Leonel Ateba Mbinda
JF-Expert Member
- Feb 20, 2023
- 644
- 2,695
Kwa namna nilivyofuatilia suala la Mosses Phiri tangu awekwe benchi mechi ya Simba day mashabiki wamelalamika sana kwann hapangwi wakati anaonekana benchi, inakuwaje Bocco awe anacheza halafu Phiri ambaye tunamjua namna alivoibeba timu na kutufanya tupige saluti kila mchezo lakini hapangwi.
Baada ya makelele na presha kubwa Phiri akaanza kupangwa, lakn anapangwa muda mchache sana kuanzia dakika ya 80 na kuendelea, yaani Phiri sio chaguo la kwanza kwenye ushambuliaji, anaanza Baleke, anafuatia Bocco halafu Phiri, sijui Chilunda atacheza lini.
Ukifuatilia kwa undani utabaini kuna kitu kimetokea baina ya Phiri na uongozi, ni mchezaji wa ukweli lakini hathamini tena, sio mchezaji ambaye tunaweza kukaa na kusema leo ataanza, hapana, anachezeshwa ili mashabiki wasipige kelele lakini hapewi heshima anayostahili.
Hata kesho na Dodoma, anaweza kuingia cha 2 au msimuone kabisa.
Ndiyo soka letu hilo.
Baada ya makelele na presha kubwa Phiri akaanza kupangwa, lakn anapangwa muda mchache sana kuanzia dakika ya 80 na kuendelea, yaani Phiri sio chaguo la kwanza kwenye ushambuliaji, anaanza Baleke, anafuatia Bocco halafu Phiri, sijui Chilunda atacheza lini.
Ukifuatilia kwa undani utabaini kuna kitu kimetokea baina ya Phiri na uongozi, ni mchezaji wa ukweli lakini hathamini tena, sio mchezaji ambaye tunaweza kukaa na kusema leo ataanza, hapana, anachezeshwa ili mashabiki wasipige kelele lakini hapewi heshima anayostahili.
Hata kesho na Dodoma, anaweza kuingia cha 2 au msimuone kabisa.
Ndiyo soka letu hilo.