MO Dewji: Tunahitaji Yanga SC imara ambayo inaweza kushindana na Simba SC

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Mfanyabiashara maarufu Tanzania, Mohammed Dewji 'MO' ameguswa na hali ya sintofahamu inayoendelea kwenye klabu ya Yanga na kuwaombea waweze kupita katika kipindi hicho kigumu kwao huku akiwataka watulie kisha waungane upya.

MO kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika kwamba "Tunahitaji Yanga imara ambayo inaweza kushindana na Simba. Tunahitaji Yanga imara kwa ajili ya timu bora ya Taifa Stars. Ninawaombea Yanga waweze kupita katika kipindi hiki kigumu kwao, wanapaswa watulia na waungane upya". Ameandika MO Dewji.
 
Wahame ule mtaa kwanza... Wasing'ang'anie sehemu ambayo haina baraka
 
Kauli zake ni nzuri. Yanga ikiwa mbovu hata washabiki viwanjani watapungua, tunahitaji ushindani uwepo kwa Simba na Yanga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…