amsterdam hamna wezi? Au haiwezekani kuwa umepelekwa Brunei? Mtu umeibiwa eapoti, central unaenda kufanya nini? Si hao jamaa wana kituo chao pale pale eapoti? Na hiyo laptop anayoizungumzia aliiweka wapi? nayo alii-check in?

Hakuna mtu mwenye akili timamu (hata FM ana akili timamu) anayeweza kusema kuwa hakuna wizi kwenye hiyo eapoti yetu. Wizi upo. Tena wa kipuuzi. Lakini si kila apigae kelele ameibiwa lazima iwe kweli. Mbona nasikia kuna mwanamuziki maarufu alidai kuwa amekwapuliwa simu na wabongo lakini haikuwa hivyo?

Kwa vile kuna waovu pale eapoti haina maana wote ni waovu.

Huyu bwana amejiita researcher halafu hajui tofauti ya exorbitant na exuberant! Muzungu Mmarekani anasema 'fucken'? Huyo Muzungu mmarekani anaomba meseji yake atumiwe State Department (tukizingatia kuwa ameisha rudi kwao)?

This guy is just yanking our collective chain!

Amandla........
 
Wengi mnazungumzia udokozi. Kuibiwa chupi, doli kutoka ndani ya mzigo. Hicho kinatokea. Huyu bwana anazungumzia mzigo (checked luggage) kupotea jumla! Mimi hapo ndipo ninapo tia shaka. Wa kulaumiwa hapo ni airline na si wapakuwa mizigo wenzangu! Au kiingereza kimempiga chenga na ana maanisha aliibiwa laptop iliyokuwa kwenye checked luggage yake? Lakini bado tatizo liko pale pale. Kwani wakina Fundi Mchundo makwapukwapu hawako eapoti za majuu?

Amandla.......
 

Huyu si zinduna na alichofanya kipo sawa sawa tunastahili kufanywa alivyo fanya. Wabongo tumekuwa na tamaa mpaka utu unatutoka. Siku hizi bongo watu hawajali utawaitaje wao ni hela tu. Vitendo kama hivi vipo na vimejaa na vinakuzwa na wanasiasa wetu.

Ntakupa mfano, mdogo wangu alihudhuria depo pale CCP-Moshi, kipindi hicho mkuu wa polisi ni Mahita. Siku ya graduation mgeni rasmi alikuwa Waziri mkuu Sumaye enzi hizo. Katika hotuba yake Mahita aliongea mbele ya waziri mkuu na alifika mahala akaamrisha microphone izimwe unajua alichoongea?
"Leo mnamaliza mafunzo mnaenda kuanza kazi, kuna mambo mengi mtakutana nayo kazini ila napenda niongelee moja kwa ufasaha, ukimkamata mtu akikupa dau la shs elfu mbili, kumi, laki chukua hapo hapo. Ila kibaya zaidi ni kudai akuongezee nyingine kwa kukupeleka sehemu akachukue hapo litakalo kukuta usimlaumu mtu"

Sasa kama viongozi wanapalilia rushwa unatarajia nini?. Haya ni matunda ya kutokuwa na uongozi thabiti tokea mwaka 1985. Enzi za mwalimu watu walikuwa wanaulizwa bila kujali cheo au nafasi yake ee bwana umepata wapi utajiri huu?, siku hizi mtu ana mshahara wa laki tatu kwa mwezi yupo kazini miaka miwili ana miliki mali zenye thamani ya shs milioni mia sita na hakuna wa kumuuliza.

Tanzania inanuka sana hasa maeneo kama customs, polisi na sehemu zote zenye huduma kwa umma. watu wamekuwa manyang'au Tanzania si binadamu tena
 

Hey Fundi zinaitwa laputopu na sio laptop
 
Hiki ni Kiingereza cha Waafrika na siyo mtu aliyezaliwa na kusoma Marekani. Inaonesha hii letter imeandikwa kwa makusudi ya kupunguza Utalii TZ; na si vinginevyo.
 
Huu waraka una sehemu ambazo zinatatiza ulitakiwa uweke source yake. Hatukatai kupotea kwa mizigo kunatokea na rushwa ipo. Kinacholeta taabu hapa ni suala la kufuatilia mzigo polisi badala ya ndege iliyombeba msafiri, unless atuambie mzigo uliibiwa mkononi mwa msafiri.

Cha ajabu ukiingia na KLM utashangaa wazungu wanapita wakipeta ukitokeza wewe mbongo wanakudaka. Rushwa pale kama huko makini wanakuingiza mkenge, jamaa yangu mmoja aliwahi tozwa visa zaidi ya ile iliyobandikwa ukutani, haikuishia hapo jamaa akadaiwa kulipia ushuru $350 gauni ya harusi aliyokuwa amebeba kuja kuoa, jamaa walipoulizwa wapi inasema nguo binafsi isiyo ya biashara inatozwa ushuru hawana jibu.
 

This is a phony email! Whoever wrote it appears not to have English as his first language. You don't write things like "Please advise any potential traveler to Tanzania to look for alternative country to visit, and if possible pass the message to the State Department as a warning to other Americans intending to visit this poor and corrupt country." to someone who's presumably a personal friend/colleague. Besides, why wouldn't the author contact the State Department himself now that he's back in the US? That said, the kinds of shenanigans mentioned do happen to be a reality for many (but far from most) a traveler and client at the JKNIA and at Dar port respectively.
 
Hizi emails zingine nazo mmhhhh!

Huyu mbantu aliyeandika hii email angeweza kufikisha ujumbe wake vizuri tu bila kujifanya Mmarekani researcher asiyejua mambo mengi ya msingi ikiwa pamoja na umuhimu wa kubeba mkononi laptop yake yenye utafiti wa miaka minne... mmhh haya bana tutafika tu!
 
Whether its cooked or raw, this document touched me personally on this, and I quote "They don’t even fucken know that we are trying to help them" end of quote, hapa amemshika nyani ******! and what do you expect ni makofi tu, regardless ni mzungu au nani anayejaribu kufikisha ujumbe kwa staili hii, huyu mtu atakuwa ana matatizo! Nani kasema tunahitaji msaada wa wazungu ili kuendelea, we dont need you nor your stupid help, helping me by giving me a car so that you can sell your spares, that aint help! . Then he goes on by saying, and I quote "I pity the African continent and her people" end of quote. Then he proceeds by saying, and I quote
"I visited Botswana with my family in 2006. I tell you, could not be more satisfied with their politeness and straightforwardness, the same was in Mozambique where we received utmost hospitality" end of quote. Sasa isn't this contradicting, piting the continent and her people na dthen say that the case is different in Botswana and Mozambique! Arent these part of the continent! And if you pity the continent and her people, who told you to come here any way? We dont need you, stay away from this place white boy!
 
Halafu washashi wakikata aka bila kiguu mnawamind.
 
Mizungu inapenda shortcut siku hizi sidhani kama hii ina ukweli ndani yake. After all alikuwa analeta nini tanzania mpaka aapize eti hatarudi? Nafikiri huyu ni displaced mzungu atuondolee uchuro wake humu ndani. Mwee!
 

....Well stated.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…