KERO Mnaotoa Vyeti vya Serikali mnakwaza kukosea Herufi za Majina ya Watumiaji wa Nyaraka hovyo

KERO Mnaotoa Vyeti vya Serikali mnakwaza kukosea Herufi za Majina ya Watumiaji wa Nyaraka hovyo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Mwanangu yuko katika hatua za kuomba nafasi chuoni mwaka huu, lakini anapata usumbufu mkubwa kubadilisha majina kwenye cheti chake cha kuzaliwa ili yaendane na yale yaliyo kwenye vyeti vya shule. Hii ni hatua muhimu ili aweze kuendelea na mchakato wa kuomba chuo.

Vivyo hivyo, hata wakati wa kujiandikisha kwa Kitambulisho cha Taifa, anakumbana na kero kwa sababu jina la pili kwenye cheti chake cha kuzaliwa limeandikwa vibaya.

Ili kutatua tatizo hili, ameshauriwa kupata barua kutoka kwa mwanasheria, jambo ambalo ni kero kubwa na linaongeza gharama zisizo za lazima.

Mara nyingi, watu wanalazimika kupitia usumbufu mkubwa kubadilisha majina kwenye nyaraka kama TIN Number, NIDA, vyeti vya kuzaliwa na vya kifo, wakati mwingine hadi kufika mahakamani kuapa.

Soma Pia: Tatizo katika uhakiki wa vyeti kwa wanafunzi wanaoomba Mkopo na huduma za RITA kwa ujumla


Wahusika wa kutoa nyaraka hizo muwe makini ili tuepuke huu usumbufu na gharama
 
Sawa kabisa na hii yote ni sababu ya wengine kuwekwa sehemu nyeti si sababu ya sifa bali connection ki mjomba mjomba, unakuta mtu anaitwa Raphael lakini anaandikiwa ,Laphael au Grace alafu Gresi yaani hayo ndio yapo huko mitaani.
 
Muda wote huo hujahakiki majina ya mtoto kuanzia primary mpaka leo anaenda chuo, huo ni uzembe wako.

Ilibidi pale RITA unapopokea cheti cha mtoto uhakiki taarifa zote kama ziko sahihi.
 
Mwanangu yuko katika hatua za kuomba nafasi chuoni mwaka huu, lakini anapata usumbufu mkubwa kubadilisha majina kwenye cheti chake cha kuzaliwa ili yaendane na yale yaliyo kwenye vyeti vya shule. Hii ni hatua muhimu ili aweze kuendelea na mchakato wa kuomba chuo.

Vivyo hivyo, hata wakati wa kujiandikisha kwa Kitambulisho cha Taifa, anakumbana na kero kwa sababu jina la pili kwenye cheti chake cha kuzaliwa limeandikwa vibaya.

Ili kutatua tatizo hili, ameshauriwa kupata barua kutoka kwa mwanasheria, jambo ambalo ni kero kubwa na linaongeza gharama zisizo za lazima.

Mara nyingi, watu wanalazimika kupitia usumbufu mkubwa kubadilisha majina kwenye nyaraka kama TIN Number, NIDA, vyeti vya kuzaliwa na vya kifo, wakati mwingine hadi kufika mahakamani kuapa.

Soma Pia: Tatizo katika uhakiki wa vyeti kwa wanafunzi wanaoomba Mkopo na huduma za RITA kwa ujumla

Wahusika wa kutoa nyaraka hizo muwe makini ili tuepuke huu usumbufu na gharama
Wenzenu wanatengeneza mazingira ya ruushwa kama hamjui
 
Cheri cha kuzaliwa, jina ni Joseph Elikunda, jinsia ni Ke.

Taasisi za umma zina shida sana.
 
Cheri cha kuzaliwa, jina ni Joseph Elikunda, jinsia ni Ke.

Taasisi za umma zina shida sana.
Sio lazima Joseph Elikunda kuwa mwanaume! Jamani watanzania tuwe makini kidogo!
 
Back
Top Bottom