R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,575
BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma limeiomba serikali ichukue hatua za sheria kwa kampuni ya Mohamed Enterprises tawi la Songea kwa kile lililochodai kuwauzia wakulima mbolea inayosadikiwa ni feki. Madiwani hao pia wametaka kampuni hiyo iwalipe fidia baadhi ya wakulima kwa kuwasababishia hasara katika msimu wa kilimo wa 2012/13.
Ombi hilo walilitoa katika kikao juzi juzi ambako pia waliwataka meya na mkurugenzi kutoa maelezo yanayojitosheleza kwenye baraza hilo kuhusu hatua zilizokwisha kuchukuliwa kwa kampuni Mohamed Enterprises.
Akizungumza katika kikao hicho, Diwani wa Kata ya Ruhuwiko, Gerad Ndimbo (CCM) alisema anashangazwa mbolea hiyo feki haijateketezwa hadi sasa.
Mbolea hiyo ni sumu hivyo haikutakiwa iendelee kuwapo hadi sasa ikizingatiwa kuwa haijulikani ni kiasi gani kilichomo katika maghala.
Naye Diwani wa Kata ya Bombambili , Keni Mbangala (Chadema) alilitaka baraza hilo kwenda kukagua maghala ya kampuni hiyo kujionea ukweli wa suala hilo kuepusha wananchi kuendelea kutumia mbolea feki.
Diwani wa Kata ya Msamala, Khalifa Mgwasa (CCM) alipendekeza zichukuliwe hatua za sheria ikiwa ni pamoja na kuifungia kampuni hiyo kupeleka mbolea Songea.
Hata hivyo, Meya wa Halmashauri ya Manispaa hiyo, Charles Mhagama alisema halmashauri haina uwezo wa kuibana hiyo kampuni hiyo.
Alisema suala hilo kwa sasa liko ngazi ya mkoa na kinachosubiriwa ni majibu.
Akizungumzia suala hilo, Mkuu wa Wilaya hiyo, Joseph Mkirikiti alisema shauri hilo lilikwisha kufanyiwa utafiti wa kina na mwenye kampuni akapewa nafasi ya kujitetea.
DC alisema serikali ilichukua sampuli ya mbolea hiyo kwenda kuifanyia utafiti na kuipima kama inafaa kwa matumizi ya kilimo.
Alipohojiwa, mwakilishi wa kampuni hiyo mkoani Ruvuma, Sadiki Mpemba alipohojiwa na waandishi wa habari alisema hafanyii kazi za majungu za wanasiasa na waandishi.
Ombi hilo walilitoa katika kikao juzi juzi ambako pia waliwataka meya na mkurugenzi kutoa maelezo yanayojitosheleza kwenye baraza hilo kuhusu hatua zilizokwisha kuchukuliwa kwa kampuni Mohamed Enterprises.
Akizungumza katika kikao hicho, Diwani wa Kata ya Ruhuwiko, Gerad Ndimbo (CCM) alisema anashangazwa mbolea hiyo feki haijateketezwa hadi sasa.
Mbolea hiyo ni sumu hivyo haikutakiwa iendelee kuwapo hadi sasa ikizingatiwa kuwa haijulikani ni kiasi gani kilichomo katika maghala.
Naye Diwani wa Kata ya Bombambili , Keni Mbangala (Chadema) alilitaka baraza hilo kwenda kukagua maghala ya kampuni hiyo kujionea ukweli wa suala hilo kuepusha wananchi kuendelea kutumia mbolea feki.
Diwani wa Kata ya Msamala, Khalifa Mgwasa (CCM) alipendekeza zichukuliwe hatua za sheria ikiwa ni pamoja na kuifungia kampuni hiyo kupeleka mbolea Songea.
Hata hivyo, Meya wa Halmashauri ya Manispaa hiyo, Charles Mhagama alisema halmashauri haina uwezo wa kuibana hiyo kampuni hiyo.
Alisema suala hilo kwa sasa liko ngazi ya mkoa na kinachosubiriwa ni majibu.
Akizungumzia suala hilo, Mkuu wa Wilaya hiyo, Joseph Mkirikiti alisema shauri hilo lilikwisha kufanyiwa utafiti wa kina na mwenye kampuni akapewa nafasi ya kujitetea.
DC alisema serikali ilichukua sampuli ya mbolea hiyo kwenda kuifanyia utafiti na kuipima kama inafaa kwa matumizi ya kilimo.
Alipohojiwa, mwakilishi wa kampuni hiyo mkoani Ruvuma, Sadiki Mpemba alipohojiwa na waandishi wa habari alisema hafanyii kazi za majungu za wanasiasa na waandishi.