Raymanu KE
JF-Expert Member
- Jan 20, 2022
- 8,611
- 16,118
Hamjamboni wanajamvi? Natumai mpo salama kbsa.
Huu uzi Ni maalum kwa ajili ya mama zetu.Tuchukue fursa hii kuwapongeza mama zetu kwa Yale mengi mazuri waliotufanyia mpaka tumefikia Hapa tulipo.
Wapo wenzetu ambao kwa Bahati mbaya waliondokewa na mama zao wapendwa na Basi tunawaombea kwa Mungu aendelee kuzilaza roho zao mahali pema peponi🙏
Naamini kila mmoja anaelewa Yale magumu na changamoto walizopitiq mama zetu kipindi wanatulea tukiwa wadogo.Akina mama wamejaaliwa sifa ya uvumilivu maana huwaga wanapitia mengi Sana.
Binafsi sijawahi kuona mwanamke mzuri kuwahi kuishi Hapa Duniani kumliko mama yangu.Naeza sema yeye Ni Mungu wangu wa pili baada ya Mwenyezi Mungu. Mama yangu ndiye mwanamke ninayempenda na kumheshimu Zaidi maishani mwangu.Indeed she's my role model na huwa namuomba Mungu kila siku ampe baraka ya maisha marefu Hapa Duniani yenye furaha tele na amani.
Kiukweli siwezi kuyaelezea mazuri yote aliyonitendea mama yangu pamoja na ndugu zangu watatu hata nikapewa fursa ya siku nzima.Ni mengi Sana kwa kweli. Mama yangu Ni mwanamke wa shoka.Ni mpambanaji kiutaftaji, amejitoa Sana kwa ajili yetu sisi wanae.Toka tunazaliwa mpaka tumekua wakubwa mama amekuwa katika mstari wa mbele kupigania haki zetu.
Zipo changamoto nyingi Sana ambazo mama yetu alikumbana nazo kipindi anatulea sisi.Mateso na manyanyaso( mengine kutoka kwa baba yetu) ambayo siwezi kuyaeleza hapa jukwaani ila mama yetu alikuwa jasiri Sana katika kupambana na hizo changamoto mpaka akashinda.
Basi wanazengo,tuchukue fursa hii kuwapongeza mama zetu kwa Yale mengi waliotufanyia na kuwaombea baraka tele kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Mungu mbariki Mama yangu.
🙏🙏
Huu uzi Ni maalum kwa ajili ya mama zetu.Tuchukue fursa hii kuwapongeza mama zetu kwa Yale mengi mazuri waliotufanyia mpaka tumefikia Hapa tulipo.
Wapo wenzetu ambao kwa Bahati mbaya waliondokewa na mama zao wapendwa na Basi tunawaombea kwa Mungu aendelee kuzilaza roho zao mahali pema peponi🙏
Naamini kila mmoja anaelewa Yale magumu na changamoto walizopitiq mama zetu kipindi wanatulea tukiwa wadogo.Akina mama wamejaaliwa sifa ya uvumilivu maana huwaga wanapitia mengi Sana.
Binafsi sijawahi kuona mwanamke mzuri kuwahi kuishi Hapa Duniani kumliko mama yangu.Naeza sema yeye Ni Mungu wangu wa pili baada ya Mwenyezi Mungu. Mama yangu ndiye mwanamke ninayempenda na kumheshimu Zaidi maishani mwangu.Indeed she's my role model na huwa namuomba Mungu kila siku ampe baraka ya maisha marefu Hapa Duniani yenye furaha tele na amani.
Kiukweli siwezi kuyaelezea mazuri yote aliyonitendea mama yangu pamoja na ndugu zangu watatu hata nikapewa fursa ya siku nzima.Ni mengi Sana kwa kweli. Mama yangu Ni mwanamke wa shoka.Ni mpambanaji kiutaftaji, amejitoa Sana kwa ajili yetu sisi wanae.Toka tunazaliwa mpaka tumekua wakubwa mama amekuwa katika mstari wa mbele kupigania haki zetu.
Zipo changamoto nyingi Sana ambazo mama yetu alikumbana nazo kipindi anatulea sisi.Mateso na manyanyaso( mengine kutoka kwa baba yetu) ambayo siwezi kuyaeleza hapa jukwaani ila mama yetu alikuwa jasiri Sana katika kupambana na hizo changamoto mpaka akashinda.
Basi wanazengo,tuchukue fursa hii kuwapongeza mama zetu kwa Yale mengi waliotufanyia na kuwaombea baraka tele kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Mungu mbariki Mama yangu.
🙏🙏