Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
NI SANAA AU UTELEZI?
Anajulikana kama DOLLO MOSSES TMK HALISI.
Nilimfahamu toka enzi za Radhia, Inahitaji roho ya chuma kuishi na watu vizuri na ngoma nyingine za Wachuja Nafaka na TMK WANAUME.
Sasa baada ya TMK kumeguka mapande mawili makuu, Nature akajitoa na kuunda TMK WANAUME HALISI huku Dollo AKIWEMO na andiko letu limejikita katika wimbo uitwao TATU BILA
Humo ndani, Dollo anasema;
"MPAKA MECHI INAISHA HAWAJAGUSA HATA MPIRAAAA"
Kiuhalisia, timu inayofungwa inatakiwa iuanze mpira, Sasa hii timu ilifungwa magoli matatu na haikugusa mpira? Mpira haukutoka kwamba warushe? Hakukuwa na faulo yoyote?
Ahh! Sijui nimewaza kwa sauti
Kisanaa, inaweza kuwa ni mbinu iitwayo Mbalagha (Hyperbole, overstatement, or exaggeration)
Je, Dollo aliikusudia hii au kalamu iliteleza?
Anajulikana kama DOLLO MOSSES TMK HALISI.
Nilimfahamu toka enzi za Radhia, Inahitaji roho ya chuma kuishi na watu vizuri na ngoma nyingine za Wachuja Nafaka na TMK WANAUME.
Sasa baada ya TMK kumeguka mapande mawili makuu, Nature akajitoa na kuunda TMK WANAUME HALISI huku Dollo AKIWEMO na andiko letu limejikita katika wimbo uitwao TATU BILA
Humo ndani, Dollo anasema;
"MPAKA MECHI INAISHA HAWAJAGUSA HATA MPIRAAAA"
Kiuhalisia, timu inayofungwa inatakiwa iuanze mpira, Sasa hii timu ilifungwa magoli matatu na haikugusa mpira? Mpira haukutoka kwamba warushe? Hakukuwa na faulo yoyote?
Ahh! Sijui nimewaza kwa sauti
Kisanaa, inaweza kuwa ni mbinu iitwayo Mbalagha (Hyperbole, overstatement, or exaggeration)
Je, Dollo aliikusudia hii au kalamu iliteleza?