Mohamed Omari Mkwawa (Tindo) na Mapinduzi ya Zanzibar 1964

Mohamed Omari Mkwawa (Tindo) na Mapinduzi ya Zanzibar 1964

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1547224643191.png


Mzee Mohamed Omari Mkwawa au kwa jina lingine Tindo alilopewa na Karume wakati wa harakati za ukombozi Zanzibar katika miaka ya 1950 amefariki dunia usiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili tarehe 5 May 2015 nyumbani kwake Mwahako Tanga.

Marehemu anatarajiwa kuzikwa kesho Jumatatu Tanga mjini. Mzee Mkwawa alipata umaarufu mwaka 2010 baada ya kutoka kitabu cha Dr. Harith Ghassany, “Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,” kitabu kilichokuja kueleza historia ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa usahihi kuliko vitabu vyote vilivyopata kuandikwa kabla.

Ilikuwa Mzee Mkwawa ndiye aliyefichua siri kubwa iliyokuwa imefichwa kwa miaka mingi ya jeshi la askari mamluki wa Kimakonde waliochukuliwa kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura wakapewa mafunzo katika mapori ya Kipumbwi na kuvushwa kwenda Zanzibar kusaidia mapinduzi ya tarehe 12 Januari 1964.

Mzee Mkwawa ndiye alikuwa akilivusha jeshi hili kwa majahazi kutokea Kipumbwi kwenda Zanzibar usiku wakiwa wamevaa mavazi kama wavuvi. Mzee Mkwawa alikuwa na mchango mkubwa katika kutegua kitendawili cha mchango wa Tanganyika katika Mapinduzi ya Zanzibar kiasi mwandishi Dr. Ghassany alipatapo kusema kuwa, "Ufunguo wa kitabu changu anao Mzee Mkwawa."

Hii picha ya pili hapo chini akiwa na Prof. Malima ni picha yangu ya kwanza kumpiga Mohamed Omar Mkwawa wakati wa kampeni za uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi 1995.

Mzee Mkwawa wa kwanza kushoto amevaa picha ya mgombea wa CUF Ibrahim Lipumba, Juma Duni Haji na Ibrahim Haruna Lipumba.

Hapa ni Ngamiani Tanga nyumbani kwa Mama Ummie bint Anzuani. Ilikuwa baada ya mkutano mkubwa sana Viwanja vya Tangamano ambao haujapata kutokea.

Mama Ummie mmoja wa viongozi wa juu wa CUF alitualika chai nyumbani kwake. Wakati ule sikuwa namjua Mzee Mkwawa baada ya miaka miwili 1997 ndipo tulipokuja kufahamiana wakati nilipohamia Tanga.

1547225025735.png


Hii picha nimempiga Mzee Mkwawa tarehe 29 Oktoba 2013 na ndiyo ilikuwa mara yetu ya mwisho kuonana.

Huyo nyuma ni mkewe.

Nilikwenda nyumbani kwake Tanga na mtafiti wa Kimarekani aliyetaka kufanya mahojiano na yeye.

Hili unaloona ni banda la kuku nyuma ya nyumba ya muhisani mwema ameligeuza kuwa makazi yake.

Mzee Mkwawa katika mazungumzo yetu na ndiyo yalikuwa ya mwisho baina yetu aliniambia, "Hivi kweli Mohamed katika kujitolea kwangu kote katika Mapinduzi ya Zanzibar ijaza yangu ndiyo hii mimi na mke wangu kulala kwenye banda la kuku?"

1547224891968.png
 
Dah kafia kwenye banda la kuku wakati watoto wadogo waliokuja mjini juzi kama kina Makonda wanaogelea kwenye utajiri.
 
DHAMBI YA Ya mauwaji Zanzibar 1964 imekuwa ikimtafuna
 
View attachment 991952

Mzee Mohamed Omari Mkwawa au kwa jina lingine Tindo alilopewa na Karume wakati wa harakati za ukombozi Zanzibar katika miaka ya 1950 amefariki dunia usiku wa Jumamosi kuamkia Jumapili tarehe 5 May 2015 nyumbani kwake Mwahako Tanga.

Marehemu anatarajiwa kuzikwa kesho Jumatatu Tanga mjini. Mzee Mkwawa alipata umaarufu mwaka 2010 baada ya kutoka kitabu cha Dr. Harith Ghassany, “Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru,” kitabu kilichokuja kueleza historia ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa usahihi kuliko vitabu vyote vilivyopata kuandikwa kabla.

Ilikuwa Mzee Mkwawa ndiye aliyefichua siri kubwa iliyokuwa imefichwa kwa miaka mingi ya jeshi la askari mamluki wa Kimakonde waliochukuliwa kutoka mashamba ya mkonge ya Sakura wakapewa mafunzo katika mapori ya Kipumbwi na kuvushwa kwenda Zanzibar kusaidia mapinduzi ya tarehe 12 Januari 1964.

Mzee Mkwawa ndiye alikuwa akilivusha jeshi hili kwa majahazi kutokea Kipumbwi kwenda Zanzibar usiku wakiwa wamevaa mavazi kama wavuvi. Mzee Mkwawa alikuwa na mchango mkubwa katika kutegua kitendawili cha mchango wa Tanganyika katika Mapinduzi ya Zanzibar kiasi mwandishi Dr. Ghassany alipatapo kusema kuwa, "Ufunguo wa kitabu changu anao Mzee Mkwawa."

Hii picha ya pili hapo chini akiwa na Prof. Malima ni picha yangu ya kwanza kumpiga Mohamed Omar Mkwawa wakati wa kampeni za uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi 1995.

Mzee Mkwawa wa kwanza kushoto amevaa picha ya mgombea wa CUF Ibrahim Lipumba, Juma Duni Haji na Ibrahim Haruna Lipumba.

Hapa ni Ngamiani Tanga nyumbani kwa Mama Ummie bint Anzuani. Ilikuwa baada ya mkutano mkubwa sana Viwanja vya Tangamano ambao haujapata kutokea.

Mama Ummie mmoja wa viongozi wa juu wa CUF alitualika chai nyumbani kwake. Wakati ule sikuwa namjua Mzee Mkwawa baada ya miaka miwili 1997 ndipo tulipokuja kufahamiana wakati nilipohamia Tanga.

View attachment 991965

Hii picha nimempiga Mzee Mkwawa tarehe 29 Oktoba 2013 na ndiyo ilikuwa mara yetu ya mwisho kuonana.

Huyo nyuma ni mkewe.

Nilikwenda nyumbani kwake Tanga na mtafiti wa Kimarekani aliyetaka kufanya mahojiano na yeye.

Hili unaloona ni banda la kuku nyuma ya nyumba ya muhisani mwema ameligeuza kuwa makazi yake.

Mzee Mkwawa katika mazungumzo yetu na ndiyo yalikuwa ya mwisho baina yetu aliniambia, "Hivi kweli Mohamed katika kujitolea kwangu kote katika Mapinduzi ya Zanzibar ijaza yangu ndiyo hii mimi na mke wangu kulala kwenye banda la kuku?"

View attachment 991960

Vipi mbona Field Marshal Okello hapewi sifa zake.
 
Vipi mbona Field Marshal Okello hapewi sifa zake.
Ngongo,
Alivishwa blanketi na likamuenea na akapewa cheo kuwa yeye ni Field Marsha cheo chake ni sawa na cheo cha Josip Tito wa Yugoslavia aliepigana na Wajerumani WW II.

John Okello akaamini kuwa kweli yeye ni Filed Marshall na akakipenda cheo hicho.

Akaamini kuwa yeye ndiye aliyefanya mapinduzi yale na bila yake yeye mapinduzi yasingefanyika.

John Okello hakuwa na habari ya mchango kutoka Tanganyika wala hakujua kuwa kuliingizwa askari mamluki kutoka Kipumbwi, Tanga waliokuwa wanaingizwa kwa siri wakivushwa na mtu mmoja anaitwa Mohamed Omari Mkwawa na kwa jina la harakati Mzee Karume alimpa jina la ''Tindo.''

Tindo alitiwa katika njama hii na mtu mmoja anaitwa Ali Mwinyi Tambwe.
Huyu mtu ana historianya pekee katika historia ya ujasusi Tanzania.

Wala Okello hakujua kuwa huyu Tindo alikuwa na mkubwa wake jina lake Victor Mkello aliyekuwa kiongozi wa chama cha wakata mkonge wa mashamba ya Sakura na Kipumbwi.

Ukiwaleta hawa katika historia ya mapinduzi John Okello haonekani.

Okello hawezi hata kukueleza kama alipatapo kabla ya mapinduzi kuhudhuria mkutano hata mmoja wa siri Zanzibar au Dar es Salaam uliokuwa na agenda ya Zanzibar.
 
Ngongo,
Alivishwa blanketi na likamuenea na akapewa cheo kuwa yeye ni Field Marsha cheo chake ni sawa na cheo Cha Josip Tito wa Yugoslavia aliepigana na Wajerumani WW II.

John Okello akaamini kuwa kweli yeye ni Filed Marshall na akakipenda cheo hicho.

Akaamini kuwa yeye ndiye aliyefanya mapinduzi yale na bila yake yeye mapinduzi yasingefanyika.

John Okello hakuwa na habari ya mchango kutoka Tanganyika wala hakujua kuwa kuliingizwa askari mamluki kutoka Kipumbwi, Tanga waliokuwa wanaingizwa kwa siri wakivushwa na mtu mmoja anaitwa Mohamed Omari Mkwawa na kwa jina la harakati Mzee Karume alimpa jina la ''Tindo.''

Tindo alitiwa katika njama hii na mtu mmoja anaitwa Ali Mwinyi Tambwe.
Huyi mtu ana historianya pekee katika historia ya ujasusi Tanzania.

Wala Okello hakujua kuwa huyu Tindo alikuwa na mkubwa wake jina lake Victor Mkello aliyekuwa kiongozi wa chama cha wakata mkonge wa mashamba ya Sakura na Kipumbwi.

Ukiwaleta hawa katika historia ya mapinduzi John Okello haonekani.

Okell hawezi hata kukueleza kama alipatapo kabla ya mapinduzi kuhudhuria mkutano hata mmoja wa siri Zanzibar au Dar es Salaam uliokuwa na agenda ya Zanzibar.


Kama si Mwl Nyerere Field Marshal Okello angekuwa kiongozi wa Zanzibar Karume akimwogopa ilibidi aombe msaada kwa Mwl Nyerere.
 
Leo tarehe 12 January ni Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar, nachukua nafasi hii kuwatakia nyote heri na fanaka za Mapinduzi na kukutakieni maadhimisho mema ya sherehe ya kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa watakao shereheka kwa wale wenye kumbukumbu njema, na kwa vile Mapinduzi Matukufu yale pia yaliandamana na umwagaji damu, natoa pole kwa wenye kumbukumbu chungu.
P
 
Back
Top Bottom