GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Hivi naandika huu Uzi kuna Mtu mmoja sasa nimemsindikiza kumpeleka kupata huduma ya Kwanza baada ya kupata Kipigo cha Shalubela / Hatari kutoka kwa Mtu ambaye alimtania na lile neno ambalo huwa linapenda sana kutumika humu JF na nahisi huyo ' Mhanga ' wa Kipigo hicho atakuwa ni mwana JF tu.
Wamebishania mambo ya Siasa kisha mara ghafla nikasia ' Mpigaji ' anaambiwa asiwe kama Mwanaume wa Dar ndipo nikaona Mtu kapigwa Kichwa ambacho sidhani hata aliyekuwa Mfungaji bora wa magoli ya Vichwa nchini Tanzania Abeid Mziba Tekero alikuwa akivipiga hivi.
Hii ni mara ya pili nashuhudia Mtu anapata Kichapo / Kipigo kutokana na ' matani ' ambayo mara nyingi huwa nayaona humu Jamvini ambapo kuna Siku nilishuhudia tena Mtu akipigwa ' Kibao ' kitakatifu baada ya kumuita mwenzake Popoma ( neno linalomaanisha Pumbavu ) ambapo hadi alizimia na kugundua kwamba yule aliyempiga Kibao lazima tu atakuwa alikuwa ni Mjeda / Mwanamedani.
Nitoe Rai kwenu tafadhalini tutaniane tu humu humu Jamvini na haya maneno yetu lakini chonde chonde msihamishie haya maneno yetu humu na mkayapeleka huko mitaani kwani mtaumia na hasa mkizingatia Watu wengi sasa hivi wana ' stress ' zao za Kimaisha.
Nawasilisha.
Wamebishania mambo ya Siasa kisha mara ghafla nikasia ' Mpigaji ' anaambiwa asiwe kama Mwanaume wa Dar ndipo nikaona Mtu kapigwa Kichwa ambacho sidhani hata aliyekuwa Mfungaji bora wa magoli ya Vichwa nchini Tanzania Abeid Mziba Tekero alikuwa akivipiga hivi.
Hii ni mara ya pili nashuhudia Mtu anapata Kichapo / Kipigo kutokana na ' matani ' ambayo mara nyingi huwa nayaona humu Jamvini ambapo kuna Siku nilishuhudia tena Mtu akipigwa ' Kibao ' kitakatifu baada ya kumuita mwenzake Popoma ( neno linalomaanisha Pumbavu ) ambapo hadi alizimia na kugundua kwamba yule aliyempiga Kibao lazima tu atakuwa alikuwa ni Mjeda / Mwanamedani.
Nitoe Rai kwenu tafadhalini tutaniane tu humu humu Jamvini na haya maneno yetu lakini chonde chonde msihamishie haya maneno yetu humu na mkayapeleka huko mitaani kwani mtaumia na hasa mkizingatia Watu wengi sasa hivi wana ' stress ' zao za Kimaisha.
Nawasilisha.