Morocco yatoa vibali 10 vya kwanza vya kilimo cha Bangi

Morocco yatoa vibali 10 vya kwanza vya kilimo cha Bangi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1664985376979.png

Vibali hivyo kwa wakulima vinawapa ruhusa kisheria kulima na kuandaa mazazo ya Bangi viwandani na kuuza nje kwa mara ya kwanza. Wakulima kutoka maeneo ya Al-Hoceima, Chefchaouen na Taounate wataruhusiwa kuzalisha na kuuza bangi kwa matumizi ya matibabu na viwandani, kwa mujibu wa sheria iliyopitishwa na Bunge mwaka 2021.

Shirika la kitaifa linalodhibiti shughuli za Bangi ambalo lilitoa vibali hivyo limesema wakulima watahimizwa kuongeza uzalishaji halali wa Bangi ili kukidhi hitaji la soko. Morocco kwa muda mrefu ilikuwa moja kati ya nchi wazalishaji wakubwa wa Bangi haramu duniani na ilikuwa ikizalishwa kutoka katika maeneo maskini zaidi ya milimani ya nchi hiyo na kusafirishwa kwenda Ulaya.

Hatua ya serikali ya kuhalalisha uzalishaji wa bangi inalenga kuboresha hali ya wakulima maskini na kuzalisha mapato kwa uchumi.
 
Watu huwa wanapenda kufanya vitu kinyume, hata Bei huwa nzuri Kama kitu kikiwa Cha magendo. Sasa walivoruhusu tu ivo, Bei katika eneo Hilo itashuka
 
Back
Top Bottom