Mo Dewji aanzisha petition ya kumuomba Rais Magufuli kubadili jina la Uwanja wa Taifa kuwa Uwanja wa Benjamin Mkapa

Mo Dewji aanzisha petition ya kumuomba Rais Magufuli kubadili jina la Uwanja wa Taifa kuwa Uwanja wa Benjamin Mkapa

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Anaandika Mo Dewji:-Leo nimeamua kuanzisha petition (maombi) kwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Magufuli kubadili jina la Uwanja wa Taifa kuwa: Uwanja wa Benjamin William Mkapa.

Amesema Itakuwa ni heshima kubwa kama uwanja wetu pendwa utaitwa jina la Uwanja wa Benjamin William Mkapa. Tunamuomba Rais John Pombe Magufuli aridhie kubadili jina la uwanja huo kwa heshima ya Hayati Mkapa ili tuendelee kumkumbuka kwa mchango wake mkubwa na hasa kwa vizazi vijavyo.

Tunawaomba Watanzania wote bila kujali ushabiki wa klabu muunge mkono kwa kuweka sahihi ili tumuombe Mhe Rais kubadilisha jina la uwanja huo uitwe Benjamin William Mkapa Stad.

Ujenzi wa Uwanja wa Taifa wa jijini Dar es Salaam ulianzishwa na Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa. Uwanja huo wenye uwezo wa kubeba mashabiki 60,000 ni miongoni mwa viwanja bora katika bara la Afrika kwa sasa.

Uwanja huo kwa namna mmoja au nyingine umesaidia kuendeleza mpira wa miguu na michezo mingine nchini Tanzania. Uzuri na ukubwa wa soka letu umedhihirishwa kwa sababu ya uwanja wetu huo ambao unashika nafasi ya 11 kwa ukubwa Afrika.
 
Huu unafiki mkubwa..
Alikuepo hai wakati serikali inatafuta jina..
Iliwahi pendekezwa jina la Mkapa ..watu
Wakajibu Kwa kashfa sana..

Sasa keshakufa ndo muanze kumpa jina
Hata hatajua kumbe mlimpa heshima hiyo..
Huu ni unafiki mkubwa
 
Kwani si ndiyo kunaitwa kwa Mkapa tokea zamani. Tena watu waliita kwa mchina,serikali ikawaambia unaitwa Mkapa.

Kwa mchina ilikuwa nickname, jina rasmi la uwanja ni Uwanja wa Taifa

Stadium.jpg
 
Sio wazo baya, lakini marehemu aligoma akiwa hai uwanja huo kuitwa jina lake. Ni vyema hiyo petition angeifanya Mkapa akiwa hai, ili muhusika atoe uamuzi kuwa alikuwa anaridhia uwanja huo uitwe jina lake. Asipokuwa makini kuna watu huko pemba wanaweza kutaka mauaji yao ya mwaka 2001, yaitwe mauaji ya Mkapa.

Nadhani huyo Mo anaongozwa na hisia za huo msiba. Kuna tabia watu kwenda kwenye misiba, wakifika hupata hisia kali za vilio vya wafiwa, kwa ajili ya msukumo wa hisia, hutoa ahadi mbele ya waombolezaji kuwa watasomesha watoto wote wa marehemu. Lakini baada ya hisia kushuka huwa hawatekelezi ahadi zao. Nadhani Mo yuko kwenye hali hiyo.
 
Kwani si ndiyo kunaitwa kwa Mkapa tokea zamani. Tena watu waliita kwa mchina,serikali ikawaambia unaitwa Mkapa.
Sio official Madam, maana ukifika pale uwanjani umeandikwa uwanja wa taifa, na sio uwanja wa Mkapa. Huku mitaani walikua wanaita kwa mchina kwa mchina, ndipo Mwakyembe akasema kuliko mpaite kwa mchina kheri mpaite kwa Mkapa, lakini haijawa official bado.
 
Sio wazo baya, lakini marehemu aligoma akiwa hai uwanja huo kuitwa jina lake. Ni vyema hiyo petition angeifanya Mkapa akiwa hai, ili muhusika atoe uamuzi kuwa alikuwa anaridhia uwanja huo uitwe jina lake. Asipokuwa makini kuna watu huko pemba wanaweza kutaka mauaji yao ya mwaka 2001, yaitwe mauaji ya Mkapa.

Nadhani huyo Mo anaongozwa na hisia za huo msiba. Kuna tabia watu kwenda kwenye misiba, wakifika hupata hisia kali za vilio vya wafiwa, kwa ajili ya msukumo wa hisia, hutoa ahadi mbele ya waombolezaji kuwa watasomesha watoto wote wa marehemu. Lakini baada ya hisia kushuka huwa hawatekelezi ahadi zao. Nadhani Mo yuko kwenye hali hiyo.

Hisia mhemuko ndo hizi
 
Huu unafiki mkubwa..
Alikuepo hai wakati serikali inatafuta jina..
Iliwahi pendekezwa jina la Mkapa ..watu
Wakajibu Kwa kashfa sana..

Sasa keshakufa ndo muanze kumpa jina
Hata hatajua kumbe mlimpa heshima hiyo..
Huu ni unafiki mkubwa
Haa ila kweli funzo nikwamba watu wanakumbuka mazuri unapokuwa umekufa
 
Hilo lilishapitishwa na serikali halihitaji maombi ya mtu.

Yeye aende uwanjani akampokee mwana Singida Tundu Lisu!
 
Rais ndio ana mandate ya kubadilisha majina ? Haya mambo ya kupeana kazi nyingine kwa mtu mmoja ndio kunapelekea huyo kuzidiwa na kazi
 
Back
Top Bottom