KERO Moshi Vijijini: Serikali isaidie Barabara ya Kata ya Mabogoni, haifai hata kidogo

KERO Moshi Vijijini: Serikali isaidie Barabara ya Kata ya Mabogoni, haifai hata kidogo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
photo_2024-05-16_10-50-23.jpg

photo_2024-05-16_10-50-23 (2).jpg

photo_2024-05-16_10-50-24.jpg
Nina wiki moja nimekuja Moshi, nimetembela baadhi ya sehemu za Wilaya ya Moshi Vijijini, Shabaha, Kata ya Mabogoni.

Wananchi wa Shabaha wanateseka sana na barabara iwe kipindi cha mvua au kiangazi kipande cha barabara mwisho wa Kituo cha Bajaji Shabaha.

Kuna barabara inaitwa Manguzoni kuelekea TPC Mita 700, imeharibika sana sana, ni barabara kubwa inayounganisha barabara ya lami kuelekea Moshi Mjini.

Gari, bajaji, pikipiki, baiskeli na Watembea kwa miguu, huwa mvua ikinyesha barabara haipitiki imechimbika sana.

Ujumbe uwafikie wahusika waitengeneze barabara hii, maana ndio barabara kubwa inayounganisha barabara mbili za kwenda Moshi Mjini.
photo_2024-05-16_10-50-25.jpg
 
Mabogini sio Mabogoni.

Toka nizaliwe sijawahi pita barabara mbovu kama hii unaweza ukahisi unaelekea kuzimu.
 
Back
Top Bottom