Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,336
- 4,731
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa wilayani Simanjiro mkoani Manyara kwa kushirikiana na ofisi ya Taifa ya mashtaka mnamo tarehe 22/06/2020 itamfikisha katika mahakama ya wilaya ya Simanjiro mmiliki wa kituo cha mafuta Simon Lemeya kilichopo Wilaya ya Simanjiro Simon Lemeya Tukai.
Lemeya atafikishwa mahakamani kwa kughushi matumizi ya nyaraka kudanganya na kuisababishia serikali hasara ya sh. milioni tano laki sita na elfu tisa (5,609,000) Kinyume cha Aya ya 10(1) jedwali la kwanza, kifungu cha 57(1) na 60(2) sheria ya uhujumu uchumi Cap 200 marejeo ya 2002.
Wengine waliounganishwa na Lemeya ni Ezekiel Fabiani Mayumba ambaye alikuwa Afisa afya na mratibu wa chanjo ya mama na mtoto wilayani Simanjiro na Ally Sadick Mnkeni na Simaloi Baby Lemeya ambao ni wafanyakazi vituo vya mafuta Simanjiro.
Uchunguzi wa TAKUKURU ulibaini kuwa mnamo mwaka 2014 walighushi nyaraka na kufanya ubadhilifu wa fedha za chanjo ya kitaifa ya Rubella na surua na kuisababishia hasara serikali ya sh. milioni tano laki sita na elfu tisa.
Lemeya atafikishwa mahakamani kwa kughushi matumizi ya nyaraka kudanganya na kuisababishia serikali hasara ya sh. milioni tano laki sita na elfu tisa (5,609,000) Kinyume cha Aya ya 10(1) jedwali la kwanza, kifungu cha 57(1) na 60(2) sheria ya uhujumu uchumi Cap 200 marejeo ya 2002.
Wengine waliounganishwa na Lemeya ni Ezekiel Fabiani Mayumba ambaye alikuwa Afisa afya na mratibu wa chanjo ya mama na mtoto wilayani Simanjiro na Ally Sadick Mnkeni na Simaloi Baby Lemeya ambao ni wafanyakazi vituo vya mafuta Simanjiro.
Uchunguzi wa TAKUKURU ulibaini kuwa mnamo mwaka 2014 walighushi nyaraka na kufanya ubadhilifu wa fedha za chanjo ya kitaifa ya Rubella na surua na kuisababishia hasara serikali ya sh. milioni tano laki sita na elfu tisa.