Mmea uitwao manuka

Ni matajiri tu ndiyo wanamudu mambo haya. Hiyo £35 sijanunu bundle ya kuchat JF!

Usiseme hivyo Sky hakuna aliyezaliwa maskini kila mtu ana utajiri wake sema tunazidiana tuu kiwango cha kuuzalisha huo utajiri.

Na linapokuja swala la afya ili kulinda uhai watu wako radhi kuwa masikini ili kunusuru uhai wa mpendwa wao. Wee niambie mtu asikie hiyo asali inaponya kisukari na ana mama yake ambaye anaugua kisukari alimlea kwa tabu hadi akamaliza chuo na sasa ana ajira. Atajopa hata vikoba aagize hiyo asali vichupa kwa vichupa ili mama yake apone, akishindwa kukopa atauza gari simu dhahabu zake tv friji ili mama apone. Uhai unapiganiwa ILA... hakuna watu wabaya kama wafanya biashara, mimi na wewe hatuna uhakika kama hiyo asali kweli imerinwa kutokana na nyuki walionyonya hayo maua.... what if wamechanganya na asali za viwandani na kuaminisha ina virutubisho hivyo asilia....

Bado naitetea asali yetu ya Tabora, mwanzo ilikuwa asilia zaidi sema wivu wao wazungu wa kutaka kututawala milele ndo kutuharibia na mazao yasiyo hata tufaidisha sie (maana wakiacha kuyanunua hatuwezi kuyala wala kuyatumia) kisha asali yetu ionekane ina niccotin na ina madhara kwa binadamu ila wao waje na hiyo asali ya Manuka watuuzie kwa bei kubwa hivyo.

Hawa dawa yao ni kwenda nao sahani moja, TIT FOR TAT, fatiki ifanyike huo mmea tuulete bongo upandwe kwenye miko atajwa yenye hali ya hewa ya ubaridu halafu hata tusipowauzia tunajitibu wenyewe na magonjwa nyemelezi. Uhai mtamu bana hakuna anayetaka kufa na matibabu ni aghali siku zote.

Ikija kwenye afya na uhai bando la kuingia JF wala hutakuwa na hamu nalo.

Mzaliwa wa Tabora.
 
Kwahiyo hii inatofauti na ile asali ya huku kwetu ya nyuki wadogo,wanaopata asali yao kwenye vyanzo vingine hata ukitajiwa unaweza usiile..?
 
Dah...vipi unasaidia saidia kidogo?😀😀😀
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…