Mnyika: Msajili Jaji Mutungi ameitisha kikao cha Makundi mbalimbali kujadili Katiba Mpya 26/5/2023, Sisi CHADEMA hatutaenda Hatuna Imani naye!

Usikatae wito kataa neno.
Kwa ushauri wangu wangeenda harafu kama ajenda kikao itaenda na kinyume cha matakwa yao hapo ndo wangekataa.
Lakini siyo kukataa wito.
 
Ccm imeharibu sana nchi na Wananchi Kwa wizi, ufisadi na uroho wa madaraka
 
Umetoa mawazo ya kujenga, Mungu akubariki
 
Mbona hawatafanikiwa akina Chadema.Kama vyama vingine vyote vya siasa vitashiriki kuunda katiba mpya na kushiriki uchaguzi mkuu,chama kimoja hakitafua dafu katika kutuchonganisha kwa jumuiya ya kimataifa.
Nyuki mmoja aweza kuzidi maelfu ya nzi
 
Hii Katiba Mpya inayosimamiwa na kuendeshwa na serikali ya chama kimoja ni upuuzi mtupu.
 
Mnyika na Lissu nawaonea huruma 🤣🤣🤣

Ni watu wenye integrity ya hali ya juu sana, lakini tatizo liko pale juu.

Ngoja tusikie mwanyekiti atasemaje, maana ni kama Mnyika kafanya 'preemptive strike' dhidi ya mwenyekiti.
Wewe nawe unatoa hoja kana kwamba siyo GT anayefikiri vyema..

CHADEMA siyo "animal farm" jombaaa..!!

Yaani wewe kwa akili yako unadhani katibu mkuu wa chama cha siasa kama CHADEMA chenye very strong administration structure anaweza kutoka public kutoa statement kwenye issue sensitive kama ya katiba mpya bila kwanza kupita kwenye vikao vya maamuzi ndani ya chama na kuwekewa msimamo wa pamoja ambavyo mwenyekiti wa vikao hivyo ndiye mwenyekiti wa chama?

Think twice ndugu...

Umiza akili yako. Acha kukaririshwa kama kasuku. Ukisikia jambo, nawe fuatilia ujue ukweli wake ndipo useme au uandike!!!
 
Katibu mkuu wa CHADEMA John Mnyika anesema amepokea Barua Kutoka kwa Msajili wa vyama vya Siasa Jaji Mutungi ikiwaalika kushiriki Mkutano wa kuratibu Katiba Mpya
😳😳 Ati amepokea Barua! Mbona jambo hili limefahamika tokea Mkuu wa nchi kutoa maagizo hayo? Ina maana alitegemea kupata mwaliko rasmi. Haijalishi......
Mnyika amesema Serikali imeamua Mutungi ndio ayaunganishe makundi yote nchini yaani Wafanyabiashara, Wasanii, Wakulima, Wafugaji, Wanasiasa nk katika maandalizi ya kuandaa Katiba Mpya

CHADEMA-Maridhiano (Asali), walitegemea wao wabaki na kutoa ushauri na maamuzi kwa kigezo kuwa (waliandika barua ya kuomba maridhiano) Huku kwingine, CHADEMA-Maridhiano (Katiba) wakiona na kushauri Vyama na asasi zingine zijumuishwe kwenye mchakato wa Mchakato wa Katiba uliotokana na kuridhiwa na CHADEMA(Asali) +CCM(Liberali) Yaani kwa hatua waliyofikia,-wengine wahusishwe, tena baada ya Wanasiasa kama Dk Slaa na Zitto na vyama vingine vya siasa kudai wanaachwa nyuma au kotohusishwa na Mchakato wa maridhiano;Lissu alijiondokea kwenda Ubeligiji pamoja nakuwa na sababu zingine-Alisusia baada yakuona hahusishwi katika maamuzi(chanzo cha mgogoro?)
Mnyika amesema CHADEMA hawamwamini Jaji Mutungi kwa sababu ndiye Kiini cha Kupandikiza Migogoro hivyo hawatahudhuria Mkutano huo
....ati sasa bado wanaendelea kumtafuta mchawi wao?? CHADEMA wamekuwa wasusaji wa karibia Michakato mingi yenye mustakabhali wa Nchi kwa sababu ya Kutokuafikiana kichama baina yao.(na uharakati)....

.... Historia inatueleza hivyo!

Yaani wakiwa hawana misimamo, huwa wanatumia Kususa au kugoma kuingia kwenye ile Michakato wanayoanzisha wao wenyewe au ile wanayotaka wachukue Credit kuanzisha! What a Shame. Historia inatueleza hivyo!

CHADEMA;Jaji Mutungi ni Msimamizi tu. Wakumbuke, hakuna Uchaguzi mwingine umefanyika toka 2020! Wasiwafanye Wananchi ni Vipofu au Viziwi. Waache hadaa. Waseme tu CCM! mfyuuuuuu
Source: Mwanahalisi Digital
 
Nadhani ilikuwa busara kuhudhuria kuliko kususa, kwani mkihudhuria mtatoa maoni yenu na kusikilizwa au hata kuchangia maoni ya wadau wengine
 
Mnyika na Lissu nawaonea huruma [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ni watu wenye integrity ya hali ya juu sana, lakini tatizo liko pale juu.

Ngoja tusikie mwanyekiti atasemaje, maana ni kama Mnyika kafanya 'preemptive strike' dhidi ya mwenyekiti.

Unadhani Mnyika anaweza kwenda kinyume na Mwenyekiti wake?
 
Mchakato wa KATIBA KUONGOZWA na mkt wa Tume ya Uchaguzi mteuliwa wa Sa100 ni MATUSI Kwa Watanzania.

Bunge lipitishe mswada wa kufufua mchakato wa KATIBA mpya ndipo Tume iteuliwe iliyo kisheria.

MUTUNGI=MUKANDALA.

Wananchi Si wajinga.

Tusubiri.
 
Kuna usemi usemao "kubali wito kataa neno".

Inawezekana kabisa shetani akawa kabeba ujumbe mzuri toka kwa roho mtakatifu.
 
Kuna usemi usemao "kubali wito kataa neno".

Inawezekana kabisa shetani akawa kabeba ujumbe mzuri toka kwa roho mtakatifu.
Rais apeleke muswada bungeni kufufua mchakato wa KATIBA mpya.

MUTUNGI anawaita wadau Ili kuwahadaa waingie uchaguzi Kwa Tume na Katiba hii hii.

Amani ni muhimu, tuidunishe Kwa kuacha hadaa.

Wananchi Si wajinga.

Tusubiri.
 
Sisi CHAUMA tunaenda na tutakaa siti za mbele. CHADEMA wanajiona spesho sana na wanataka kudekezwa kama Demu wa Chuo. Huo muda hatuna.
 
Hawa Chadema siku hizi naona wana mambo mengi ya ajabu ajabu tu, kule Mbowe yupo kwenye maridhiano, huku Mnyika anasema wamegomea wito, sasa kwanini hilo dai lao wasingempa Mbowe akaliwasilishe kwenye maridhiano lifanyiwe kazi?

Kama wanaona maridhiano hayana maana, wajitoe huko, lakini sio hivi sasa kila mmoja ana uelekeo wake, wengine kulia wengine kushoto, wafuasi nao wanaita hiyo ndio akili kubwa, kumbe kwa mtazamo wetu hata machizi nao wanaweza kuwa na akili kubwa!.

Muhimu hapa watambue jambo moja, kugoma kwasababu ya uwepo wa mtu hakuna maana yoyote, very likely anaweza kuteuliwa mwingine na Samia halafu naye akaja na mentality ile ile ya Mutungi, hivyo work done ya Chadema kumgomea Mutungi ikawa zero.

Hawa jamaa nawashauri watulize vichwa vyao watumie akili kuamua mambo yao, kugomea kila kitu wakati mwingine ni kujichelewesha mwenyewe kuwasilisha hoja/ madai yako sehemu husika ili yafanyiwe kazi.
 
Kubadilisha personality sio tatizo, hilo ni jambo la kawaida tu tena hasa kwa awamu hii ya Samia, kila siku anateua wapya.

Kama hilo ndilo dai lenu, binafsi nawapa pole sana, hiyo sura mnayotaka ibadilishwe itabadilishwa na bado huyo atakayekuja atakuwa na mawazo ya Mutungi pia, sababu wote bosi wao ni mmoja.
 
Hapo anayegomewa ni Mbowe siyo Jaji Mutungi
 
Kwani wasipokwenda chadema inapunguza nini. Chadema imebaki jina tu. Wao la msingi ni kuhakikisha kuna migogoro ila sio kuitatua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…