Mbigirikavu
Senior Member
- Aug 19, 2022
- 101
- 118
Tunajua kuwa wewe Mo ni shabiki na mwanachama wa Simba SC, tunaamini kuna wakati unajitolea kwa hali na mali kuifanya Simba iwe bora sambamba na kuinua furaha yako na mashabiki wenzako.
Lakini kwa sasa tunafahamu kuwa umeingia kwenye mkataba wa kibiashara na Simba SC ambao malengo ni kuongeza ukubwa wa Simba na kuongeza mapato kwa upande wa biashara yako.
Umeikuta Simba ikiwa na uongozi ambao hawakuwa na hela na walizoea hali hiyo, na leo una viongozi hapo Simba wa aina hiyo hiyo. Tofauti sana na wewe uliyezaliwa kwenye hela na umebarikiwa kutambua njia za kuzinasa hizo hela kuliko viongozi wako waliopo hapo.
Kwa hiyo nakukumbusha kuwa kichwa na mhimili wa kuingiza mapato kwenye biashara zako kupitia Simba SC, ni wewe tu Mohammed Dewji.
Usiwaachie timu hao wenye hisa 51% ukatarajia kupata hela hapo Simba. Ingia wewe 'physically'. Hao wengine hawana weledi wa biashara kubwa kama za Mo. Watakufelisha.
Mashabiki wa Simba tunaamini wewe Mo ni chapa kubwa sana Afrika na Duniani kote. Uliypotia mkono wewe panaaminika na wafanyabiashara wengi wakubwa.
Kuna vilabu vikubwa Afrika vinavyomilikiwa na watu uliowazidi mbali sana kifedha, umaarufu, na hadhi. Wewe Mo kuingia kwako kwenye mpira kiuwekezaji kunatazamwa na Afrika nzima kama siyo Dunia.
Hadi kufikia miaka minne ya uwekezaji, kwa tunavyouona utajiri wako Afrika, na ushabiki wako kwa Simba, tulitarajia kuona Simba imebeba Kombe la Mabingwa Afrika.
Wengi tunafahamu kuwa kadiri Simba itakavyokuwa bora ndivyo wadhamini wakubwa watakavyoipigania Simba na mapato ya Simba kuwa makubwa zaidi hatimaye malengo yako ya kuwekeza Simba kibiashara kutimia.
Lakini usithubutu kuwaachia timu watu ambao hawana utalaamu wala utashi wa kweli kuendeleza uwekezaji wako. Watakufelisha na kuangusha chapa yako uliyoijenga barani Afrika na Duniani kwa ujumla.
Ingia wewe, kusajili wachezaji, makocha na vifaa, kama ulivyofanya miaka miwili iliyopita. Akina Salum Abdallah "Try again" wamekuangusha na wataendelea kukuangusha kwa sababu hawajui mifumo ya kibiashara.
Chunguza kidogo tu, timu mwaka juzi, ilitolewa na Kaizer Chief, lakini hiyo Kaizer Chief ndiyo iliyofika fainali. Mwaka jana ilitolewa na Orlando Pirates, nayo ndiyo iliyofika fainali.
Sasa angalia Simba ilivyokuwa dhaifu misimu hiyo. Ingekuwa bora kidogo tu Simba ilikuwa fainali moja kwa moja na leo lingekuwa linaimbwa jina lako kila mahali.
Ubingwa wa Afrika unauchelewesha wewe Mo kwa kuwaachia timu watu wasiyo na malengo ya kibiashara. Wao wanakula, wanalala, wanapata mishara na posho, maisha yanawaendea. Suala la biashara ni la kwako wewe Mo.
Biashara zako zipambanie wewe mwenyewe.
Nakutakia Jumatatu njema.
Lakini kwa sasa tunafahamu kuwa umeingia kwenye mkataba wa kibiashara na Simba SC ambao malengo ni kuongeza ukubwa wa Simba na kuongeza mapato kwa upande wa biashara yako.
Umeikuta Simba ikiwa na uongozi ambao hawakuwa na hela na walizoea hali hiyo, na leo una viongozi hapo Simba wa aina hiyo hiyo. Tofauti sana na wewe uliyezaliwa kwenye hela na umebarikiwa kutambua njia za kuzinasa hizo hela kuliko viongozi wako waliopo hapo.
Kwa hiyo nakukumbusha kuwa kichwa na mhimili wa kuingiza mapato kwenye biashara zako kupitia Simba SC, ni wewe tu Mohammed Dewji.
Usiwaachie timu hao wenye hisa 51% ukatarajia kupata hela hapo Simba. Ingia wewe 'physically'. Hao wengine hawana weledi wa biashara kubwa kama za Mo. Watakufelisha.
Mashabiki wa Simba tunaamini wewe Mo ni chapa kubwa sana Afrika na Duniani kote. Uliypotia mkono wewe panaaminika na wafanyabiashara wengi wakubwa.
Kuna vilabu vikubwa Afrika vinavyomilikiwa na watu uliowazidi mbali sana kifedha, umaarufu, na hadhi. Wewe Mo kuingia kwako kwenye mpira kiuwekezaji kunatazamwa na Afrika nzima kama siyo Dunia.
Hadi kufikia miaka minne ya uwekezaji, kwa tunavyouona utajiri wako Afrika, na ushabiki wako kwa Simba, tulitarajia kuona Simba imebeba Kombe la Mabingwa Afrika.
Wengi tunafahamu kuwa kadiri Simba itakavyokuwa bora ndivyo wadhamini wakubwa watakavyoipigania Simba na mapato ya Simba kuwa makubwa zaidi hatimaye malengo yako ya kuwekeza Simba kibiashara kutimia.
Lakini usithubutu kuwaachia timu watu ambao hawana utalaamu wala utashi wa kweli kuendeleza uwekezaji wako. Watakufelisha na kuangusha chapa yako uliyoijenga barani Afrika na Duniani kwa ujumla.
Ingia wewe, kusajili wachezaji, makocha na vifaa, kama ulivyofanya miaka miwili iliyopita. Akina Salum Abdallah "Try again" wamekuangusha na wataendelea kukuangusha kwa sababu hawajui mifumo ya kibiashara.
Chunguza kidogo tu, timu mwaka juzi, ilitolewa na Kaizer Chief, lakini hiyo Kaizer Chief ndiyo iliyofika fainali. Mwaka jana ilitolewa na Orlando Pirates, nayo ndiyo iliyofika fainali.
Sasa angalia Simba ilivyokuwa dhaifu misimu hiyo. Ingekuwa bora kidogo tu Simba ilikuwa fainali moja kwa moja na leo lingekuwa linaimbwa jina lako kila mahali.
Ubingwa wa Afrika unauchelewesha wewe Mo kwa kuwaachia timu watu wasiyo na malengo ya kibiashara. Wao wanakula, wanalala, wanapata mishara na posho, maisha yanawaendea. Suala la biashara ni la kwako wewe Mo.
Biashara zako zipambanie wewe mwenyewe.
Nakutakia Jumatatu njema.