Watu 30 wamelazwa kwenye hospitali mbali mbali za kaunti ya Mombasa pwani mwa Kenya baada ya kuugua ugonjwa wa Chikungunya, kwa mujibu wa shirika la habari la serikali KBC.
Gavana wa Mombasa Hassan Joho, amezindua magari matano yenye mashine na dawa kunyunyiziwa katika kaunti hiyo wakati ugonjwa unazidi kuwatishia watu zaidi.
Chini ya miezi mitatu iliyopita kaunti ya Mombasa ilikuwa ikikabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ambapo watu kadhaa walilazwa hospitalini na maeneo kadhaa ya mankuli kufungwa katika kaunti hiyo.
Joho alithibitisha kuwa kumekuwa na visa 120 vya wagonjwa huo na visa 32 vilivyothibitiwa kati ya hivyo vimedai kuwa vile vya ugonjwa wa chikungunya.
Kufuatia ugonjwa huo kusambazwa na mbu Gavana Joho amewashauri wenyeji wa Mombasa kushirikiana kwa karibu na serikali ya kaunti kuondoa mazingira salama kwa mbu.
Chanzo: BBC Swahili
========
About Chikungunya
Chikungunya is a viral disease transmitted to humans by infected mosquitoes. It causes fever and severe joint pain. Other symptoms include muscle pain, headache, nausea, fatigue and rash.
Joint pain is often debilitating and can vary in duration.
The disease shares some clinical signs with dengue and zika, and can be misdiagnosed in areas where they are common.
There is no cure for the disease. Treatment is focused on relieving the symptoms.
The proximity of mosquito breeding sites to human habitation is a significant risk factor for chikungunya.
The disease mostly occurs in Africa, Asia and the Indian subcontinent. However a major outbreak in 2015 affected several countries of the Region of the Americas.
Source: WHO