Moja ya hasara za kutegemea uchawi,ni kuwaweka boarding wachezaji wa timu wakati wana wake na familia zao

Moja ya hasara za kutegemea uchawi,ni kuwaweka boarding wachezaji wa timu wakati wana wake na familia zao

Cashman

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2018
Posts
3,017
Reaction score
5,294
Maisha ya soka hapa Tanzania yamejaa maswali mengi sana.Unaweza ukafikiri mpira ni kipaji,uwezo,nidhamu na kujituma sana katika mazoezi.Kwa hapa Tanzania jibu ni lah!

Watanzania wengi wakiwemo viongozi wa timu hizi wanaamini kuwa mchezaji anaweza kurogwa kupitia mahusiano ya kimapenzi na mwanamke kiasi kwamba anaweza kuathiriwa uwezo wake wa kuonyesha kipaji chake.

Imani kama hizo ambazo sio za kiweledi kabisa,zinasababisha timu yenye wachezaji wakubwa kuwekwa kuishi kambini na kuziacha familia zao nyumbani.

Hivi mtu ana mke na watoto,anawezaje kuishi Avic town mke anamwacha Tegeta?

Huyo mke mnamsaidiaje kihisia au mnadhani pesa inaaweza kumaliza changamoto zote?

Wachezaji wanatakiwa kuwekewa utaratibu wa kuwadhibiti kwenye nidhamu nje ya uwanja pasipo kuwapoka uhuru wao.Huwezi kuishi mwaka mzima kama mwanafunzi wa sekondari boarding wakati wewe ni professional player.

Tuache fikra za kichawi tunapoendesha soka la kisasa,wachezaji washindane kwa vipaji na uwezo wao uwanjani na sio mazingira ya nje ya uwanja kama inavyofanyika kwetu

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Uko sahihi mkuu. Huu mfumo wa kukaa kambi umekaa kizamani sana.

Muhimu nidhamu izingatiwe na ilindwe kwa gharama yoyote.
 
Uko sahihi mkuu. Huu mfumo wa kukaa kambi umekaa kizamani sana.

Muhimu nidhamu izingatiwe na ilindwe kwa gharama yoyote.
Mentality za wachezaji wengi wanaocheza Tanzania, usipowaweka kambini umekwisha.
Wengi wao hawana 'Self Control '
 
Mentality za wachezaji wengi wanaocheza Tanzania, usipowaweka kambini umekwisha.
Wengi wao hawana 'Self Control '
Swali je tunawabadilisha vipi? Tutakua hivi milele?

Wakati dunia inaenda kulia ni sahihi sisi tuendelee kubaki kushoto?
 
Swali je tunawabadilisha vipi? Tutakua hivi milele?

Wakati dunia inaenda kulia ni sahihi sisi tuendelee kubaki kushoto?
Tukitengeneza mifumo bora kuanzia chini kwa maana ya Academies itaondoa hiyo kadhia kwa kiasi kikubwa.
 
Back
Top Bottom