mnaomba msaada wako mdau

Kristonsia Nkya

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2013
Posts
302
Reaction score
292
Je kupungua kwa homoni ya
Gonadotropin kunaweza kusababisha
mwanamke asipate mimba? ! Rafiki yangu
amekaa na mke wake zaidi ya miezi 5 bila
kupata mtoto baada ya kwenda kupima
wote wawili dkt akasema kwamba
mwanamke anaupungufu wa hiyo
homoni!! Je hili tatizo linaweza kutibika?
Msaada kwa kiswahili plz wadau
 

Pole kwa rafiki wa dada Kristonsia Nkya...Gonadotropins ni group la vichocheo (hormones) 3 ambavyo kwa kiasi kikubwa ndio vinacontrol mzunguko wa mwanamke wa mwezi. Kiasi cha vichocheo hivyo katika damu ndio vinacontrol ovaries (viwanda vya kuzalishia mayai ya kike) kutoa kichocheo kingine kiitwacho Estrogen, pia kupevuka kwa yai la kike, na kisha kutolewa kwa yai la kike lilopevuka. Yai hili ndio hurutubishwa na baadae kutunga mimba. Vichocheo vya gonadotropins pia uhusika na kusimamia mimba hasa ikiwa changa.

Unapokosa kiasi cha kutosha vichocheo vya gonadotropins (inategemea kichocheo kipi kati ya hivyo vi3 au vyote) kunaweza sababisha mayai yasipevuke, yai lisitolewe, au linapopevuka na kutolewa na kurutubishwa..lisiweze kujishikiza kwenye kizazi (uterus) na kutungisha mimba.

Matibabu inategemea na nini sababu ya kutokuwa na vichocheo vya gonadotropins vya kutosha. Mara nyingi kama matatizo ya levels tu, unaweza tumia hormonal replacement therapy, kwa kupewa dawa za kuongeza kiasi cha gonadotropins zilizupungua, au kama ni uvimbe wa Ovary au Pituitary (matezi yasimamiayo uzalishwaji wa vichocheo hivyo)..utahitaji uchunguzi zaidi na matibabu.

Ushauri: Nenda kamuone daktari bingwa wa maginjwa wa kina mama atanabaishe tatizo ni nini, kisha atakushauri nini cha kufanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…