Molinga asamehewe

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Midadi ya kucheza na moyo wa wa kupenda kuisadia timu yake ipate matokeo dhidi ya Biashara United kupitia mchango wake ndicho hasa kilichosababisha David Molinga aonyeshe kukerwa na kutolewa uwanjani na kocha wake. Hasa kutokana na mchango wake kwenye mechi zilizotangulia. Hamaki kama hizi ziko hata kwa wachezaji wakubwa huku ulaya.

Tumsamehe tu kwakuwa nia yake haikuwa mbaya hasa kutokana na kuipatia Yanga matokeo kwenye mechi zilizotangulia. Hivyo aliamini hata kwenye mechi Ile angeweza kuisadia pia lakini alisahau kuwa kocha ndiye mwenye mamlaka ya mwisho kuhusu nani atoke na nani aanze mechi.

Kusamehe ni kuonyesha ukomavu na kamwe sio udhaifu
 
Huyo Molinga ni kiazi afukuzwe kabisa.
Simba mnamuogopa molinga kuliko mchezaji yeyote Yanga, akifukuzwa kwenu ni aheri kubwa.

Alichokifanya mchezaji ni hamu tu ya kuendelea kucheza akiamini bado anazo nguvu na uwezo wa kuisaidia timu yake. Kocha ni mzazi, mzoefu na aliwahi kuwa mchezaji mkubwa, pengine alilifahamu hili kuliko mimi. Sidhani kama Molinga alikosea saaana kama kijana na mchezaji ambae ameshaanza kuisaidia timu yake baada ya kushindwa kufanya hivyo katika siku zake za awali Yanga
 
Huyo Molinga ni kiazi afukuzwe kabisa.
Ni mchezaji wa kawaida sana, aache jeuri, naona ndala wameimarisha sana safu yao ya ushambuliaji, Ditram Nchimbi, Tariq Kiakala, yule muaivorikosti, kiuhalisia sioni kabisa nafasi yake.
 
Je, amejutia makosa?

Sent from my SM-T355Y using Tapatalk
 
Je, amejutia makosa?

Sent from my SM-T355Y using Tapatalk
malezi ya mchezaji na kocha ni muhimu sana kwenye soka. Je, baada ya mchezaji kutenda kosa alifanya nini na baada ya kocha kuona mchezaji amekosea alisema na kufanya nini. Maisha na matendo ya mchezaji na kocha baada ya kosa kutokea ni muhimu sana katika kumaliza tatizo. Mara nyingi malezi ya kiswahili hayaruhusu kusamehe kwa haraka
 
Kosa alilofanya Molinga ni la kimichezo kabisaa, lakini adhabu aliyopewa baada ya kosa kutokea sio ya kimichezo hasa kwa club kubwa kama Yanga. Big up kwa walioliona hili
 
Molinga asamehe, ona katuokoa na aibu dhidi ya Namungo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…