Moyo wangu umekuwa na kiherehere jamani nisaidieni,

Moyo wangu umekuwa na kiherehere jamani nisaidieni,

BLISS

Member
Joined
Mar 31, 2011
Posts
54
Reaction score
13
jamani mimi naomba msaada, ninaujauzito wa wiki kumi sasa, lakini moyo wangu umekuwa unaenda mbio sana kwa muda then unarudi katika hali ya kawaida, na hii hunitokea mara ninaposimama, kufanya kitu chochote, au nikiwa nataka kuamka, je hii inatokana na nini? na nini cha kufanya? nimejaribu kutumia juic ya ukwaju lakini naona bado haipiti siku bila kusikia hali hii..

naomba ushauri wetu naamini mtanisaidia jamani maana kuna wataalamu wengi huku akiwepo mtaalamu RIWA.

ASANTENI,
 
pole dada BLISS...hiyo kitaalam inaitwa 'postural hypotension' (postural - something to do with position, hypotension - low blood pressure), yaani ni mabadiliko ambapo pressure ya damu mwilini hupungua ikisababishwa na kubadilisha mkao. Hali hii inaweza ikatokea kwa biandamu yeyote awe mgonjwa wa moyo au la, awe mja mzito au la. Inasabishwa na ukweli kwamba unapokuwa katika mkao fulani kwa muda mara nyingi ukiwa umekaa kitako au umelala, moyo unakuwa umezoea kupiga katika hali hiyo. Unaposimama ghafla na moyo kunotice kuwa position imechange, basi moyo unajaribu kucompensate hayo mabadiliko, na hivyo pressure inashuka na mapigo ya moyo yanaongezeka, wakati mwingine inaweza ikawa mbaya zaidi hata ukazimia. Hali iyo inadumu kwa muda mfupi tu mpaka moyo utakavyoweza kuaccomodate hiyo position mpya basi dalili zinaacha.

Kwa kawaida wakati wa ujauzito, wingi wa damu mwilini (blood volume) huwa unaongezeka, na mabadiliko hayo yanaweza tokea haraka haraka wakati moyo ukijitahidi kucope na hiyo hali. Kwa hiyo uwezekano wa kuwa unapata postural hypotension ni mkubwa zaidi ukiwa mjamzito, sana sana uja uzito mkubwa. ni hali ya kawaida kidogo,yaani sio ya kukufanya uogope kuhusu afya yako au maendeleo ya mtoto.

Cha kufanya: Kuwa makini unapobadilisha position/pozi, sana sana ukiwa unasimama toka kwenye kulala au kukaa kitako (wakati mwingine hata kugeuka unapokuwa umekaa au kulala). Inabidi usimame/ugeuke taratibu ili kuupa moyo muda wa kucompensate hizo changes za position bila pressure kushuka, moyo kwenda mbio au wewe kuzimia. Unapoona moyo unapiga mbio try to relax, take a deep breath iiin..and ooout, na tulia katika pozi moja mpaka mapigo yanavyopotea Yaani huyasikii tena), basi endelea kubadili position taratibu.

Ukiona hii hali inazidi, basi jaribu kuonana na daktari wa moyo 'cardiologist' kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
 
nashukuru kwa ushauri mzuri, nitaufanyia kazi..

ubarikiwe RIWA
 
Zaidi ya hapo tumia bio water yanayotengenezwa na bio disc. tembelea Amezcua. kama utahitaji maelezo zazidi niandikie private mail
 
yaani dada Blis tatizo ulilonalo ni kama langu, mimi ni mwanaume na siku si chache nimejigundua kuwa na tatizo hilo, inatokea sometimes moyo unapiga haraka haraka inaweza kuwa usiku au mchana, nimeenda hospitali na nimepima vipimo tofauti tofauti na nimeonekana sina tatizo la moyo, kwamba moyo huko normal, ila nikaambiawa inawezekana ni matatizo ya nerves au yawezekana kuna mabadiliko ya hali ya hewa.Kama kuna mtu liishawahi kupata tatizo kama hili tunaomba atujuze kwa kina hasa kuhusu hili.
 
nashukuru kwa ushauri, asanteni na mungu awabariki..

pole sana kaka, kama unatatizo kama langu..
 
Punguzeni uzito/unene kwa mazoezi, chakula bora na unywaji wa maji kwa wingi na tatizo litakwisha kabisa.
 
yaani dada blis tatizo ulilonalo ni kama langu, mimi ni mwanaume na siku si chache nimejigundua kuwa na tatizo hilo, inatokea sometimes moyo unapiga haraka haraka inaweza kuwa usiku au mchana, nimeenda hospitali na nimepima vipimo tofauti tofauti na nimeonekana sina tatizo la moyo, kwamba moyo huko normal, ila nikaambiawa inawezekana ni matatizo ya nerves au yawezekana kuna mabadiliko ya hali ya hewa.kama kuna mtu liishawahi kupata tatizo kama hili tunaomba atujuze kwa kina hasa kuhusu hili.
,

mimi ilinitokea nikatumia artic c ya forever living nikapona, piga 0718 754 694 kwa maelezo zaidi
 
pole dada BLISS...hiyo kitaalam inaitwa 'postural hypotension' (postural - something to do with position, hypotension - low blood pressure), yaani ni mabadiliko ambapo pressure ya damu mwilini hupungua ikisababishwa na kubadilisha mkao. Hali hii inaweza ikatokea kwa biandamu yeyote awe mgonjwa wa moyo au la, awe mja mzito au la. Inasabishwa na ukweli kwamba unapokuwa katika mkao fulani kwa muda mara nyingi ukiwa umekaa kitako au umelala, moyo unakuwa umezoea kupiga katika hali hiyo. Unaposimama ghafla na moyo kunotice kuwa position imechange, basi moyo unajaribu kucompensate hayo mabadiliko, na hivyo pressure inashuka na mapigo ya moyo yanaongezeka, wakati mwingine inaweza ikawa mbaya zaidi hata ukazimia. Hali iyo inadumu kwa muda mfupi tu mpaka moyo utakavyoweza kuaccomodate hiyo position mpya basi dalili zinaacha.

Kwa kawaida wakati wa ujauzito, wingi wa damu mwilini (blood volume) huwa unaongezeka, na mabadiliko hayo yanaweza tokea haraka haraka wakati moyo ukijitahidi kucope na hiyo hali. Kwa hiyo uwezekano wa kuwa unapata postural hypotension ni mkubwa zaidi ukiwa mjamzito, sana sana uja uzito mkubwa. ni hali ya kawaida kidogo,yaani sio ya kukufanya uogope kuhusu afya yako au maendeleo ya mtoto.

Cha kufanya: Kuwa makini unapobadilisha position/pozi, sana sana ukiwa unasimama toka kwenye kulala au kukaa kitako (wakati mwingine hata kugeuka unapokuwa umekaa au kulala). Inabidi usimame/ugeuke taratibu ili kuupa moyo muda wa kucompensate hizo changes za position bila pressure kushuka, moyo kwenda mbio au wewe kuzimia. Unapoona moyo unapiga mbio try to relax, take a deep breath iiin..and ooout, na tulia katika pozi moja mpaka mapigo yanavyopotea Yaani huyasikii tena), basi endelea kubadili position taratibu.

Ukiona hii hali inazidi, basi jaribu kuonana na daktari wa moyo 'cardiologist' kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Kaka ni kama vile umefunga thread!!

Joseph Masamaki likes this..
 
Back
Top Bottom