La Quica
JF-Expert Member
- Dec 19, 2017
- 1,009
- 2,315
Mwenye gari hili aliamka asubuhi na kung'amua mzingiro huo mweupe kwa usafiri wake.
Kwa hofu ya dhahiri, aliacha kulitumia akawa anaenda kwa taxi kazini kwake. Muungwana huyu alimuita Fundi Makenika asaidie kulivuta, lakini mwigo wa hofu ukamwingia fundi nae akatokomea baada ya kuona mzingiro huo.
Sasa, akitoka kazini anakuta Mwanae anacheza cheza kwenye duara hilo. Baba alimbwatukia si kitoto, lakini mwana huyo mdogo akamwambia "Baba ni mimi nimezungushia hapa. Mama alinipa unga wa mahindi uliokwisha muda wake kuumwaga. Nikazungushia hapa ili niwe nacheza kwenye duara."
Hadi unaposoma ujumbe huu amini kwamba, yule Bwa'Mdogo anakula kichapo.
Kwa hofu ya dhahiri, aliacha kulitumia akawa anaenda kwa taxi kazini kwake. Muungwana huyu alimuita Fundi Makenika asaidie kulivuta, lakini mwigo wa hofu ukamwingia fundi nae akatokomea baada ya kuona mzingiro huo.
Sasa, akitoka kazini anakuta Mwanae anacheza cheza kwenye duara hilo. Baba alimbwatukia si kitoto, lakini mwana huyo mdogo akamwambia "Baba ni mimi nimezungushia hapa. Mama alinipa unga wa mahindi uliokwisha muda wake kuumwaga. Nikazungushia hapa ili niwe nacheza kwenye duara."
Hadi unaposoma ujumbe huu amini kwamba, yule Bwa'Mdogo anakula kichapo.