Elections 2010 Mpendazoe aibukia Kinondoni

Elections 2010 Mpendazoe aibukia Kinondoni

Luteni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2010
Posts
2,274
Reaction score
302
Sekretarieti ya CHADEMA jimbo na Wilaya ya Kinondoni imemwomba mwanachama wake aliyehamia chama hicho hivi karibuni, Fred Mpendazoe (CHADEMA) kuwania ubunge katika Jimbo la Kinondoni. Tayari Mpendazoe amekubali kuchukua fomu ya kugombea ubunge kwenye jimbo hilo.
 
Naombeni matoke ya kinondoni na mtera
Jimbo la Kinondoni aliyeongoza ni Bw. Iddi Azan) akifuatiwa na Bi. Shy-Rose Bhanji
Jimbo la Mtera aliyeongoza ni Bw. Livingstone Lusinde (5,810) akifuatiwa na Bw. John Malecela (5,379),
 
mi namshauri apoe kwanza, apime alikotoka na anaenda wapi!
 
ni kiranja mzuri bungeni, anastahilim kuwepo lakindi ndio kazi inabidi ifanyike
 
Mtera Mzeee wetu kaangukia pua kwa kijana Lusinde.................
 
Sekretarieti ya CHADEMA jimbo na Wilaya ya Kinondoni imemwomba mwanachama wake aliyehamia chama hicho hivi karibuni, Fred Mpendazoe (CHADEMA) kuwania ubunge katika Jimbo la Kinondoni. Tayari Mpendazoe amekubali kuchukua fomu ya kugombea ubunge kwenye jimbo hilo.

jamani mwacheni abaki huku huku Segerea apambane na Mahanga mwakilishi wa RA. chonde chonde CHADEMA mpeni nafasi ya kugombea huku, mimi nina usongo na huyu mwakilishi wa mafisadi. Mpendazoe atakuwa mhanga na mmoja wa wapiganaji dhidi ya ufisadi huku Makongoro akiwakilisha mafisadi! patakuwa patamu nami nimeamua kuondokana na siasa za kujificha nitatoka hadharani na kumsaidia Mpendazoe, shujaa wangu aliyeacha ubunge na marupurupu yote kwa ajili ya ukombozi wa nchi yetu.
 
3rd August 10
Mpendazoe aibukia ubunge Kinondoni

Mwandishi Wetu

Baada ya kuangushwa kwenye kura za maoni za kuwania ubunge jimbo la Segerea jijini Dar es Salaam kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), aliyekuwa Mbunge wa Kishapu (CCM), Fred Mpendazoe, ameombwa na chama hicho kuwania ubunge wa jimbo la Kinondoni .
Ni baada ya Mpendazoe kuangushwa kwenye kura za maoni wa jimbo la Segerea hivi karibuni na Rachel Mashishanga katika uchaguzi ndani ya chama hicho uliofanyika hivi karibuni.
Katika uchaguzi huo, Rachel alipata kura 41 na kumbwaga Mpendazoe aliyeambulia kura 28.
Kwa mujibu wa Katibu wa Chadema, Wilaya ya Kinondoni, Fred Kimath, sekretarieti ya chama hicho jimbo na Wilaya ya Kinondoni ilikaa jana na kutoa uamuzi wa kumshauri Mpendazoea kuwania ubunge katika jimbo hilo.
" Kwa kutambua umuhimu wa kuwa na watu mashuhuri kama Mpendazoe na Mashishanga, sekretarieti ilituma ujumbe kumwomba agombee jimbo la Kinondoni na amekubali kufanya hivyo, “ alisema Kimath.
Alisema ujumbe ulioonana na Mpendazoe ni pamoja na Mwenyekiti wa jimbo hilo, Michael Sebugabo, Katibu Fred Kimath, Mweka Hazina, Edgar Njwaba, Katibu Mwenezi Moses Raymond, Katibu wa Mkoa wa Kinondoni, Henry Kilewo.
Kimath, alisema sekretarieti imeitisha kikao cha kamati ya utendaji kwa ajili ya kuwasilisha mapendekezo yake kabla ya mkutano wa kura za maoni na uteuzi kwa kuzingatia Katiba na kanuni za chama.
“Sekretarieti inamshukuru Mpendazoe kwa kukubali wito huu wa kuwatumikia Watanzania ikiamini Mpendazoe ni Mbunge wa Taifa ambaye m chango wake unahitajika kuing’oa CCM,” alisema Kimath.
Mpendazoe alikihama Chama cha Mapinduzi CCM mapema mwaka huu, akidai kuwa kimepoteza mwelekeo na kuhamia Chama cha Jamii (CCJ).
Baada ya chama hicho kukosa usajili wa kudumu hivyo kukosa sifa ya kushiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, Mpendazoe aliamua kuhamia Chadema.

NIPASHE
Mpendazoe aibukia ubunge Kinondoni
 
ITS A GUD MOVE I GUESS...! tunahitaji wabunge wa chadema wazidi 50. tumuunge mkono plzz..!
 
na mrema ntasemaje?mwacheni ajaribu bahati yake
 
Anajuta na atajuta kuhama ccm, kuhama jimbo lake, angebadilisha kimoja, either chama au jimbo, amekurupuka, amebadilsha vyote, sasa anahaha, wale akina chiligati walisema wanamtakia maisha mema, hata mimi naungana nao. segerea amechemsha, sasa kinondoni, bila shaka alikuwa hajapima kina cha maji, sasa ndo anajua kuwa nikirefu, na uwezekano wa kisurvive ni mdogo. aje tuungani tu huku mtaani kuuza magazeti, si ajabu story yake imeishia hapo. Aliondoka kwa mbwembwe nyingi mara ccm si mama yangu, sasa atajua kuwa ccm ni zaidi ya mama yake kwenye siasa. siajabu hata angeshindwa wangemsaidia kuiba, japokuwa uchaguzi wa mwaka huu mzee wakaya kasema kila mmoja kashabaleghe, akajitafutie, asije kulia hapa kila siku baba baba. Pole sana mpendazoe, ndiyo na maanisha pole sana. Hiyo ndo siasa.
 
Ubunge sio kukurupuka ni kupanga mikakati na kuangalia ni jinsi gani unaweza kusaidia sehemu yenye matatizo. Sasa kwenda tu kwenye jimbo mradi liko wazi wananchi tunakuwa na wasiwasi kwa kweli.
 
Back
Top Bottom