Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Miongoni mwa watuhumiwa hao ni Erick Maguru Julias (33) mkulima, mkazi wa Miembeni. Alikamatwa Juni 2, 2024 baada ya kutuhumiwa kumuua kwa kutenganisha kichwa na kiwiliwili mtoto wake wa kufikia aitwae Johnson Eniath Ngonyani (6) mwanafunzi wa shule ya awali Mwembeni Mlimba. Mtuhumiwa alimuua mtoto huyo na kumnyofoa baadhi ya viungo ambavyo ni kichwa, viungo vya uzazi na kukata viganja vyote viwili, tukio ambalo lilitokea Juni 1, 2024 usiku katika kitongoji cha Kigamboni, Kijiji cha Mwembeni, Kata ya Mlimba, Wilaya ya Kilombero, Mkoa wa Morogoro. Baada ya tukio hilo mtuhumiwa alikamatwa kutokana na taarifa za raia wema ambapo alihojiwa na kukiri kufanya mauaji hayo na kutoa ushirikiano wa kuonyesha sehemu alikoficha hivyo viungo.
Wakati huo huo Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro limemkamata Jovina Stephen Mwakiyee, (33), mkulima na mkazi wa Kijiji cha Mang'ula A kwa tuhuma za kula njama na kumuua mume wake wa ndoa. Tukio hilo limetokea Juni 1, 2024 usiku huko katika kitongoji cha Gengeni, Kijiji cha Mang'ula A, kata ya Mang'ula, wilaya ya Kilombero, Mkoa wa Morogoro, ambapo mwalimu aitwae Christian Revocatus Tungaraza (39) mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Signal aliuwawa kwa kupigwa na kitu butu wakati akiwa amelala ndani ya nyumba yake. Upelelezi zaidi unaendelea kuwakamata watuhumiwa wengine walioshiriki mauaji hayo.
Aidha, Katika operesheni hiyo Jeshi la Polisi Morogoro limefanikisha kukamatwa kwa watuhumiwa, wanne ambao ni Hassan Mohamed Mbwambo (31) mganga wa kienyeji, mkazi wa Same, Mkoa wa Kilimanjaro, John Samwel Matunda (20) Bodaboda, mkazi wa Dumila wilaya ya Kilosa, Boniface Welesi Mwendi (31) Mkulima, mkazi wa Dumbalume Berega na Neema Johnson Mbwambo (32) Mkulima, mkazi wa Moshi.
Watuhumiwa walikuwa wanatafutwa kwa mauaji ya mfanyabiashara aliyefahamika kwa majina ya Elly Kimaro (Elly Maro) (53) mfanyabiashara wa madini, mkazi wa jijini Arusha, Tukio ambalo lilibainika Mei 26, 2024 saa mbili kamili usiku. Watuhumiwa baada ya kumuua walimnyang'anya kiasi cha shulingi milioni 15.
Kabla ya tukio hilo Mei 25, 2024 Marehemu alisafiri kwa basi liitwalo Mapenzi ya Mungu akifuatana na Hassan Mohamed Mbwambo kuja Mkoa wa Morogoro eneo la Turiani kwa ajili ya kufanya biashara ya madini.
Baada ya kufika Eneo la Turiani Mtuhumiwa kwa kushirikiana na John Samwel Matunda akiwa na pikipiki Walimteka hadi Kijiji cha Berege na kumnyang'anya kiasi hicho cha pesa na kumtaka mume wa marehemu awatumie kiasi kingine cha Tsh.milioni 5 ili aweze kuachiwa. Baada ya kupatiwa kiasi hicho walimuua na kumtelekeza katika shamba la Mbaazi katika Kijiji cha Berega hadi alipoonekana na wasamalia wema.
Kwa upande mwingine, Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro linafuatilia malalamiko ya ndugu Wolter Fuime (32) mkazi wa Mjimwema ambaye analalamika kushambuliwa na askari Polisi waliokuwa doria. Mei 26, 2024 askari Polisi walifika kwenye banda lake la kuonyesha video majira ya usiku kufanyia kazi taarifa fiche kuwa eneo hilo linatumiwa kufanya matendo yaliyo kinyume na maadili ikiwemo kuonyesha picha za video zisizo na maadili kwa Watoto na kumkamata mmiliki huyo wa banda na baadae kumwachia kwa dhamana.
Baadae alilalamika kuwa hajisikii vizuri hivyo anaomba hati ya kutibiwa ambayo amepewa na kwa kuwa kila hati ya matibabu inayotolewa lazima kuwe na uchunguzi, hivyo tumechukua hatua ya kulichunguza suala hilo kubaini ukweli.
Uchunguzi wa matukio haya unakamilishwa haraka iwezekanavyo kwa ajili ya maamuzi mengineyo kwa mujibu wa sheria.
Nitoe wito kwa wananchi kuchukua tahadhari mbalimbali dhidi ya wenza wao katika Maisha. Matukio haya yamesababishwa na sababu kadha wa kadha ikiwemo Imani za kishirikina, Tamaa ya mali na migogoro ya kifamilia. Jamii ichukue jukumu lake la msingi la kusimamia maadili ya watu wake ili kuepukana na matukio haya mabaya ya ukatili. Jeshi la Polisi kwa mara nyingine linawashukuru sana wananchi ambao wamesaidia kwa kubadilishana taarifa na kufankiwa kuwakamata watuhumiwa.
Imetolewa na
Alex Mkama-SACP
Kamanda wa Polisi Mkoa Morogoro.