Mossad, operation bayonet: Jinsi kisasi kinavyoweza kuwa njia bora ya kupata haki yako

Exact mkuu. Hakuna ambaye aliuepuka huo mkono wa mungu
 
Complex,the bold wote mko vizuri sana.
 
kama mambo ya itaendelea ni ya kizamani kama unavyosema wewe, Leo hii kusingekuwa na tamthiliya/TV series mbalimbali zinazorushwa kila leo huku ya leo ikiwa ni muendelezo wa ilipoishia jana.
Mkuu huwezi mfurahisha kila mtu!! Wewe fanya majukumu ukimaliza njoo uendelee mkuu!!!

BTW hata wanaokutukana usiwalaumu maana ni dalili kisa kimetulia!!
 
Kilichoniuma kwenye revenge hii ni kijana aliyeuwawa kimakosa huku mkewe ni mjamzito.
 
kama mambo ya itaendelea ni ya kizamani kama unavyosema wewe, Leo hii kusingekuwa na tamthiliya/TV series mbalimbali zinazorushwa kila leo huku ya leo ikiwa ni muendelezo wa ilipoishia jana.
Sasa mkuu wale wapo kibiashara kuna faida kubwa wanapata na ndio maana wanawadhamini. Sasa ww mwenzangu na mm zaidi ya kuelimishana na kuburudishana hakuna kingine unachopata! Sasa kwann utufanyie hv!?
 

 
naongezea mkuu....!! huyo jasusi aliyefanya interview na hamshari baada ya kuchunguza mazingira ya nyumba kesho yake alikuja na van karibu na nyumba yake ndani kukiwa huyo jasusi na vifaa vya kuweza kujiunganisha moja kwa moja na simu ya hamshari, baada ya kujiunganisha walianza kutibua simu alizokua anawasilina na watu wengine baada ya muda alipiga simu kwenye kampuni ya simu ili waje warekebishe jamaa akawa anakata mawasiliano mpaka baadae ndipo walimpigia na kujitamblisha kwamba wanampigia kutoka kampuni ya simu. hamshari alielezea shida yake na jamaa walimwambia kwamba wangetuma mtu siku ya pili lakini hamshari alikataa na kusisitiza alihitaji arekebishiwe siku hiyo hiyo ndipo hatimae asubiri fundi atakwenda. ikumbukwe hawa jamaa walikuwa umbali sio mrefu kutoka nyumbani kwake, waliona kila aneingia na kutoka. walipoona watoto na mke wametoka, ndipo huyo jasusi alikwenda akiwa kavalia sawa sawa na mfanyakazi wa kampuni ya simu, alifika pale na kujitambulisha kwa mlinzi, mlinzi alipouliza aliambiwa ni kweli amewapigia, hamshari alikuwa na ulinzi mkali. jamaa aliingia ndani na alipoonyeshwa simu ilipo alienda na kuanza kuifanyia kazi ya kuweka bomu. jamaa kwenye van walizuia simu zote kwa wakati huo, bomu lilikua lilipuke baada ya kupokea simu. jamaa baada kumaliza na kuaga, alirudi kwenye van ndipo walimpigia simu alipopokea tu, likalipuka na kumchana chana vibaya kuanzia tumboni mpaka kwenye mapaja, alifariki baada ya siku chache....
 
Kisa kizuri sana, hivi visa kama hivi mnavipataje? maana sie wengine isingekuwa wewe na mtu kama The bold hakika tusingekuwa tunajua chochote.
 
Historia nzuri sana tunashukuru sana kiongozi kwa kazi nzuri, nimepata heshima kwa baadhi ya wanajamii yangu kuwapa sehem tu ya visa vya namna hii. Ombi langu ni kwamba, kama unaweza nipa list ya documentaries, Vitabu au Movies zinazoelezea harakati mbali mbali za WanaIsrael ili nizitafute na kupata ujuzi zaidi juu ya harakati zao. Natanguliza shukrani.
 
Naskiaga yule mmoroco baada ya kuuwawa mke wake wakimlipa fidia hela nyingi lakini hawakumuomba msamaha.

baadaye walimtumia mwanamke kuja kumuua yule waliokuwa wanamtafuta. walimuua kwa bomu la garini ambalo lilikuwa linatumia remote.

kaktika operation iliyoharibu sifa ya MOSSAD ni hii. maana kuna maafisa wake walikamatwa huko norway kama sijakosea.

nadhani sijaharibu ila nakumbuka tu hapa
 

Upo sahihi kabisa boss
 
Kisa kizuri sana, hivi visa kama hivi mnavipataje? maana sie wengine isingekuwa wewe na mtu kama The bold hakika tusingekuwa tunajua chochote.

Mkuu visa kama hivi huwa vipo documented kwa njia ya vitabu ama documentry ya video.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…