Ab-Titchaz
JF-Expert Member
- Jan 30, 2008
- 14,630
- 4,253
Mohamed Ali: Barua kwa Duale, Moses Kuria, Mutahi Ngunyi na wenzao
Je, wataka kuwa maarufu Kenya? Ni rahisi kabisa - unga viongozi pamoja na serikali mkono.
Bora wakishuta wasifu kwa kusema ni harufu ya marashi, walimbikizie sifa wakituhumiwa kuiba, sifu kabila zao na wake zao, heshimu maamuzi ya mipango yao ya kando serikalini.
Ukifanya hivyo, bilashaka utaogopewa na kila mtu kwani sheria yao itakukinga.
Ukipenda, fungua hospitali kisha uwabake wanawake wanaotafuta matibabu, simama kwenye jukwaa na useme kabila fulani likatwe kwa upanga likipinga mwito wa serikali iliyo madarakani, watusi kwa kuwaita maskini baada ya serikali hiyo hiyo unayoabudu kuwafilisi raia wake, kuwa mbunge na ubake ndani ya ofisi yako kwani sheria ni ya mama zenu si yetu sote, tena waite viongozi wadini kwa kigezo cha kuombea taifa baada ya kufanya maasi kwa wananchi wako, cheza na jina la Mungu kila kukicha kwani mungu wako ni senti, simama imara na serikali kisha vunja sheria. Hakika utalindwa.
Kenya hamna sheria. Wakenya watakumbuka jinsi mahakama ya Willy Mutunga mnamo mwaka wa 2013 ilivyotoa uamuzi wa dakika tatu dhidi ya kesi ya uchaguzi iliyo wasilishwa na upande wa Cord. Ndio, dakika tatu! Sisemi majaji hao walikosea, bali kutoa maamuzi ya taifa kwa dakika tatu ni sawia na kutwanga maji kwenye kinu.
Daktari Willy Mutunga sasa kiza kinene kimetunga mithili ya ukungu. Haiheshimiwi tena, ni sawia na simba wa matopeni anayeteleza ovyo ovyo. Wakenya waliheshimu maamuzi yenu, lakini sasa waliotangazwa washindi hawaheshimu maamuzi mliotoa kuhusu waalimu.
Moses Kuria
Sitaki kumwita mheshimiwa kwani vitendo vyake na matamshi yake si vya kiheshimiwa. Waliomchagua na wamwite mheshimiwa, mimi simo. Kumbuka nchi hii itakapoteketea kwa sababu ya matamshi kama yako, hata shetani hatakuwa na wasaa wa kusikia umaarufu wako wa kuwatenganisha Wakenya. Iko siku haki itashinda na hiyo ndio siku utakapojua tofauti ya kuvua chupi na kuvua samaki.
Mutahi Ngunyi
Sisi ni maskini. Tumesalitiwa na serikali, tumeibiwa na kudhalilishwa na hiyo hiyo serikali unayoabudu. Lakini, kumbuka aliyekupa wewe ndiye aliyeninyima mimi. Itakuwaje Mutahi atutusi kisha atualike kunywa pombe naye? Kumbuka dawa ya maskini si pombe, bali chakula. Kama wataka kufanya ukuruba na sisi, iambie serikali ipunguze bei ya vyakula ikiwemo maziwa ili watoto wetu wafaidi. Pia serikali ambayo unaitetea sana, iambie maafisa wake waache kutumia nguvu za bunduki kuwaua vijana ovyo ovyo, na maafisa wakome kupora mali ya umma. Usisahau kueleza kuhusu walanguzi wa dawa za kulevya, sio kuwahangaisha wateja. Pitisha ujumbe kuwa vijana hawana ajira na uchumi umezidi kuzorota - shilingi ya Kenya imefika 107 dhidi ya dola ya Merekani.
Ukifikisha salamu hizi, basi sisi maskini hatutaki pombe yako, hatutaki kuleweshwa kisha mali yetu kuibiwa tukiwa ulevini. Sisi hatuna kinyongo nawe, lakini tutakusamehe na umaskini wetu kwani sisi ni maskini lakini wakubwa kimapenzi moyoni.
Aden Duale
Juzi nilikuona ukijipiga kifua na kutetea viranja wa Jubilee na kusahau wana-Garissa hawana vitambulisho, vijana wanatekwa nyara na watu wanaodaiwa kuwa maafisa wa polisi na kuuawa, hamna waalimu Garissa na Mandera. Mtihani unabisha hivyo jitayarishe kuwa na vizazi visivyo na elimu kwa sababu umefeli kuwashughulikia waliokuchagua na badala yake kupiga domo ukiitetea serikali.
Kipchumba Murkomen
Ni hatari sana msomi anayefahamu sheria kwenda kinyume na sheria. Kumbuka kuwa siasa sio mchezo mchafu, bali mtu binafsi ndiye mwenye siasa chafu. Kuwa kibaraka sio dhambi, lakini kujidhalilisha ndio dhambi kuu. Tumewaona wanasiasa wengi, makalulu na wenye vihoja chungu nzima. Leo hawapo tena. hata chama ambayo kwao ilikuwa kama baba na mama haipo tena.
Kumbuka, wanaotawala sasa ni Wakenya kwa nguvu za Rabuka ambaye leo kila mtu anacheza na jina lake.
Mbona sikukuona ukiwaombea waliouawa na wakimbizi wa ndani kwa ndani? Mungu atatulipia sisi wanyonge, Mungu atasikia maombi yetu na ya wale waliouawa mwaka wa 2007. Hatutaombea kabila hili wala lile, bali tutaombea makabila yote kwa maana sisi twaabudu Mungu aliye mkuu. Kipchumba Murkomen Mungu ni mkuu.
Mohammed Ali ni Mhariri Mkuu wa Kitengo cha upekuzi KTN.
Wasiliana naye kupitia thenairobian@standardmedia.co.ke ama mali@standardmedia.co.ke. Unaweja pia kujumuika naye katika mitandao ya kijamii - Facebook: Official Jicho Pevu with Mohammed Ali, Twitter: Mohajichopevu
http://www.sde.co.ke/thenairobian/a...-moses-kuria-mutahi-ngunyi-na-wenzao?pageNo=2
Je, wataka kuwa maarufu Kenya? Ni rahisi kabisa - unga viongozi pamoja na serikali mkono.
Bora wakishuta wasifu kwa kusema ni harufu ya marashi, walimbikizie sifa wakituhumiwa kuiba, sifu kabila zao na wake zao, heshimu maamuzi ya mipango yao ya kando serikalini.
Ukifanya hivyo, bilashaka utaogopewa na kila mtu kwani sheria yao itakukinga.
Ukipenda, fungua hospitali kisha uwabake wanawake wanaotafuta matibabu, simama kwenye jukwaa na useme kabila fulani likatwe kwa upanga likipinga mwito wa serikali iliyo madarakani, watusi kwa kuwaita maskini baada ya serikali hiyo hiyo unayoabudu kuwafilisi raia wake, kuwa mbunge na ubake ndani ya ofisi yako kwani sheria ni ya mama zenu si yetu sote, tena waite viongozi wadini kwa kigezo cha kuombea taifa baada ya kufanya maasi kwa wananchi wako, cheza na jina la Mungu kila kukicha kwani mungu wako ni senti, simama imara na serikali kisha vunja sheria. Hakika utalindwa.
Kenya hamna sheria. Wakenya watakumbuka jinsi mahakama ya Willy Mutunga mnamo mwaka wa 2013 ilivyotoa uamuzi wa dakika tatu dhidi ya kesi ya uchaguzi iliyo wasilishwa na upande wa Cord. Ndio, dakika tatu! Sisemi majaji hao walikosea, bali kutoa maamuzi ya taifa kwa dakika tatu ni sawia na kutwanga maji kwenye kinu.
Daktari Willy Mutunga sasa kiza kinene kimetunga mithili ya ukungu. Haiheshimiwi tena, ni sawia na simba wa matopeni anayeteleza ovyo ovyo. Wakenya waliheshimu maamuzi yenu, lakini sasa waliotangazwa washindi hawaheshimu maamuzi mliotoa kuhusu waalimu.
Moses Kuria
Sitaki kumwita mheshimiwa kwani vitendo vyake na matamshi yake si vya kiheshimiwa. Waliomchagua na wamwite mheshimiwa, mimi simo. Kumbuka nchi hii itakapoteketea kwa sababu ya matamshi kama yako, hata shetani hatakuwa na wasaa wa kusikia umaarufu wako wa kuwatenganisha Wakenya. Iko siku haki itashinda na hiyo ndio siku utakapojua tofauti ya kuvua chupi na kuvua samaki.
Mutahi Ngunyi
Sisi ni maskini. Tumesalitiwa na serikali, tumeibiwa na kudhalilishwa na hiyo hiyo serikali unayoabudu. Lakini, kumbuka aliyekupa wewe ndiye aliyeninyima mimi. Itakuwaje Mutahi atutusi kisha atualike kunywa pombe naye? Kumbuka dawa ya maskini si pombe, bali chakula. Kama wataka kufanya ukuruba na sisi, iambie serikali ipunguze bei ya vyakula ikiwemo maziwa ili watoto wetu wafaidi. Pia serikali ambayo unaitetea sana, iambie maafisa wake waache kutumia nguvu za bunduki kuwaua vijana ovyo ovyo, na maafisa wakome kupora mali ya umma. Usisahau kueleza kuhusu walanguzi wa dawa za kulevya, sio kuwahangaisha wateja. Pitisha ujumbe kuwa vijana hawana ajira na uchumi umezidi kuzorota - shilingi ya Kenya imefika 107 dhidi ya dola ya Merekani.
Ukifikisha salamu hizi, basi sisi maskini hatutaki pombe yako, hatutaki kuleweshwa kisha mali yetu kuibiwa tukiwa ulevini. Sisi hatuna kinyongo nawe, lakini tutakusamehe na umaskini wetu kwani sisi ni maskini lakini wakubwa kimapenzi moyoni.
Aden Duale
Juzi nilikuona ukijipiga kifua na kutetea viranja wa Jubilee na kusahau wana-Garissa hawana vitambulisho, vijana wanatekwa nyara na watu wanaodaiwa kuwa maafisa wa polisi na kuuawa, hamna waalimu Garissa na Mandera. Mtihani unabisha hivyo jitayarishe kuwa na vizazi visivyo na elimu kwa sababu umefeli kuwashughulikia waliokuchagua na badala yake kupiga domo ukiitetea serikali.
Kipchumba Murkomen
Ni hatari sana msomi anayefahamu sheria kwenda kinyume na sheria. Kumbuka kuwa siasa sio mchezo mchafu, bali mtu binafsi ndiye mwenye siasa chafu. Kuwa kibaraka sio dhambi, lakini kujidhalilisha ndio dhambi kuu. Tumewaona wanasiasa wengi, makalulu na wenye vihoja chungu nzima. Leo hawapo tena. hata chama ambayo kwao ilikuwa kama baba na mama haipo tena.
Kumbuka, wanaotawala sasa ni Wakenya kwa nguvu za Rabuka ambaye leo kila mtu anacheza na jina lake.
Mbona sikukuona ukiwaombea waliouawa na wakimbizi wa ndani kwa ndani? Mungu atatulipia sisi wanyonge, Mungu atasikia maombi yetu na ya wale waliouawa mwaka wa 2007. Hatutaombea kabila hili wala lile, bali tutaombea makabila yote kwa maana sisi twaabudu Mungu aliye mkuu. Kipchumba Murkomen Mungu ni mkuu.
Mohammed Ali ni Mhariri Mkuu wa Kitengo cha upekuzi KTN.
Wasiliana naye kupitia thenairobian@standardmedia.co.ke ama mali@standardmedia.co.ke. Unaweja pia kujumuika naye katika mitandao ya kijamii - Facebook: Official Jicho Pevu with Mohammed Ali, Twitter: Mohajichopevu
http://www.sde.co.ke/thenairobian/a...-moses-kuria-mutahi-ngunyi-na-wenzao?pageNo=2