pole dada BLISS...hiyo kitaalam inaitwa 'postural hypotension' (postural - something to do with position, hypotension - low blood pressure), yaani ni mabadiliko ambapo pressure ya damu mwilini hupungua ikisababishwa na kubadilisha mkao. Hali hii inaweza ikatokea kwa biandamu yeyote awe mgonjwa wa moyo au la, awe mja mzito au la. Inasabishwa na ukweli kwamba unapokuwa katika mkao fulani kwa muda mara nyingi ukiwa umekaa kitako au umelala, moyo unakuwa umezoea kupiga katika hali hiyo. Unaposimama ghafla na moyo kunotice kuwa position imechange, basi moyo unajaribu kucompensate hayo mabadiliko, na hivyo pressure inashuka na mapigo ya moyo yanaongezeka, wakati mwingine inaweza ikawa mbaya zaidi hata ukazimia. Hali iyo inadumu kwa muda mfupi tu mpaka moyo utakavyoweza kuaccomodate hiyo position mpya basi dalili zinaacha.
Kwa kawaida wakati wa ujauzito, wingi wa damu mwilini (blood volume) huwa unaongezeka, na mabadiliko hayo yanaweza tokea haraka haraka wakati moyo ukijitahidi kucope na hiyo hali. Kwa hiyo uwezekano wa kuwa unapata postural hypotension ni mkubwa zaidi ukiwa mjamzito, sana sana uja uzito mkubwa. ni hali ya kawaida kidogo,yaani sio ya kukufanya uogope kuhusu afya yako au maendeleo ya mtoto.
Cha kufanya: Kuwa makini unapobadilisha position/pozi, sana sana ukiwa unasimama toka kwenye kulala au kukaa kitako (wakati mwingine hata kugeuka unapokuwa umekaa au kulala). Inabidi usimame/ugeuke taratibu ili kuupa moyo muda wa kucompensate hizo changes za position bila pressure kushuka, moyo kwenda mbio au wewe kuzimia. Unapoona moyo unapiga mbio try to relax, take a deep breath iiin..and ooout, na tulia katika pozi moja mpaka mapigo yanavyopotea Yaani huyasikii tena), basi endelea kubadili position taratibu.
Ukiona hii hali inazidi, basi jaribu kuonana na daktari wa moyo 'cardiologist' kwa ajili ya uchunguzi zaidi.