Mpaka wa Namanga wafungwa kwa muda baada ya Kenya kuwazuia madereva malori kutoka Tanzania kwa kutokuamini vipimo vyao vya #Corona

Mpaka wa Namanga wafungwa kwa muda baada ya Kenya kuwazuia madereva malori kutoka Tanzania kwa kutokuamini vipimo vyao vya #Corona

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
MPAKA wa Namanga upande wa Tanzania umesitisha shughuli zote za kibiashara na nchi jirani ya Kenya kwa muda kutokana na nchi hiyo kutoamini vyeti vya ugonjwa wa Covid -19 unaosababishwa na virusi vya corona vya madereva wa malori wa Tanzania vinavyoonyesha kuwa hawajaambukizwa.

boda.jpg

Mkuu wa Wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe, ameiambia Nipashe jana kuwa hatua hiyo imefikiwa baada ya upande wa Kenya kukiuka makubaliano ya pande hizo mbili, waliyotiliana saini Mei, mwaka huu kwa kuzuia madereva wa Tanzania, kukataa vyeti ili wawaruhusu kuingia Kenya.

“Nadhani wenzetu wana ajenda ya siri kutuhujumu kiuchumi, tumeshakubaliana dereva anapopimwa upande wa Tanzania aruhusiwe upande wa Kenya kwa cheti, sasa wamekiuka makubaliano, wakifika upande ule wanataka wawapime tena sijui wana maana ipi nashindwa kuwaelewa kabisa, tumeamua kuchukua hatua na haturudi nyuma,” alisema.

Katika makubaliano hayo waliamua katika lori itaruhusiwa dereva na wasaidizi wawili kuingia katika nchi husika wote wakiwa wamepimwa kama wana maambukizo ya corona.
Hata hivyo, alisema upande wa Kenya wamebadilika juzi (Jumatatu) kwa kuzuia na kutaka kuwapima tena.

“Pamoja na juhudi za mimi na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, kuwasiliana na viongozi wenzetu wa Kenya, lakini zimegonga mwamba na ndipo tukaamua kuzuia vyeti vyote na magari ya mizigo kutoka Kenya pamoja bidhaa zote zinazoingia kutoka nchini humo hadi hapo tutakapokaa tena na kufikia muafaka maana sote tunategemeana, Kenya wanatuhitaji kama soko na sisi wanatuhitaji pia ili kuuza bidhaa,” alisema Mwaisumbe.

Alisema mwezi Mei makubaliano ya kuruhusu kuaminiana pande mbili yalikaliwa kikao na mawaziri wa mambo ya nje za nchi, makatibu wakuu, wataalamu na viongozi wengine wa mikoa na wilaya wa kutoka nchi mbili katika mpaka wa Namanga, kufuatia mazungumzo ya Rais John Magufuli na Rais Uhuru Kenyata ambao waliwaagiza viongozi wanaohusika kukaa na kufanya vikao na makubaliano, huku wakichukua tahadhari za ugonjwa huo na kuona namna ya kuendelea na biashara kwa nchi hizo.

Alisema kama hali ya kutoaminiana itaendelea, itawalazimu kutoa uamuzi wa kuigeuza Namanga kuwa bandari kavu na majirani Wakenya watashusha mizigo au bidhaa upande wake na Tanzania kuichukua na pia hata Tanzania itapeleka wa Tanzania ili Kenya waifuate.

“Nchi yetu ni huru inayojitegemea haihitaji kubembeleza nchi nyingine kufanya biashara kwa sababu sisi tunategemeana, haiwezekani mambo ambayo yameagizwa na marais viongozi wa chini hawatekelezi…linaashiria dharau na ajenda ambayo wanadhani ni siri iliyofichika kumbe sisi tunaifahamu, hatutaweza kuivumilia hata kidogo,” alisema.

Alisema, nia ya Rais Magufuli ni kuwasaidia watu wa hali ya chini kwa kuwa uamuzi huo unapofanyika wanao umia ni watu wa chini.

“Nataka nikuhakikishie ndugu kupima kipimo cha Covid-19 sio lelemama kinaumiza sana, sasa haiwezekani siku mbili mtu amechokonolewa pua, halafu anatoka upande wa Tanzania anaenda upande wa Kenya anafanyiwa kitu kile kile, sasa hali hii kwa kweli sio sahihi, tunataka hiyo agenda yao ya siri ijitokeze hadharani tushughulike nayo kuliko kutumia ugonjwa wa Covid-19, sisi hatutakuwa tayari,” alisema Mwaisumbe.
 
Tanzanian President John Magufuli has said the number of coronavirus patients in hospitals is declining, although the government has not released data on infection rates for many weeks.

The president has repeatedly downplayed the risk of the pandemic, causing alarm among neighbouring African countries and international organisations.

The government has even urged Tanzanians to dedicate three days for thanksgiving this weekend as they say they're beating the virus.

So what do we know about the situation in Tanzania?

Where is the data?

The main issue is that there's been no official data on the coronavirus for weeks, and there are concerns that the authorities are trying to downplay the extent of the outbreak.

Doctors and healthcare professionals are afraid to speak out about coronavirus because of a climate of fear.

"Tanzania has always had very repressive laws against freedom of expression and the press," says Roland Ebole, a regional researcher at Amnesty International.

"We are now seeing these laws being used in a more intensive way to target those who are speaking out, especially about Covid-19," says Mr Ebole.

The government stopped releasing daily updates on the number of positive cases in April, with the president saying they were creating panic.

The Africa Centres for Disease Control and Prevention has "strongly" called on Tanzania to release its latest data on the outbreak.

The last figures, published on 29 April, reported 480 cases and 21 deaths (its island territory Zanzibar has since added 29 more cases in May).
 
Safi sana. Nilikua napata hasira nikijaribu kuamini eti Kenya itaruhusu Watanzania waingie ingie kisa wana vyeti, na walivyo makajanja watafoji vyeti kariokoo na kuingia na corona.

Nchi inayothamini uhai na afya ya watu wake lazima iwe makini, hata kama italazimu kufungiana mipaka kabisa. Miaka ya 1977 EAC ilivunjwa na kutupwa kule, mipaka ikafungwa na kila mtu akaishi kwake, na wala hakuna aliyekufa.
 
Kuna mtu aliwahi kupendekeza . Ili hili jambo liende sawa . Madkatari wetu wawepo mpakani.

Wanaoingia Kenya waanze kupimwa mpaka wa Tanzania. The baadae mpaka mpaka wa Kenya wapimwe tena.
Kuwe na some sort of check and re-check system.
 
Safi sana. Nilikua napata hasira nikijaribu kuamini eti Kenya itaruhusu Watanzania waingie ingie kisa wana vyeti, na walivyo makajanja watafoji vyeti kariokoo na kuingia na corona.

Nchi inayodhamini uhai na afya ya watu wake lazima iwe makini, hata kama italazimu kufungiana mipaka kabisa. Miaka ya 1977 EAC ilivunjwa na kutupwa kule, mipaka ikafungwa na kila mtu akaishi kwake, na wala hakuna aliyekufa.
Mtachemsha mawe watoto walale na njaa 😀 😀 😀 😀 😀
 
Kenya nawaelewa msimamo wao kwa Sababu msimamo wa Tanzania ni kuwa ugonjwa wa Corona umeisha kwa maombi, sijui wamebaki wagonjwa 4 tu.

Sasa kwa mtu anayetumia logic haiwezi kuamini huu ujinga, lazima awapime Tena.

Tuache uzalendo uchwara tusimame na logic na reason.
 
Tanzania tunafanya mambo kiajabu sana, na hii yote inasababishwa na kufuata mawazo ya mtu mmoja, haiwezekani mseme vipimo vyenu vilikuwa vibovu baada ya kuvichunguza, halafu baada ya muda mnaanza kulazimisha idadi ya wagonjwa wa Corona imepungua, mtu mwenye akili atajiuliza imepungua kwa vipimo gani mlivyowapimia?

Hao wakenya ni haki yao kugoma, kwasababu kwanza tulishajifunga wenyewe kwa kukiri vipimo vyetu vilikuwa vibovu, sasa kwanini waamini hivyo vyeti vinavyopelekwa na madereva wetu? waacheni watumie vipimo vyao kuwapima wajiridhishe.

Halafu kwa akili za viongozi wetu watakurupuka nao kuwazuia wakenya, sijui watawazuia kwasababu gani wakati wakenya hawakuwahi kukiri kama vipimo vyao ni vibovu hivyo tusiwaamini madereva wao.
 
Kuna mtu aliwahi kupendekeza . Ili hili jambo liende sawa . Madkatari wetu wawepo mpakani.
Wanaoingia kenya.. waanze kupimwa mpaka wa tanzania. The baadae mpaka mpaka wa kenya wapimwe tena.
Kuwe na some sort of check and re-check system.
Kenya haawaamini Tanzania kwa Sababu tz unasema Corona umeisha kwa maombi, hii haingii akilini kwa mtu yoyote
 
Safi sana, nilikua napata hasira nikijaribu kuamini eti Kenya itaruhusu Watanzania waingie ingie kisa wana vyeti, na walivyo makajanja watafoji vyeti kariokoo na kuingia na corona.

Nchi inayodhamini uhai na afya ya watu wake lazima iwe makini, hata kama italazimu kufungiana mipaka kabisa. Miaka ya 1977 EAC ilivunjwa na kutupwa kule, mipaka ikafungwa na kila mtu akaishi kwake, na wala hakuna aliyekufa.
Safari hii Magufuli asipokee simu ya yeyote
 
Safi sana, nilikua napata hasira nikijaribu kuamini eti Kenya itaruhusu Watanzania waingie ingie kisa wana vyeti, na walivyo makajanja watafoji vyeti kariokoo na kuingia na corona.

Nchi inayodhamini uhai na afya ya watu wake lazima iwe makini, hata kama italazimu kufungiana mipaka kabisa. Miaka ya 1977 EAC ilivunjwa na kutupwa kule, mipaka ikafungwa na kila mtu akaishi kwake, na wala hakuna aliyekufa.
Njaa na mfumuko wa bei ndio mwamuzi mkuu.
 
Safi sana, nilikua napata hasira nikijaribu kuamini eti Kenya itaruhusu Watanzania waingie ingie kisa wana vyeti, na walivyo makajanja watafoji vyeti kariokoo na kuingia na corona.

Nchi inayodhamini uhai na afya ya watu wake lazima iwe makini, hata kama italazimu kufungiana mipaka kabisa. Miaka ya 1977 EAC ilivunjwa na kutupwa kule, mipaka ikafungwa na kila mtu akaishi kwake, na wala hakuna aliyekufa.
Sasa kwa nini Kenya walikubali in the first place, wangeonyesha msimamo kuwa haawaamini hizo certificate za vipimo kutoka Tz, sio wakubali halafu wabadilike tena.
 
Back
Top Bottom