Morogoro: Mama agoma mwanaye asizikwe, ataka mwili upelekwe kanisani aombewe ili afufuke

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakuu

Hali ya sintofahamu imeibuka eneo la Forest Hill, mjini Morogoro baada ya kifo cha binti Irene Joseph Akaro (30), ambapo mama wa marehemu ametaka mwili kupelekwa Kanisa la Kipentekoste la Ufufuo na Uzima ili aombewe ili afufuke, huku ndugu upande wa baba mzazi ukitaka taratibu za maziko ziendelee kwa imani ya Kikatoliki na mwili usafirishwe kwenda Moshi kwa maziko au mchungaji afike nyumbani kwa maombi hayo wanayoamini ya ufufuo.
Your browser is not able to display this video.
 
Mama kapata changamoto ya Afya ya Akili!Duuh Pole yake
 
Siku za Mwisho zimeka
siku za Mwisho zimekaribia
 
Anahisi mwanae karogwa maskini 😥
 
Wakina Gwajima wamechafua akili za watu. Sasa kama mbunge aje afanye miujiza kwa niaba ya CCM ya kutatua kero za mwananchi
 
🤣🤣🤣 Aiseee kunakaz kubwa ya kumtowa ujinga uyo mama
 
Haya apelekwe faster kwa mwamposa au Gwajima 😄

Ova
 
Hawa manabii feki wameharibu sana watu, hususani akina mama. Kuna mama mmoja aliugua brucellosis kama ilivyo bainishwa na madaktari, lakini ndg wa huyo mama hususani mama yake mzazi na dada yake mgonjwa walikataa katakata huyo mama kutibiwa hospital wakadai wampeleke kwa Mwamposa ili aombewe apone. Kidogo huyo mama akate kamba. Bahati nzuri mgonjwa alijiongeza na kurudi kuendelea na dawa za hospital, hadi sasa ni mzima wa afya.
 
Natamani kusema huyo mama wampeleke wakampime akili, ila kwa uchungu wa kufiwa tena na mtoto, asamehewe. Apatiwe tu ushauri kukubali ukweli, kila mtu ataonja umauti.
 
Wengi wanaenda Kwa Mwamposa ni wagonjwa baada ya hospitali kushindwa kutibu magonjwa.
 

Kazi sana...Gwaji Boy, opportunity has presented itself. Come showcasing your skills and abilities
 

"Religion is the opium of the people."

Karl Marx
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…