Muuza Kangala
JF-Expert Member
- Jul 21, 2021
- 1,242
- 4,813
Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Emilian Makalla (46) Mkazi wa Bigwa Barabarani wilaya ya Bigwa Mkoani Morogoro amejinyonga kwa kutumia chandarua na kufariki dunia nyumbai kwake huku chanzo kikiwa hakijafahamika.
Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu wameeleza kwamba Emillian alikuwa akisumbuliwa na changamoto ya ugonjwa wa afya ya akili jambo ambalo lilikuwa likipelekea kupelekwa hospitali mara kwa mara japo kwa sasa hakijulikani chanzo kulichopelekea kufanya maamuzi ya kujinyonga.
“Kaka yetu alikuwa na matatizo ya akili mara nyingi ana anguka na kufingwa mikono na miguu tunapigiwa simu tunahangaika nae anapona anarudi vizuri na kazi yake ni kulima na kufyatua matofali” Amesema Stella Thomas dada wa marehemu.
Soma Pia: Mwanafunzi darasa la saba ajinyonga kwa kutumia kamba ya chandarua
Aidha Afisa Mtendaji Kata hiyo amefika eneo la tukio na amesema tayari mwili wa marehemu umechukuliwa na kupelekwa hospitali na uchunguzi unaendelea kujua hasa nini kilipelekea Emilian kufanya maamuzi hayo
Kwa mujibu wa ndugu wa marehemu wameeleza kwamba Emillian alikuwa akisumbuliwa na changamoto ya ugonjwa wa afya ya akili jambo ambalo lilikuwa likipelekea kupelekwa hospitali mara kwa mara japo kwa sasa hakijulikani chanzo kulichopelekea kufanya maamuzi ya kujinyonga.
“Kaka yetu alikuwa na matatizo ya akili mara nyingi ana anguka na kufingwa mikono na miguu tunapigiwa simu tunahangaika nae anapona anarudi vizuri na kazi yake ni kulima na kufyatua matofali” Amesema Stella Thomas dada wa marehemu.
Soma Pia: Mwanafunzi darasa la saba ajinyonga kwa kutumia kamba ya chandarua
Aidha Afisa Mtendaji Kata hiyo amefika eneo la tukio na amesema tayari mwili wa marehemu umechukuliwa na kupelekwa hospitali na uchunguzi unaendelea kujua hasa nini kilipelekea Emilian kufanya maamuzi hayo