Moshi mjini kuna fursa gani?

iMind

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2011
Posts
3,039
Reaction score
4,889
Nategemea kuhamia Moshi kikazi. Je pale Moshi nini naweza kufanya kwa capital ya 3- 5m?
 
tena mwambie atoe advance kabisa ili jamaa awe na uhakika wa soko
 
Nategemea kuhamia moshi kikazi. Je pale moshi nini naweza kufanya kwa capital ya 3- 5m?

kwakua unataka kuamia karibuni sio mbaya ungekuwa na subra ukifika utaweza kuona fursa unazoweza kufanya sababu fursa anayeweza kuona mtu mwingine ni tofauti na ww utakazoziona sababu picha inaweza kuwa moja lkn mtazamo tofauti!
 
Mkuu Moshi hakuna kitu...pale ni mwendo wa kubana hela tuu so ukianzisha biashara utaweka vitu na kuvinunua mwenyewe!
 
Aisee kwakweli Moshi ni pagumu kwasababu haina customers wengi sana wa biashara yoyote labda uuze pombe aina zote in December, Pia mji ni mdg na umeshakabwa vilivyo

Kingine kupata tu hata kiamba cha kujenga nyumba ya kuishi au hata ya kuku ni vigumu sana
 
Mahali ulipo furusa huja hapo hapo na kuondoka kama hukuiona, kisha huja furusa nyingine nayo huondoka kama hukuiona, kama umeiona ikamate utaona maajabu yake.
 
Moshi haiwezi kuwa na mzunguko wa hela kwa sababu moshi wanaofanya biashara ni wazee wa kichaga tena wale wa miaka toka 80yr.
Moshi hawauzi mashamba kama kwingine.
Wahindi nao wamekimbia wamekimbilia dar es slaam na Arusha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…