MNEC Ruvuma atoa msaada wa Chakula kwa wahanga wa maafa ya mvua

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Ruvuma, Hemed Chale, ametoa msaada wa chakula kwa wahanga wa maafa yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha tarehe 28 Desemba 2024 na tarehe 2 Januari 2025 wilayani Songea, mkoani Ruvuma.

Mvua hizo zilileta uharibifu mkubwa wa miundombinu, ambapo nyumba 155 ziliharibiwa. Msaada huo ulijumuisha mchele kilo 345, Maharage kilo 138, na mafuta ya kupikia, na umekabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Songea ili kusaidia wahanga katika kipindi hiki cha maafa, ambapo wanajitahidi kurejesha hali ya kawaida na mazingira bora ya kuishi.

Pia, Soma: Waziri Dkt. Ndumbaro Awafariji Waathirika wa Mvua Songea

Akipokea msaada huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa na Mkuu wa Wilaya ya Songea, Wilman Kapenjama Ndile, alimuhukuru kiongozi huyo kwa msaada alioutoa kwa jamii iliyokumbwa na maafa.

Vilevile, Ndile alitoa wito kwa Maafisa Tawala na Viongozi wa Serikali ya Mtaa kuhakikisha kuwa misaada hiyo inawafikia walengwa kwa usahihi na kwa wakati.
 
ni muhimu sana kujitolea kwa wahitaji 🐒
 
Anataka Ubunge wa wapi huyu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…