KERO Morogoro: Barabara ya Kilombero iwekewe matuta, tunapoteza Watu kutokana na mwendokasi wa Vyombo vya Moto

KERO Morogoro: Barabara ya Kilombero iwekewe matuta, tunapoteza Watu kutokana na mwendokasi wa Vyombo vya Moto

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
de78dac8b9f4b232b7f2d341c039b765.jpeg

Naomba nitoe malalamiko kwa Serikali juu ya Barabara ya Kilombero Mkoani Morogoro ambayo mwanzo ilikuwa ya vumbi ila Serikali ya Awamu ya 6 imetutengenezea lami, napongeza kwa hilo.

Barabara hiyo ambayo inajulikana pia Barabara ya Ifakara - Kidatu Wilayani Kilombero pamoja na hivyo, shida ni moja haijawekwa matuta, pia pembezoni mwa barabara kuna Shule, matukio ya ajali yamekuwa mengi sana.

Kila siku iendayo kwa Muumba kutokana na vyombo vya moto ikiwemo magari na Bodaboda kuendeshwa kwa spidi kubwa bila wahusika kujali Watu wanaopita pembeni au kuvuka Barabara.

Ombi letu Wananchi, Serikali ifikirie hilo, tuwekewe matuta kupunguza, tunasikitika kusema kuwa kutokana na ajali tumepoteza Watu wengi tunaowapenda.
 
Hivi ile Elimu inayofundishwa shule za Msingi darasa la Pili/tatu la matumizi ya barabara inazingatiwa?
Nakumbuka tulikuwa tunafundishwa
Kabla ya kuruka barabara; Angalia upande wa kulia, kama hakuna gari, angalia kushoto na kama hakuna gari; angalia kulia tena, na kama hakuna gari vuka kwa kutembea haraka haraka kwa kukatiza barabara bila kupinda pinda (na bila kukimbia)

Nashauri hiyo Elimu ya darasa la Pili/tatu ilirudiwe kwenye mikutano ya vijiji napengine iwe kwa maeneo yote yaliyopitiwa na barabara kuu (highway)
 
View attachment 2964131
Naomba nitoe malalamiko kwa Serikali juu ya Barabara ya Kilombero Mkoani Morogoro ambayo mwanzo ilikuwa ya vumbi ila Serikali ya Awamu ya 6 imetutengenezea lami, napongeza kwa hilo.

Barabara hiyo ambayo inajulikana pia Barabara ya Ifakara - Kidatu Wilayani Kilombero pamoja na hivyo, shida ni moja haijawekwa matuta, pia pembezoni mwa barabara kuna Shule, matukio ya ajali yamekuwa mengi sana.

Kila siku iendayo kwa Muumba kutokana na vyombo vya moto ikiwemo magari na Bodaboda kuendeshwa kwa spidi kubwa bila wahusika kujali Watu wanaopita pembeni au kuvuka Barabara.

Ombi letu Wananchi, Serikali ifikirie hilo, tuwekewe matuta kupunguza, tunasikitika kusema kuwa kutokana na ajali tumepoteza Watu wengi tunaowapenda.
Utii wa Sheria za usalama barabarani nchini Tanzania ni tatizo kubwa sana, watumiaji wengi wa barabara hawana Utamaduni wa kutii Sheria bila shuruti.

Mkiona Serikali haiwasaidii kwa wakati ktk kuweka matuta ili kupunguza ajali za mara kwa mara, chukueni Sheria mkononi. Chimbueni barabara ya lami kwa kuikata kama vile mnachimba mtaro wa kupitisha bomba la Maji kutoka upande mmoja wa barabara hadi upande mwingine wa pili. Chimbeni mtaro wenye upana kama wa mita moja na kina Kama cha sentimita hamsini kwenda chini kwenye sehemu ambazo mnaona zinapaswa kuwekwa matuta, baada ya siku chache mtawaona watu wa TANROAD watakuja wenyewe bila ya nyinyi kuwaita kwa ajili ya kuweka matuta katika sehemu mlizochimbua.
Mkizubaa bila kuchukua hatua stahiki mapema, watoto wenu wataendelea kupukutishwa na kufa kutokana na ajali za barabarani.
 
Hivi ile Elimu inayofundishwa shule za Msingi darasa la Pili/tatu la matumizi ya barabara inazingatiwa?
Nakumbuka tulikuwa tunafundishwa
Kabla ya kuruka barabara; Angalia upande wa kulia, kama hakuna gari, angalia kushoto na kama hakuna gari; angalia kulia tena, na kama hakuna gari vuka kwa kutembea haraka haraka kwa kukatiza barabara bila kupinda pinda (na bila kukimbia)

Nashauri hiyo Elimu ya darasa la Pili/tatu ilirudiwe kwenye mikutano ya vijiji napengine iwe kwa maeneo yote yaliyopitiwa na barabara kuu (highway)
Nadhani kwa Tanzania ni Mafinga pekee inazingatiwa. Kila ukipita pale asubuhi unaona vijana wanafunzi wakiwa katika mavazi maalum na vibao vya kusaidia kuongoza magari.

Hongera sana kwa mkuu wa usalama barabarani Mafinga na askari wote.
 
Utii wa Sheria za usalama barabarani nchini Tanzania ni tatizo kubwa sana, watumiaji wengi wa barabara hawana Utamaduni wa kutii Sheria bila shuruti.

Mkiona Serikali haiwasaidii kwa wakati ktk kuweka matuta ili kupunguza ajali za mara kwa mara, chukueni Sheria mkononi. Chimbueni barabara ya lami kwa kuikata kama vile mnachimba mtaro wa kupitisha bomba la Maji kutoka upande mmoja wa barabara hadi upande mwingine wa pili. Chimbeni mtaro wenye upana kama wa mita moja na kina Kama cha sentimita hamsini kwenda chini kwenye sehemu ambazo mnaona zinapaswa kuwekwa matuta, baada ya siku chache mtawaona watu wa TANROAD watakuja wenyewe bila ya nyinyi kuwaita kwa ajili ya kuweka matuta katika sehemu mlizochimbua.
Mkizubaa bila kuchukua hatua stahiki mapema, watoto wenu wataendelea kupukutishwa na kufa kutokana na ajali za barabarani.
Wakati wanafanya hayo Tanroads watakua wako usingizini ama unajifanya hujui ambacho kitawapata kupitia jeshi letu pendwa lile 😂
 
Dah! Poleni sana. Ila watanzania tujifunze kufuata sheria za barabara. Hizi akili za kuweka matuta ndo akili tulizo nazo hata kwenye maisha ya kawaida kuwekeana "matuta"... Tanzania ina tume za udhibiti nyingi mno. Yaani tunawaza kudhibiti tu badala ya kuchochea mambo yaende kasi. Barabara za bongo zinaongoza kwa matuta
 
Kwanza sio awamu ya 6 ,ni awamu ya Tano ya chuma

6(iliyopingwa na polepole ikampa ubalozi aache kuchonga) imeendeleza

Mwisho ,jamii yoyote inayopata kipya hasa lami hata ukiweka matuta itagongwa tu Hadi izoee hali yenyewe. WaPOGOLO Hawa hawahitaji matuta wanatakiwa kuzoea na kufata alama za barabarani

Kidinilo ,imekuwa kiswele ya zamani
 
Wakati wanafanya hayo Tanroads watakua wako usingizini ama unajifanya hujui ambacho kitawapata kupitia jeshi letu pendwa lile 😂
Hao TANROAD kwani huwa wanafanya doria ya kukagua barabara muda wote usiku na mchana? Umeshawahi kupata dhahama ya mtu wako wa karibu sana kama vile mtoto wako kugongwa na gari barabarani na kupoteza maisha kutokana na Uzembe wa madereva kwa kuendesha kwa mwendo mkubwa?
 
Hao TANROAD kwani huwa wanafanya doria ya kukagua barabara muda wote usiku na mchana? Umeshawahi kupata dhahama ya mtu wako wa karibu sana kama vile mtoto wako kugongwa na gari barabarani na kupoteza maisha kutokana na Uzembe wa madereva kwa kuendesha kwa mwendo mkubwa?
Sijawahi pata mkuu isipokuwa tu hii nchi yetu naijua ambavyo haiko proactive. Inasubiriaga mpaka majanga yatokee ndio ichukue hatua. Nashauri mngeungana kujenga daraja la juu la chuma.
 
Utii wa Sheria za usalama barabarani nchini Tanzania ni tatizo kubwa sana, watumiaji wengi wa barabara hawana Utamaduni wa kutii Sheria bila shuruti.

Mkiona Serikali haiwasaidii kwa wakati ktk kuweka matuta ili kupunguza ajali za mara kwa mara, chukueni Sheria mkononi. Chimbueni barabara ya lami kwa kuikata kama vile mnachimba mtaro wa kupitisha bomba la Maji kutoka upande mmoja wa barabara hadi upande mwingine wa pili. Chimbeni mtaro wenye upana kama wa mita moja na kina Kama cha sentimita hamsini kwenda chini kwenye sehemu ambazo mnaona zinapaswa kuwekwa matuta, baada ya siku chache mtawaona watu wa TANROAD watakuja wenyewe bila ya nyinyi kuwaita kwa ajili ya kuweka matuta katika sehemu mlizochimbua.
Mkizubaa bila kuchukua hatua stahiki mapema, watoto wenu wataendelea kupukutishwa na kufa kutokana na ajali za barabarani.
🤣 🤣 🤣
 
Back
Top Bottom