Morogoro: Daktari Kituo cha Afya cha Mikumi mbaroni kusabisha mjamzito kujifungua kwenye bajaji

Morogoro: Daktari Kituo cha Afya cha Mikumi mbaroni kusabisha mjamzito kujifungua kwenye bajaji

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Martine Shigella ameamuru daktari katika Kituo cha Afya cha Mikumi (jina tunalo) akamatwe akituhumiwa kusababisha mjamzito ajifungue akiwa kwenye pikipiki ya matairi matatu maarufu kwa jina la bajaj.

Shigella alitoa agizo hilo aliposikiliza kero za wananchi wakati wa mkutano wa hadhara katika Mji Mdogo wa Mikumi wilayani Kilosa.

Wakati wa mkutano huo, kijana aliyejulikana kwa jina la Abdallah Agustino, mkazi wa Mikumi alidai kuwa, Aprili mwaka huu alimpeleka mkewe, Jenifa Francis katika Kituo cha Afya cha Mikumi ili kujifungua.

Alidai walipofika kituoni hapo, daktari aliyekuwa zamu alimueleza kuwa Jenifa alitakiwa afanyiwe upasuaji na akamtaka ampe Sh 120,000 ili atumie vifaa vyake, badala ya kwenda kununua sehemu nyingine.

Agustino alidai kuwa, alishindwa kutoa kiasi hicho cha fedha na daktari alimweleza achague ama kumpa fedha hizo, au aondoke na mkewe.

Alidai walioondoka sehemu hiyo na wakati wakiwa njiani kwenda katika Kituo cha Afya cha Mtakatifu Kizito cha Mikumi, mkewe alijifungua wakiwa kwenye bajaji.

Akijibu swali la mkuu wa mkoa huyo juu ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya daktari huyo, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Dk George Kasibante, alisema tayari wamebadili uongozi wa kituo hicho cha afya na kumpa onyo mhusika.

Shigela alisema haridhishwa na hatua zilizochukuliwa dhidi ya daktari huyo ukilinganisha na ukubwa wa kosa alilolifanya kutokana na majibu aliyopewa na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilosa.

Aliwaagiza polisi wamkamate daktari huyo na kumuweka rumande na kisha akamwagiza Mkuu wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Morogoro, Manyama Tungaraza, kufanye uchunguzi kuhusu suala hilo na ikithibitika kuna kosa, achukuliwe hatua za kinidhamu.

Shigella aliwataka watumishi wa umma katika sekta ya afya mkoani humo kuacha kunyanyasa wajawazito.
 
Kuna siku nilikuwa hospitali moja ya Mkoa, akaja binti kama 18 years, mjamzito, akaambiwa na nesi atembee mwenyewe ile manesi wanatakaga wamama wafanye mazoezi, huwezi amini yule binti alipojaribu kutembea mtoto akachomoka akadondoka chini. alikufa baadaye.

Nilichojiuliza, binti ana 18, hiyo mashine imekuwa pana kiasi kwamba ile kutembea kuelekea wodini tu mtoto kachoropoka. wakati kuna wake zetu huwa wanahangaika, wekewe uchungu, sukuma hadi wanakandamizwa tumbo ndio mtoto anatoka kwa shida. kabinti kenyewe kembamba tu, kanyaturu.
 
Kuna siku nilikuwa hospitali moja ya Mkoa, akaja binti kama 18 years, mjamzito, akaambiwa na nesi atembee mwenyewe ile manesi wanatakaga wamama wafanye mazoezi, huwezi amini yule binti alipojaribu kutembea mtoto akachomoka akadondoka chini. alikufa baadaye.

Nilichojiuliza, binti ana 18, hiyo mashine imekuwa pana kiasi kwamba ile kutembea kuelekea wodini tu mtoto kachoropoka. wakati kuna wake zetu huwa wanahangaika, wekewe uchungu, sukuma hadi wanakandamizwa tumbo ndio mtoto anatoka kwa shida. kabinti kenyewe kembamba tu, kanyaturu.
Duh,kama njia ilishafunguka jee??
 
Nimesikiliza mwananchi akilalamika kuombwa pesa ili mke wake afanyiwe upasuaji na daktari wakati wa kujifungua ihali hapakuwa na haja hiyo.

Anaeleza kuwa mke wake alipokelewa usiku na nesi wa zamu akamwambia kuwa mkewe atajifungua salama kwani njia uzazi imefunguka vizuri, lakini daktari alipokuja alimtaka atoe kiasi cha pesa mkewe afanyiwe upasuaji.

Huyo mwananchi alilazimika kuondoka na mkewe kwani hakuwa nabpesa hiyo, akiwa ndani ya bajaji alijifungua.

Mkasa huu unaonyesha jinsi gani baadhi ya madaktari mbali na kwenda kinyume na maadili ya kazi pia hawana utu.

Daktari sngesababisha kifo kisicho cha lazima kwa upasuaji au kwa kumnyima huduma mama mjamzito kwani kujifungua nje ya hospitali ni hatari.

Hii imenifikirisha sana kwa jinsi tunakosa utu.
Screenshot_20210729-142730_Instagram.jpg
 
MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Martine Shigella ameamuru daktari katika Kituo cha Afya cha Mikumi (jina tunalo) akamatwe akituhumiwa kusababisha mjamzito ajifungue akiwa kwenye pikipiki ya matairi matatu maarufu kwa jina la bajaj.

Shigella alitoa agizo hilo aliposikiliza kero za wananchi wakati wa mkutano wa hadhara katika Mji Mdogo wa Mikumi wilayani Kilosa.

Wakati wa mkutano huo, kijana aliyejulikana kwa jina la Abdallah Agustino, mkazi wa Mikumi alidai kuwa, Aprili mwaka huu alimpeleka mkewe, Jenifa Francis katika Kituo cha Afya cha Mikumi ili kujifungua.

Alidai walipofika kituoni hapo, daktari aliyekuwa zamu alimueleza kuwa Jenifa alitakiwa afanyiwe upasuaji na akamtaka ampe Sh 120,000 ili atumie vifaa vyake, badala ya kwenda kununua sehemu nyingine.

Agustino alidai kuwa, alishindwa kutoa kiasi hicho cha fedha na daktari alimweleza achague ama kumpa fedha hizo, au aondoke na mkewe.

Alidai walioondoka sehemu hiyo na wakati wakiwa njiani kwenda katika Kituo cha Afya cha Mtakatifu Kizito cha Mikumi, mkewe alijifungua wakiwa kwenye bajaji.

Akijibu swali la mkuu wa mkoa huyo juu ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya daktari huyo, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Dk George Kasibante, alisema tayari wamebadili uongozi wa kituo hicho cha afya na kumpa onyo mhusika.

Shigela alisema haridhishwa na hatua zilizochukuliwa dhidi ya daktari huyo ukilinganisha na ukubwa wa kosa alilolifanya kutokana na majibu aliyopewa na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilosa.

Aliwaagiza polisi wamkamate daktari huyo na kumuweka rumande na kisha akamwagiza Mkuu wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Morogoro, Manyama Tungaraza, kufanye uchunguzi kuhusu suala hilo na ikithibitika kuna kosa, achukuliwe hatua za kinidhamu.

Shigella aliwataka watumishi wa umma katika sekta ya afya mkoani humo kuacha kunyanyasa wajawazito.
Hivi kwa Nini hizi office za Umma wanapenda sana pesa hadi utu wanaweka pembeni,ukienda Police shida hiyo hiyo hadi watu kumbakiziana mi kesi, Mahakamani nako usiseme ni mwendo wa pesa tu,Kama huna utanyanyapaliwa Kama Mgonjwa wa ukoma! Sasa ebu washikishe mpunga uwone wanavyopiga kazi hatari!!
 
Kila nisomapo naona kama kila Mtu anamshambulia Daktari kabla hata hatujamsikia upande wake.

Hata huyo Mkuu wa Mkoa hakupaswa kuchukua tu maamuzi baada ya kusikiliza upande mmoja...walioweka mifumo ya Mahakama ili kusikiliza pande zote zinazohusika walishajiridhisha ukubwa wa matatizo ya mfano kama huu.

Sina haja ya kumtetea huyo Daktari lakini pia silazimiki kumuamini Mlalamikaji moja kwa moja.
 
Hivi kwa Nini hizi office za Umma wanapenda sana pesa hadi utu wanaweka pembeni,ukienda Police shida hiyo hiyo hadi watu kumbakiziana mi kesi, Mahakamani nako usiseme ni mwendo wa pesa tu,Kama huna utanyanyapaliwa Kama Mgonjwa wa ukoma! Sasa ebu washikishe mpunga uwone wanavyopiga kazi hatari!!
hii nji rushwa ni mbaya sana....idara zote za serikali.......hicho ndio kielelezo...
 
Back
Top Bottom