Mo Dewji kamzidi vipi Bakhresa kwa Utajiri?

Mwanaume kuanza kubishania utajili wa watu wengine si dalili njema.

Jitafakari, labda kama wewe ni jinsia ya kike basi uko sahihi hakuna shida.
 
Mo anahesabika ni Tajiri sababu anakopa sana kwenye mabenki ya nje, Bakhressa yeye hakopi hivyo ni ngumu kutambulika kwenye hayo majarida sababu dhamana zake hazijulikani

Mo anaonyesha mashamba ya mikonge, kahawa, pamba ambayo alipewa serikalini kifisadi ndio anachukulia mikopo huko duniani pamoja na viwanda kibao ambavyo haviendelezi..... kwenye utajiri wake wanahesabia kama mali zake binafsitu hata kama hayaendelezi.

Ndio maana kwenye uwekezaji wa Simba janja janja nyingi lakini mpunga haweki.

Bakhressa yeye no janja janja, pesa ipo.
 
Kwanza huyo Mo ni msimamizi wa Kampuni za familia yake anakuwaje tajiri kwa mali ambazo sio za kwake??
 
Hii mada itakuwa na upinzani mkali kati ya Waislamu wa madhehebu ya Sunni vs Shia.
 
hizi taarifa za Forbes zinauhakika? ama wanazitoa wapi?
 
Bakhresa ana hela chafu ni mwisho! Ukifika tu alipojenga hotel yake kule Zanzibar hakika Mwamedi utamfuta! Uwekezaji aliouweka pale Verde Hotel ni hatari kabisa!
 
Huna ushahidi wa vyote ulivyoandika.
 
Kama Mo energy ni uchafu mbele ya Azam energy
Mwanangu ilie Mo energy naielewa kuliko ile ya bakhresa japo naunga mkono [emoji1666] uzi.
Muddy ni mbabaishaji tu hana pesa ya kumzidi bakhresa.
 
Usicomplicate sana mambo ya duniani mzee baba!

Kuna stori zingine mtu mnapiga just kujifurahisha na kupumzisha akili baada ya majukumu mazito.

Unataka vitu vyote duniani viwe realy, hakuna fun hakuna burudani siyo?

Nikuulize, ukikuta watu wasio wachezaji wanjadili soka, huwa unawadharau sana'eeh?

Wafanyie utafiti wa mmoja mmoja, uone kama wote hao wewe unawazidi maendeleo just kwa sababu wanajadili kisichowalipa!

Kwani kila mjadala hata humu Jf lazima ukunufaishe na kukuingizia kipato?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utajiri wa Mwamedi ni wa Chupli Chupli tu....
Mafaniko ya Simba ya miaka minne ni ya Chupli Chupli tu..
Biashara zake zinaendeshwa kiChupli Chupli tu..
Mishahara kwa wafanyakazi wake ni ya kichupli Chupli tu..

So Mwamedi ni Mr Chupling.
 
Ninavyoelewa ili utolewe maelezo yako Forbes, ni lazima uwalipe. Hawatakujia, Ila wewe utawafuata. Hivyo wataandika ulichowapa waandike na hawajisumbui kujua kama kuna anayekuzidi au la, mpaka huyo mwingine naye awalipe. No biashara, ukiitangaza, lazima ulipie.
 
Forbes na Bloomberg hiyo ni kazi/biashara yao na wanalipwa kwa hizo tafiti au data wanazokusanya na wanaaminika kwa ukweli wao ili kuwawezesha wawekezaji wengine kutambuana

Sasa wewe T14 Armata na LICHADI tuambie mnafaidikaje ? na sisi tujifunze ?
Nani anawalipa forbes mkuuu?

Sent from my SM-G955F using JamiiForums mobile app
 
Hapa ukija kuangalia zaidi utaona kuna usimba na uyanga. Mo ana viwanda vingi Africa kuliko Bakhresa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…