Morogoro: Polisi yachunguza tukio la Mwanafunzi wa SUA kukutwa amejinyonga katika makazi ya Wanachuo

Morogoro: Polisi yachunguza tukio la Mwanafunzi wa SUA kukutwa amejinyonga katika makazi ya Wanachuo

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Sua mwanafunzi.jpg

TAARIFA KWA UMMA Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linachunguza tukio la kifo cha Yosia Johani Keya (25) mwanachuo mwaka wa tatu katika chuo Cha kilimo cha Sokoine (SUA).

Tukio hilo limefahamika tarehe 9.3.2025 asubuhi huko katika eneo la makazi ya wanachuo hao kampasi ya Mazimbu, kata ya Mazimbu, Manispaa ya Morogoro.

Marehemu amekutwa amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia shuka ambalo alifunga kwenye Kenchi la makazi ya wanachuo upande wa baraza la nyuma. Uchunguzi wa tukio hilo umeanza ili kubaini chanzo cha tukio hilo.

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa vijana na watu wengine kuacha kuchukua maamuzi kam hayo ya kujitoa uhai kama suluhu ya changamoto zao.

Badala yake watumie fursa ya madawati mbalimbali ya ushauri nasaha na nasihi kueleza changamoto hizo. Imetolewa na; Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro.

Imetolewa na;
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro
 
Mtu akijinyonga lazima ajinyeee na kamasi litoke chezea koromeo wewe😂
 
Jeshi la Polisi mkoani Morogoro linachunguza tukio la kifo cha Yosia Johani Keya (25) mwanachuo mwaka wa tatu Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA).

Kwa mujibu wa taarifa za polisi, tukio hilo limegundulika jana, Machi 9, 2025 asubuhi katika eneo la makazi ya wanachuo hao Kampasi ya Mazimbu, Kata ya Mazimbu, Manispaa ya Morogoro.
Screenshot_20250310_103940_Lite.jpg


Marehemu amekutwa amefariki dunia kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kujinyonga kwa kutumia shuka ambalo inadaiwa alifunga kwenye kenchi la makazi ya wanachuo upande wa baraza la nyuma.

Uchunguzi wa tukio hilo umeanza ili kubaini chanzo cha tukio hilo ambapo Jeshi la Polisi limetoa wito kwa vijana na watu wengine kuacha kuchukua maamuzi kama hayo ya kujitoa uhai kama suluhu ya changamoto zao.

Jeshi la Polisi limeshauri kuwa badala yake, watumie fursa ya madawati mbalimbali ya ushauri nasaha na nasihi kueleza changamoto hizo.
 
Mpaka kufikia hatua hiyo alipitia phrases nyingi sana,i wish watu wangemsoma mapema.
Isikie tu hii situation 💔💔
 
Back
Top Bottom