Morogoro: Kituo cha Polisi Kihonda Kingejengwa Karibu na Stesheni ya Mwendokasi Badala ya Youth Mission

Morogoro: Kituo cha Polisi Kihonda Kingejengwa Karibu na Stesheni ya Mwendokasi Badala ya Youth Mission

Faana

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2011
Posts
38,657
Reaction score
44,759
Nimesikia tetesi kutoka kwa rafiki wa karibu kuwa serikali inakusudia kujenga kituo kingine cha polisi kwa kushirikisha nguvu za wananchi katika Kata ya Kihonda, ni jambo jema na zuri, binafsi ningeshauri kituo hicho kijengwe karibu na stesheni ya mwendokasi badala ya kwenda kulijenga eneo la youth mission ambako ni mbali na miundombinu muhimu kama barabara na reli:
  • Kituo kikijengwa karibu na stesheni ya mwendokasi kitasaidia kurahisisha huduma kwa wasafiri watakaokutana na changamoto za kiusalama wawapo kwenye mchakato wa kusafiri na mwendokasi au mabasi ya kawaida, hapa nazungumzia wasafiri watokao maeneo mbalimbali kuja kupanda treni hiyo pamoja na wale washukao kutoka kwenye treni hiyo
  • Kituo kitasaidia wasafiri watumiao barabara ya Morogoro - Dodoma kwa urahisi endapo kituo hicho kitajengwa karibu na highway hiyo badala ya huko pembezoni ambako ni takribani kilomita moja na zaidi kutoka highway na kilomita mbili toka kituo cha SGR
  • Kwa kujenga kituo hicho karibu na SGR itarahisisha kukifikia kituo kwakuwa tuta la SGR limeigawa Kihonda katika vipande viwili na sehemu yenye urahisi wa kufikiwa na wananchi wa pande zote ni eneo la karibu na stesheni ya SGR.
  • Kujenga kituo hicho youth mission kutaigharimu serikali kujenga barabara mpya ya lami kurahisisha ufikaji kwa haraka na hasa ukizingatia kuwa polisi wanahitaji barabara za uhakika ili kuwahi matukio ya kihalifu
 
Msubiri kwanza tushughulike na chattle nyie wengine baadae
 
Kihonda imepanuka sana na haina KITUO CHA AFYA, yaani wakazi wa Kihonda huduma za afya lazima waende Mafika au Nunge. Sasa ni maajabu mengine haya badala ya kufikiria kujenga kituo cha afya cha uhakika, eti wanajenga kituo cha polisi. Yaani huyu Mbunge ABOOD na meya wake bure kabisa, no wonder JPM amewachana live bila chenga!!!

Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
 
Kihonda imepanuka sana na haina KITUO CHA AFYA, yaani wakazi wa Kihonda huduma za afya lazima waende Mafika au Nunge. Sasa ni maajabu mengine haya badala ya kufikiria kujenga kituo cha afya cha uhakika, eti wanajenga kituo cha polisi. Yaani huyu Mbunge ABOOD na meya wake bure kabisa, no wonder JPM amewachana live bila chenga!!!

Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
Upo sahihi Mkuu kuna shida
 
Back
Top Bottom