Moja katika picha adimu za harakati ya kupigania Uhuru wa Tanganyika: Abbas Sykes, Dossa Aziz na Julius Nyerere 1950s

Moja katika picha adimu za harakati ya kupigania Uhuru wa Tanganyika: Abbas Sykes, Dossa Aziz na Julius Nyerere 1950s

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1568321929296.png

Waliokaa kwenye viti mbele wa kwanza Dossa Aziz na nyuma yake wa kwanza aliyesimama ni Abbas Sykes na mbele waliokaa kwenye viti wa tano kutoka kulia ni Julius Nyerere ndani ya picha moja.

Jicho la camera siku zote linahifadhi kile jicho la binadamu lilishuhudia.

Katika utafiti wa historia ya TANU niligundua kitu kimoja.

Ile kamati ya ndani, ndani ya kamati kubwa wale watu watano hawa ndiyo walikuwa New Street TANU Office Dar es Salaam: Mzee John Rupia, Abdul na Ally Sykes, Dossa Aziz na Julius Nyerere wakipendana sana.

Hamza Mwapachu hapo yuko ''jela'' kisiwani Nansio, hawa wakipendana sana na wale watu waliokuwa pembeni yao ndani ya TANU waliwapa majina ya utani.

Abdul wakimwita, ''The Sweet Abdul Sykes,'' kwa ule ukarimu wake na Dossa, ''The Bank,'' kwa ajili ya utajiri wake.

Mzee Rupia bila shaka kwa ule utu uzima wake hawakuweza kumfanyia maskhara kiasi cha kumpachika jina.

Nyerere baadae na yeye akapachikwa jina na Bi. Titi katika mkutano wa hadhara akasema, ''Huyu ni Mwalimu,'' akiwa na maana Nyerere atawasomesha Waingereza na Gavana Twining wao siasa katika kupambananao na toka siku ile jina likashika.

Mwalimu akaingia na jina hili kaburini.

Alikuwapo mwalimu Steven Mhando lakini TANU hata siku moja hawakumwita kwa jina hilo.

Siku hizo Julius Nyerere alikuwa akivuta sigara.

Kwenye meza yake pale meza kuu kama wako kwenye dhifa Ukumbi wa Arnautoglo au wapi wakimwekea pakiti ya sigara na kibiriti.

Nyerere alikuwa akivuta, ''Pall Mall Cigarettes,'' sigara za Kimarekani zikipendwa sana na vijana watanashati wa mji wa wakati ule.
 
Mkuu shukran Kwa kumbukumbi hii adhimu .Naomba picha zingine za harakati za Uhuru kama ile nyerere akiea na bibi titi jukwaani na zingine
 
  • Thanks
Reactions: Ctr
Mkuu asante kwa picha hii lakn hebu jaribu kuingia ndani zaidi unataka kutuambia nini
Shark,
Labda nami nikuulize swali lakini nakutaka radhi kwa mie badala ya kukujibu swali lako nakuuliza swali.

Kwani wewe unapata ujumbe gani katika picha hiyo?
 
Historia nzuri sana, japo mie nasikitika Dossa alivyoporwa mali za urithi na watoto wa Hamza. Laana itawatafuna watoto wa Hamza kwa kudhulumu mali ya "The Bank" na kumsababishia ufukara.
 
Mzee Mohamed naomba kujua Mzee Rupia alikuwa kabila gani na alifariki mwaka gani?
 
Waliokaa kwenye viti mbele wa kwanza Dossa Aziz na nyuma yake wa kwanza aliyesimama ni Abbas Sykes na mbele waliokaa kwenye viti wa tano kutoka kulia ni Julius Nyerere ndani ya picha moja.

Jicho la camera siku zote linahifadhi kile jicho la binadamu lilishuhudia.

Katika utafiti wa historia ya TANU niligundua kitu kimoja.

Ile kamati ya ndani, ndani ya kamati kubwa wale watu watano hawa ndiyo walikuwa New Street TANU Office Dar es Salaam: Mzee John Rupia, Abdul na Ally Sykes, Dossa Aziz na Julius Nyerere wakipendana sana.

Hamza Mwapachu hapo yuko ''jela'' kisiwani Nansio, hawa wakipendana sana na wale watu waliokuwa pembeni yao ndani ya TANU waliwapa majina ya utani.

Abdul wakimwita, ''The Sweet Abdul Sykes,'' kwa ule ukarimu wake na Dossa, ''The Bank,'' kwa ajili ya utajiri wake.

Mzee Rupia bila shaka kwa ule utu uzima wake hawakuweza kumfanyia maskhara kiasi cha kumpachika jina.

Nyerere baadae na yeye akapachikwa jina na Bi. Titi katika mkutano wa hadhara akasema, ''Huyu ni Mwalimu,'' akiwa na maana Nyerere atawasomesha Waingereza na Gavana Twining wao siasa katika kupambananao na toka siku ile jina likashika.

Mwalimu akaingia na jina hili kaburini.

Alikuwapo mwalimu Steven Mhando lakini TANU hata siku moja hawakumwita kwa jina hilo.

Siku hizo Julius Nyerere alikuwa akivuta sigara.

Kwenye meza yake pale meza kuu kama wako kwenye dhifa Ukumbi wa Arnautoglo au wapi wakimwekea pakiti ya sigara na kibiriti.

Nyerere alikuwa akivuta, ''Pall Mall Cigarettes,'' sigara za Kimarekani zikipendwa sana na vijana watanashati wa mji wa wakati ule.
Mzee wangu Mohamed Said, Shikamoo.
Asante kwa hizi kumbukumbu unazotumegea kila siku. Mie nilichoona haraka ni kwamba wengi wa wazee hawa maarufu wa TANU waliwekeza sana kwa watoto na wakaja kuwa na nyadhifa muhimu hapa nchini. Mzee Rupia,nafikiri mwanae alikuja kuwa chief secretary, Dossa Aziz mwanae alikuja kuwa IGP, Hamza Mwapachu wanae wawili ni maarufu sana hapa Tanzania katika siasa na diplomasia hapa namaanisha Bakari na Juma. Sijajua Watoto wa akina Sykes kama walipata nyadhifa serikalini zaidi ya Sykes mdogo kuwa balozi. Hata Mtemvu nae nakumbuka mwanae mmoja kuwa mbunge. Zaidi ya Makongoro (mwanajeshi) na Rose kuwa wabunge sijui watoto kama watoto wa Mwalimu pia waliingia katika nyadhifa za utendaji.

Mwisho ningefurahi siku moja nitembelee maktaba yako endapo utaridhia.
Nitangulize shukurani.
 
Kumbe alikuwa ana "Smoke"
Si kidogo, kuna kipindi inasemwa sigara iliwasha nyingine. Moja ya sifa zake ni kuachana na uvutaji sigara pale alipoamua. Ngumu sana kuacha sigara kwa uvutaji wa kiwango kile.
 
kwenye picha zako naona mmiliki wa picha ni wale wale doza na syk wengine sijui hawakuwa na uwezo wa picha
 
Mzee wangu Mohamed Said, Shikamoo.
Asante kwa hizi kumbukumbu unazotumegea kila siku. Mie nilichoona haraka ni kwamba wengi wa wazee hawa maarufu wa TANU waliwekeza sana kwa watoto na wakaja kuwa na nyadhifa muhimu hapa nchini. Mzee Rupia,nafikiri mwanae alikuja kuwa chief secretary, Dossa Aziz mwanae alikuja kuwa IGP, Hamza Mwapachu wanae wawili ni maarufu sana hapa Tanzania katika siasa na diplomasia hapa namaanisha Bakari na Juma. Sijajua Watoto wa akina Sykes kama walipata nyadhifa serikalini zaidi ya Sykes mdogo kuwa balozi. Hata Mtemvu nae nakumbuka mwanae mmoja kuwa mbunge. Zaidi ya Makongoro (mwanajeshi) na Rose kuwa wabunge sijui watoto kama watoto wa Mwalimu pia waliingia katika nyadhifa za utendaji.

Mwisho ningefurahi siku moja nitembelee maktaba yako endapo utaridhia.
Nitangulize shukurani.
Bullet,
Karibu Maktaba.

Hamza Aziz IGP ni mtoto wa Aziz Ali kwa hiyo ni mdogo wake Dossa Aziz.

1568391378519.png

Hamza Aziz akiwa askari miaka ya 1960​
 
kwenye picha zako naona mmiliki wa picha ni wale wale doza na syk wengine sijui hawakuwa na uwezo wa picha
Ofisa,
Nyaraka nyingi na picha za historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika zipo mikononi mwa watu binafsi.

Nimepata picha kutoka kwa watoto wa akina Dossa Aziz, Sheikh Abdallah Chaurembo, wanafunzi wa Sheikh Hassan bin Ameir, wajukuu wa Jumbe Tambaza, watoto wa Ali Msham, watoto wa Abdallah na Maulidi Kivuruga wa Tabora, watoto wa Yusuph Chembera na Salum Mpunga wa Lindi, watoto wa Yusuf Olotu wa Moshi, wajukuu wa Makata Mwinyi Mtwana wa Tanga na watoto wa Sheikh Abdallah Rashid Sembe wa Tanga kwa kweli wachangiaji picha ni wengi na hapa nitaeleza kuhusu mchango wa sisi wajukuu wa Salum Abdallah.

Nimepokea picha za babu yangu Salum Abdallah kutoka kwa binamu yangu Bi. Mgeni bint Farijallah kutoka Tabora picha ambazo alizihifadhi baba yake na baada ya kifo cha baba yake mama yake baada ya kifo cha baba yake.

Picha hizi zilihifadhiwa baada ya kifo cha babu kwana wa 1974 na kwa miaka 45 hakuna aliyekuwa anajua zilipo kiasi cha kuamini kuwa zimepotea.

Picha hizi ni katika historia ya siasa za vyama vya wafanyakazi Tanganyika wakati wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) iliyoundwa mwaka wa 1955.

Baada ya kuhangaika sana kuzitafuta watoto wa Kassanga Tumbo aliyekuwa Katibu muasisi wa TRAU babu yangu akiwa Rais muasisi waliniletea picha kutoka Sikonge lakini zilikuwa zimharibika sana kwa kukosa matunzo ndipo nilipotembelewa na Bi. Mgeni na nikamuuliza kuhusu picha.

Jibu lake lilikuwa nitazitafuta kwa mama.
Hakichukua muda akaniletea picha nzuri kabisa zenye ubora.

1568392846132.png

Viongozi wa TRAU
Mstari wa kati kulia ni Salum Abdllah akifuatiwa na Kassanga Tumbo

Picha nyingi nimepata katika Maktaba ya Sykes na sababu kubwa ni kuwa wao wamekuwa katika harakati hizi kutoka mwaka wa 1929 na vitu vingi walivihifadhi katika nyumba zao.

Hata hivyo zipo baadhi ya picha nimepata nimepata kwa watoto wa wazalendo wengine na nyingine kwa watu wa kawaida na mpaka hivi sasa bado napokea picha.
 
Back
Top Bottom