Mohamed Dewji Tsh 20 bilioni naweza kununua timu Ulaya

Mohamed Dewji Tsh 20 bilioni naweza kununua timu Ulaya

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
CowgvwPW8AAfHel.jpg


Leo Jumatatu, Agosti,1 mfanyabiashara bilionea Mohamed Dewji alikuwa na mkutano na waandishi wa habari, akasema uwekezaji wa 20 bilioni anaotaka kuufanya angeweza kununua timu Ulaya ya daraja la pili lakini anafanya sababu ya mapenzi yake kwa timu ya Simba.

Pia akakosoa shutumia alizotupiwa na viongozi wa Simba na kusema ameshakutana zaidi ya mara tatu na rais wa Simba na ameshakuja ofisini kwake zaidi ya mara tatu.
 
Tuache ulimbukeni. Timu za Tanzania zinahitaji watu kama Mo.
Tunapaswa kubadilika. 20b ni pesa nyingi hapa kwetu
Kama unasema timu sasa zinamhitaji mtu kama Mo kwa hiyo wewe hazikuhitaji!?
 
Mimi timu inanihitaji sana na watu makini wenye pesa na utaalam timu inawahitaji
 
Angeweza kununua huko ulaya lakini biashara zake ziko hapa Bongo.
So akinunua hapa atapata mwanya wa kukuza brand zake za 'Mooo'...
 
Limbukeni ni wewe unayedhani timu ni Simba tu. Si anunue Maji Maji au Toto Africa!
Nafikiri uwezo wako wa kusoma na kuelewa kiswahili ni mdogo sana. Mimi nimesema timu za Tanzania zinawahitaji watu kama Mo. Sijasema Simba ndo timu peke yake mkuu. Jaribu kuacha jazba kama siyo lazima.
Kama unasema timu sasa zinamhitaji mtu kama Mo kwa hiyo wewe hazikuhitaji!?
 
Nafikiri uwezo wako wa kusoma na kuelewa kiswahili ni mdogo sana. Mimi nimesema timu za Tanzania zinawahitaji watu kama Mo. Sijasema Simba ndo timu peke yake mkuu. Jaribu kuacha jazba kama siyo lazima.
Usije ukafikiri niliteleza au sikukuelewa. Wenye timu si wanaona wanajimudu? Kinamshinda nini Mo kununua isiyojimudu kama nia yake ni mpira wa Tanzania kukua? Mimi nilikujibu kwa muktadha wa why Simba.

Yeye aseme ana agenda gani. Kama ni timu ziko nyingi tu akanunue aoneshe namna fedha zake zinavyoweza kuleta mabadiliko.
 
Mimi nafikiri hatutofautiana sana mawazo kuhusu uwekezaji kwenye timu zetu ; ila uhuru wa mtu huwezi kuungilia. Kama unafuatilia hata wawekezaji kwenye timu za huko nje huwa wanawekeza kwenye timu wanazozipenda au ambazo zitawarudishia faida haraka. Lengo la mfanyabiashara ni kupata faida. Sasa brand ya timu kama majimaji utailinganisha na brand ya Simba au Yanga?
 
Hivi ile timu yake iliishiaga wapi?,kwanza aueleze uma kwanini ilikufa
 
Back
Top Bottom