Mo Aache Ushikaji Amfukuze haraka Sana Try Again asihusike kwenye Mipango ya timu msimu ujao

Robidinyo

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
4,043
Reaction score
8,686
Try Again na Kamati ya Usajili ya Simba Hawapaswi Kuhusika kwa chochote Kwenye Mipango ya Timu kwa Msimu Ujao

Huyu try Again hakuna anachojua kwenye mpira, ni kiongozi aliyehusika kuleta wachezaji wabovu ndani ya kikosi cha Simba, kaua mahusiano na wale Mawakala waliokua wanatuletea wachezaji bora na Imara, kaweka mahusiano na mawakala wapiga deal wanamletea wachezaji wabovu na wasio na Uwezo

Ikiwezekana hata bodi nzima Ivunjwe, mangungu aombwe tu kulinda heshima yake ajihuzuru

Try Again na Mangungu hawajui chochote kwenye Soka La bongo nje na ndani ya Uwanja, Inafikia hatua watu wanacheza mechi za Simba nje ya Uwanja yapo hayafanyi lolote
 
Sio rahisi kihivyo Kwa sababu na yeye yupo pale kishkaji. Watavujisha na ya kwake patachimbika
 
Mo amfukuze kama nani?
Au ndo kusema mo ashanunua team lake
Hujui Try Again kawekwa nani hapo? Na hujui mwenye mamlaka ya kumtoa hapo? Unafanya nini kwenye jukwaa la michezo
 
Kuna vitu naomba kuvijua
1) Try again ndiye anayehusika na kusajili au yule mzungu head of scouting?
2) unasema kaua mahusiano na mawakala waliokuwa wanawaletea wachezaji wazuri je hao mawakala ni wakina nani? Na sasa hivi mawakala wanaotumika ni wakina nani?
 
Sijawahi kumuona muhindi aliyewekeza kwente soko ni sawa na mchina,hawa hamaa wanadamu ya kunguni aisee..muhindi awekeze kwenye viwanda vya pili pili,biscut,juice na pipi ila mchina apambane na barabara
 
Mo ndie aliyemweka Try Again pale Simba tena bila kufuata katiba. Kwa hiyo Mo ndio anapaswa kumuondoa huyo Try Again. Mo anajulikani ni mwepesi sana kutimua wachezaji na makocha timu inapokuwa na matokeo mabaya. Lakini cha ajabu inapofika kumtimua Try Again Mo ameufyata na anapata kigugumizi. Kuna siri gani ambayo Try Again anaijua dhidi ya Mo kiasi Mo anaogopa kumtimua?

Mangungu yeye amewekwa na wanachama na wanachama ndio wanye uwezo wa kumuondoa kupitia mkutano. Wanachotakiwa wanachama ni kujikusanya kuandaa barua na saini zao waushinikize uongozi uitishe mkutano wa dharura na ukigoma waiombe serikali kupitia BMT na wizara inayohusika na michezo iwaamuru viongozi waitishe mkutano kwa lazima ili wafanye maamuzi juu ya uongozi wao.

Wapenzi, wanachama na mashabiki wa Simba wajue wazi huyo Try Again na Mangungu wasipoondoka sasa hivi kabla ligi haijaisha basi wajiandae kwa maumivu makubwa msimu ujao. Hao viongozi wamefeli kwa kila kitu kiasi makombe yote yameondoka. Ni vema hata wao wenyewe waone aibu waondoke wawapishe watu wengine kwani kufeli sehemu fulani ni jambo la kawaida katika maisha yetu kama wanadamu.

Leo narudia tena ili Simba ifanikiwe mwakani ni lazima usajili wa kwanza uwe kusajili viongozi wapya na kuwaondoa Mangungu na Try Again. Hilo likishindikana basi hata usajili wa wachezaji wapya wazuri au hata kuwazuia wachezaji wazuri wa zamani wasiondoke itakuwa ngumu sana kwa Simba. Sasa hivi timu kubwa zimeshaanza usajili na maandalizi ya msimu ujao wakati Try Again na Mangungu wako "busy" wanabishana na Kibu juu mkatba mpya na huku wanajiuliza juu ya Saidoo. Hivi kweli timu kubwa kama Simba ndio imefikishwa katika hali hii na hao viongozi wawili. Hapana inahitajika mabadiliko ya uongozi haraka sana.

Ni mtizamo tu.
 
Sidhani kama inawezekana maana tumesema Sana.
 
Pole sana mkuu, wana simba wote tunafeel unachokisema. Believe me this time Mo ataingia mwenyewe kwenye usajili wa wachezaji huyo jaribu tena anawekwa kuwa mtazamaji tu. Kingine hii ndio hulka ya Mo, amebana fungu makusudi ili timu iyumbe then atatumia karata hiyo kuirudisha timu kwenye mstari ili yeye aabudiwe.

Unaikumbuka huu msemo miaka michache tuu hapo nyuma?
1. B20 haijawekwa mtani kala 4
2. B20 haijawekwa nimechukua ubingwa mfululizo
3. B20 haijawekwa nacheza robo klab bingwa
4. B20 haijawekwa nimemfunga alhly
5 B20 haijawekwa n.k n.k n.k

Hivo ndivyo Mo anavotaka.
 
Umenena vyema mkuu
 
Mo ndio kirusi no 1 Tena ana watu wake mtandaoni anawalipa wamtetee si muda mrefu utawaona.
 
Ila wakati mnawasajili hao wachezaji wenu, huwa mnawamwagia magunia ya sifa mpaka basi! Huku mkiponda usajili wa Yanga!

Na mambo yakianza kugeuka kwa upande wenu, story kama hizi sasa ndiyo zinaanza kutawala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…