SIMBA NA YANGA Tuachane kabisa na Matajiri hawa wenye mrengo wa CCM Au hata wa Vyama vingine vya Siasa... wote ni wapenzi na washabiki wa kutupwa wa CCM ..Tuachane kabisa kuuza timu au kukodisha hizi timu ambazo zinaunganisha Watanzania wote bila ya kujali tofauti za Kisiasa au Dini Kuna Hatari zake.
Nitakupeni Mfano wa wazi.
Kabla Ya Uchaguzi wa Kwanza wa Vyama vingi Kule Zanzibar Football ilipanda Juu sana. Timu za Zamani kama
Malindi
Miembeni
Vikokotoni
Kikwajuni
KMKM
Jamhuri
na zile Mpya kama
Small Simba
Black Fighters
Annur
Shangani nk
zilikua katika hali ya kiwango cha Juu na kuweza kutoa wachezaji wengi wazuri kwenye timu Ya Taifa Stars...
Malindi mwaka 1994 ilikua chini ya Mohammed Raza Na Naushad, Mwana CCM kINDAKI NDAKI...iliweza kusajili wchezaji wazuri na makocha wa nje. Ilifanikiwa Kuingia Fainali ya FA la Africa...
Baadhi ya Timu Hizi zimewahi kuchukua Ubigwa wa Tanzania Wakati ule Ligi ni Moja
Small Simba nayo ilikuwa chini ya Raza mdogo
nazo Timu za Shangani , Annur zilipata Ufadhili wa Matajiri wa CCM...Zote zilikuja Juu.
Ukaja Uchaguzi 1995 Na majimbo haya ambayo timu hizo zipo kwa bahati nzuri yaka chukuliwa na CUF.... Hawa wafadhili wakapata pressure na hatimae wakkaacha kufadhili hizi timu...Hatua Hii haikutarajiwa kabisa na hizi timu waliwaachia hawa wafadhili kila kitu ...hizi Timu zikafa kabisa na kushuka Daraja.. Hili likaleta athari kubwa ya Football Zanzibar. ..Kila Mtu atakubali kuwa hali ya Football zanzibar iko chini sana , imeanguka kweli kweli...Sasa hivi hakuna Small Simba wala Malindi wala Miembeni....Sasa hivi Mpira Zanzibar Unachezwa hivo hivo na Timu za Majeshi. Kuna
Mafunzo
Kmkm
JKU
Na Timu ya CCM Valantia au Green Guards....nao hawachezi mpira ..wanajitoa majasho tu kusukuma siku.
Hivyo Tusifanye Makosa hatua hizi zinaweza kuja angusha kabisa Mpira wa Tanzania. Siasa zetu bado sio zile zilizokomaa sana..
Tujifunze na Kusoma Ilikuwaje Simba..Ikagombana na Hatimae Ikagawanyika na Kuundwa RED STARS
Na ilikuwaje Yanga Ikavurugika na kugawanyika na Kuzaliwa PAN AFRICAN......
Pia someni Historia ya Cosmopolitan. Cosmo Ilikua Timu moja Kongwe zaidi na ilokuwa na ushawishi zaidi ya Simba na Yanga Miaka Ya nyuma. Ilikua na Uhusiano Maalum na Timu Kongwe ya Vikokotoni Zanzibar..Hizi Timu zote zilikua zikiongozwa na Ndugu wawili wa Kizanzibari Mansour Magram alikua Cosmo na Said Magram alikua Kocha wa Vikokotoni. Wakati huo huo Mzanzibari mwengine Abdalla Khalifa Salim ( Kinara) ndie alikua Rais wa Cosmo
Cosmo iliporomoka....Karume hakua anaipenda Vikokotoni Akaziwezesha Simba na Yanga....Cosmo Ikabaki kwenye vitabu vya historia.
Pia tusome Kisa na uhusiano wa Mwalimu na Tabu Mangara ..mara baada ya Ile Mechi Maarufu ya Yanga na Simba Kule Nyamagana Mwanza
Moja ya sababu ya migongano hiii ilikua ni Siasa......
kwa heshima na mtag mwanahistoria maarufu nae kama atatusaidia namna gani siasa ziliathiri maendeleo ya mpira Tanzania.
Mohamed Said
HISTORIA NI MWALIMU MZURI