Morgan Tsvangirai, Ikulu, Dar Es Salaam.

Halisi

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2007
Posts
2,802
Reaction score
614
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425


PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Na Mwandishi Maalum


Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Rais Jakaya Mrisho Kikwete jioni ya leo, Jumatano, Desemba 3, 2008 amekutana na kufanya mazungumzo na kiongozi wa chama cha Movement for Democratic Change (MDC) cha Zimbabwe, Bwana Morgan Tsvangirai, Ikulu, mjini Dar Es Salaam.

Katika mazungumzo hayo, Bwana Tsvangirai amemweleza Rais Kikwete juu ya mazungumzo yanayoendelea kati ya MDC na chama tawala cha Zimbabwe cha ZANU-PF kuhusu uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa nchini humo.

Bwana Tsvangirai amemweleza Rais Kikwete kuwa mazungumzo hayo bado yamekwama na akamwomba mwenyekiti huyo wa AU kutumia mamlaka ya umoja huo kuangalia jinsi ya kukwamua mazungumzo hayo.

Mazungumzo hayo ya kuundwa kwa serikali ya kitaifa nchini humo ni mchakato wa AU, ambayo imeiomba Jumuia ya Uchumi Kusini mwa Afrika (SADC) kusimamia moja kwa moja mazungumzo hayo chini ya mpatanishi Mheshimiwa Thabo Mbeki, Rais wa zamani wa Afrika Kusini.


Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

03 Desemba, 2008
 
Hawa mabwege bado wanatumia yahoo tu? Hata baada ya Sarah Palin kuwa spoofed and all?

Juzi nimeona top echelon ya polisi wote wanatumia yahoo, gmail, lycos etc.

Kazi tunayo!
 
..tatizo la Morgan Tsivangarai ni kwamba usipokubaliana naye anaishia kukuita majina ya ajabu-ajabu.

..halafu taarifa haielezi ni nini msimamo wa Tanzania kuhusu mgogoro wa Zimbabwe.

..inasemekana msimamo wetu unafana-fanana na ule wa Botswana.

..nimeona niwaletee barua ya Thabo Mbeki inayoonyesha frustrations zake na tabia za Morgan Tsivangarai na MDC-T.

 
Leo tumesikia kwamba Raila ametaka viongozi wa Afirka wafikirie jinsi ya kumuondoa Mugabe na kumtangaza moja kwa moja Tsvangirai kuwa Rais. Ni maneno yametustusha wengi. Lakini ni jambo ambalo linaweza kujadiliwa.
Kwa sababu Mugabe is an old man,who has done his task,na anaweza kupumzika. Na kama ikiwezekana kwa elders kumuomba Kustaafu,itakuwa jambo zuri.
Kenya uhalifu ulitokea,Raila alishinda,tatizo likatanzazuliwa na Kofi Annan solution,kwa kumpa Raila Uwaziri Mkuu. That crime cannot be committed twice. It was a tragedy,Kenya ingeweza kuwa Somalia,lakini,by the Grace of God,there was peace.
This is not about Mugabe. He is a respected person,ameleta Uhuru Zimbawe,na hata akistaafu sasa ataheshimika.
Aombwe aachie ngazi,aondolewe peacefully,emphasi on" peacefully"
 

Ya kweli haya? "Tumesikia" ni wingi, wewe na nani? Kutoka wapi?

Kama kweli alikuwa wapi siku zote anasubiri moto mpaka unazimika ndiyo anataka kupata shughuli mpya ya kuuanzisha tena?
 
Mbeki alishindwa kutafuta suluhu ndani ya chama chake mwenyewe, je anaweza kweli kutafuta suluhu katika nchi ye wengine? SADC wasituletee ujinga hapa wa kusema power sharing kati ya Robati na Mogani; ingekuwa Robati ndiye amepata kura kama za Mogani unadhani kungekuwepo huu mjadara wa power sharing? Angesema ameshinda kama alivyofanya Salmini pale Zanzibar mwaka 1995 na kuchukua madaraka yote. Mugabe must go now!
 
Kichuguu,

..huu siyo muda wa Morgan kuzunguka akitafuta kuungwa mkono kupata madaraka/Uraisi Zimbabwe. badala yake atumie muda huu kutafuta msaada wa kupambana na kipindupindu na balaa la njaa nchini kwake.
 
Mugabe should be charged with crimes against humanity. He's letting his people eat excreta and die of cholera among other preventable diseases. He needs to do something about his ego before Zim becomes another version of somalia
 
Kwa wale wote wanaotaka kumsulubu Mugabe je ungekuwa wewe ndio Raisi Mugabe ungefanyeje ili kupata ardhi ya mababu zako iliyoporwa kwa mtutu wa bunduki, uliyoiomba kwa ustaarabu wa hali ya juu kwa kutumia usomi wako wa sheria lakini counterpart wako akakuzunguka?
 
..hakuna nchi iliyoko tayari kubeba gharama za kumuondoa Mugabe madarakani.

..South Africa wanaogopa kuchukua mzigo wa wakimbizi. wana-prefer soft landing ktk kumuondoa Mugabe.

..Botswana wanapiga kelele lakini hawana uwezo wa kijeshi kumtoa Mugabe. zaidi hawana credibility miongoni mwa majirani wa SADC. Botswana haikuwahi kuwawekea vikwazo au kufunga mpaka wake wakati wa utawala wa Smith na makaburu. kipindi hicho Raisi wa Botswana alikuwa Sir.Seretse Khama, baba mzazi wa Raisi wa sasa Lt.Gen.Ian Khama.

..nchi yenye nguvu za kijeshi za kumuondoa Mugabe ni Angola. tatizo ni kwamba Mugabe aliwasaidia sana wakati wakipigana na Savimbi wa Unita. Mozambique nao ndio usiseme; deni lao kwa Zimbabwe, ZDF,ZANU-PF, na Mugabe, halina mfano.
 

jokakuu, Botswana walikuwa ni member wa Petriotic Front countries, kuwa na uwezo au kutokuwa na uwezo si suala la how big your military is; you can act as a launch pad for the big guys. Hicho ndicho mugabe anahofia kwa Botswana. Suala la kutofunga mipaka au kufunga was more economical than political. this country have been a sole democratic country in Africa; which was born democratic; maamuzi ya kufunga mipaka hayaamuliwi na "fikra za mwenyekiti Zidumu" kama sisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…