Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,750
DPP awaachia watuhumiwa wa mauaji ya maalbino
2009-02-12 10:32:05
Na Pendo Fundisha, Mbeya
Mahakama ya Wilaya ya Rungwe imewaachia huru washitakiwa wawili waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka ya mauaji ya albino, Henry Mwakajila, aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha pili wa Shule ya Sekondari ya Ukukwe iliyopo Wilaya ya Ileje.
Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Stephen Mbungu jana alisema kuwa washtakiwa hao wanaachiwa huru kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) baada ya kuagiza kuwa hakuna haja ya kuendelea kusikilizwa kwa kesi hiyo.
Mbungu aliwataka waliochiwa kuwa ni Mganga wa jadi maarufu kama sangoma, Asangalwisye Katite na Gererde Kalonga, Wakazi wa Wilaya ya Ileje.
Mara baada ya mahakama hiyo kutangaza kuwaachia huru, washitakiwa hao walijikuta furaha yao ikikatishwa ghafla na kupigwa bumbuwazi kisha kupiga kelele baada ya kukamatwa tena na askari polisi na kupelekwa katika kituo cha Wilaya ya Rungwe kichopo mjini Tukuyu.
Akizungumza na waandishi wa habari Hakimu huyo alisema tatizo la mauaji ya malbino lisichukuliwe mzaha hata kidogo la sivyo jitihada zote za viongozi wakuu wa nchi hazitazaa matunda kuyakomesha.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Rungwe , Mariamu Lugaila alisema maamuzi hayo yanaweza kuleta matatizo katika jamii na kukwamishwa mauaji ya maalbino.
Washtakiwa hao walikamatwa na polisi Febuari 27, mwaka jana kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya viungo vya binadamu.
Inadaiwa polisi waliwafanyia upekuzi na kuwakamata na baadhi ya viungo vya binadamu vilivyosadikiwa kuwa ni vya albino na kuhusishwa na mauaji ya mwanafunzi huyo baada ya kupotea nyumbani kwao katika Kijiji cha Kiwira februari 27, mwaka jana katika mazingira ya kutatanisha.
SOURCE: Nipashe
2009-02-12 10:32:05
Na Pendo Fundisha, Mbeya
Mahakama ya Wilaya ya Rungwe imewaachia huru washitakiwa wawili waliokuwa wakikabiliwa na mashtaka ya mauaji ya albino, Henry Mwakajila, aliyekuwa mwanafunzi wa kidato cha pili wa Shule ya Sekondari ya Ukukwe iliyopo Wilaya ya Ileje.
Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Stephen Mbungu jana alisema kuwa washtakiwa hao wanaachiwa huru kwa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) baada ya kuagiza kuwa hakuna haja ya kuendelea kusikilizwa kwa kesi hiyo.
Mbungu aliwataka waliochiwa kuwa ni Mganga wa jadi maarufu kama sangoma, Asangalwisye Katite na Gererde Kalonga, Wakazi wa Wilaya ya Ileje.
Mara baada ya mahakama hiyo kutangaza kuwaachia huru, washitakiwa hao walijikuta furaha yao ikikatishwa ghafla na kupigwa bumbuwazi kisha kupiga kelele baada ya kukamatwa tena na askari polisi na kupelekwa katika kituo cha Wilaya ya Rungwe kichopo mjini Tukuyu.
Akizungumza na waandishi wa habari Hakimu huyo alisema tatizo la mauaji ya malbino lisichukuliwe mzaha hata kidogo la sivyo jitihada zote za viongozi wakuu wa nchi hazitazaa matunda kuyakomesha.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Rungwe , Mariamu Lugaila alisema maamuzi hayo yanaweza kuleta matatizo katika jamii na kukwamishwa mauaji ya maalbino.
Washtakiwa hao walikamatwa na polisi Febuari 27, mwaka jana kwa tuhuma za kujihusisha na biashara ya viungo vya binadamu.
Inadaiwa polisi waliwafanyia upekuzi na kuwakamata na baadhi ya viungo vya binadamu vilivyosadikiwa kuwa ni vya albino na kuhusishwa na mauaji ya mwanafunzi huyo baada ya kupotea nyumbani kwao katika Kijiji cha Kiwira februari 27, mwaka jana katika mazingira ya kutatanisha.
SOURCE: Nipashe