Albinoomweusi
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 3,433
- 8,585
Ni Katikati ya mwaka 2013, zimbwe jr yupo kwenye basi la kagera Sugar anamtoroka meneja wake Heri Mzozo ili akasaini mwaka mmoja na wanankurukumbi. Hii ni baada ya tindikali za moto zilipounguza moyo wake akiwa Azam academy ambapo vijana aliyocheza nao hapo (simon Msuva na Aishi manula) walishaanza kutoboa. Huku kocha Stewart Hall akimuondoa Zimbwe na wenzake Kambini.
.
Zimbwe anaona maisha ni kama mlima uliyomlalia kifuani. Lichw ya akili za kitoto za Zimbwe, Heri Mzozo akafanya juu chini na mungu si Athumani zimbwe akasaini simba, enzi hizo yupo Isa Rashid baba Ubaya na Abdi Banda. Mbavu zilizo shiba, Zimbwe jr anajiuliza je "nitatoboa kweli?" Mungu anaonesha miujiza yake, Abdi banda anabadilishwa namba huku Baba ubaya yupo Majeruhi. Ni zimbwe pekee aliyebaki kuzilinda mbavu za mnyama. Anapewa nafasi kisha anafanya maajabu.
.
Naam hiki ni kisha kifupi cha Zimbwe na Simba. Leo naongea nanyi watanzania kisha nitaongea na Zimbwe.
Samuel Goldfish ni Producer mkongwe wa filamu Marekani, yeye aliwahi kusema "“The harder I work, the luckier I get.” kadri anavyofanya kazi ndivyo kadri anavyopata bahati. Nataka kuwaambia si Uchawi wala fitna, bali ni juhudi ndiyo zinamfanya zimbwe awe maridadi kazini.
.
Tanzania ina mbavu imara za kushoto, kama kisiki basi ni cha Mpingo, na kama laini basi ni kama muwa bungala, zimbwe yupo kama spana malaya, kila mfumo yeye twende tu, ukitaka Pira gumu yuko tayari, ukitaka pira Laini (biriani) twende. Si uchawi, ni juhudi tu.
.
Sasa naongea na wewe zimbwe, "Alipangalo Mola Huwa" yuko wapi tena Yupo wapi Tena Jamal Mwambeleko, nioneshe alipo Asante kwasi, amekwenda wapi Stephano mwasika? Basi jua kwamba huu ni wakati wako, mungu amekufungulia milango ya riziki, ingia jibwede mwanaume, wahenga walistaajabu sana kuona wembamba wa Reli lakini Treni Ilipita juu yake, leo Afrika inashangaa umbo lako na mambo yako, waache washangae tu, kama majibu hawana basi wakaliangalie koti la suti, ni kubwa mno, lakini lote linashonwa na kasindano kadogodogo.
.
Asante kwa burudani yako ewe Digi digi mwenye mapafu ya farasi wa vita. The time is yours, use it.
.
Zimbwe anaona maisha ni kama mlima uliyomlalia kifuani. Lichw ya akili za kitoto za Zimbwe, Heri Mzozo akafanya juu chini na mungu si Athumani zimbwe akasaini simba, enzi hizo yupo Isa Rashid baba Ubaya na Abdi Banda. Mbavu zilizo shiba, Zimbwe jr anajiuliza je "nitatoboa kweli?" Mungu anaonesha miujiza yake, Abdi banda anabadilishwa namba huku Baba ubaya yupo Majeruhi. Ni zimbwe pekee aliyebaki kuzilinda mbavu za mnyama. Anapewa nafasi kisha anafanya maajabu.
.
Naam hiki ni kisha kifupi cha Zimbwe na Simba. Leo naongea nanyi watanzania kisha nitaongea na Zimbwe.
Samuel Goldfish ni Producer mkongwe wa filamu Marekani, yeye aliwahi kusema "“The harder I work, the luckier I get.” kadri anavyofanya kazi ndivyo kadri anavyopata bahati. Nataka kuwaambia si Uchawi wala fitna, bali ni juhudi ndiyo zinamfanya zimbwe awe maridadi kazini.
.
Tanzania ina mbavu imara za kushoto, kama kisiki basi ni cha Mpingo, na kama laini basi ni kama muwa bungala, zimbwe yupo kama spana malaya, kila mfumo yeye twende tu, ukitaka Pira gumu yuko tayari, ukitaka pira Laini (biriani) twende. Si uchawi, ni juhudi tu.
.
Sasa naongea na wewe zimbwe, "Alipangalo Mola Huwa" yuko wapi tena Yupo wapi Tena Jamal Mwambeleko, nioneshe alipo Asante kwasi, amekwenda wapi Stephano mwasika? Basi jua kwamba huu ni wakati wako, mungu amekufungulia milango ya riziki, ingia jibwede mwanaume, wahenga walistaajabu sana kuona wembamba wa Reli lakini Treni Ilipita juu yake, leo Afrika inashangaa umbo lako na mambo yako, waache washangae tu, kama majibu hawana basi wakaliangalie koti la suti, ni kubwa mno, lakini lote linashonwa na kasindano kadogodogo.
.
Asante kwa burudani yako ewe Digi digi mwenye mapafu ya farasi wa vita. The time is yours, use it.