Mpenzi wangu kanipa ultimatum kuwa nisipomuoa mwaka huu, atachukua maamuzi magumu

Na bado tutakoma,nchi si wanaongoza?tuende nao taratibu na kwa kutulia🙂
 
Kumbe jibu tayari unalo bwana mkubwa
 
Ndoa ngumu bora usubirie tu hayo maamuzi magumu unaweza ku fight nayo lakini sio changamoto za ndoa
Nadhani kati ya watu walotoa ushauri basi ushauri wako nimuhimu sana,umeandika maneno machache yenye ujumbe mzito,binafsi simshauri aoe kwa sababu ya pressure kutoka upande mmoja kwenye kuoa kila mtu anamipango yake na wengine wanakuwa na malengo ya kutimiza ndo wakaoe,unaoa et kwa sababu wadogo zako wote wameoa??ni ujinga,unaoa et kwa sababu classmates wako wote wameoa ni ujinga,unaoa et kisa una miaka 30 ni ujinga?kikubwa ishi kwa malengo
 
Miaka mitatu mmehitimu shahada ya nini?

Mahusiano yenye fyucha huwezi kukaa miaka yote hiyo.

Yupo sahihi.
Kwani kuoana Ni lazima !? [emoji3][emoji3]

Hamuwezi kuwa ktk mahusiano bill kuoana na maisha yakasonga mkuu!?
 
Huyo tayari ana bwana wake tofauti na wewe shtuka na uanze kumuheshimu Mwanamke wa Mtu sasa [emoji3]
 
Hata walio oa/kuolewa hawana majibu ya kuridhisha kwanini wameoa

1. Wapo waliooa kwasababu ya shinikizo la wazazi, wapo wazazi wamekua wakiwalalamikia watoto zao kuwa umri unaenda wanataka wajukuu

2. Lipo kundi ambalo wameoa/kuolewa kwasababu wamekua wakiona watu wa rika zao wote wameoa hivyo wana inferior kuwa jamii inawaona kwa jicho baya

3. Wapo walio oa kwasababu ya mkumbo wamekuta jamii ikiishi katika utamaduni huo kua umri fulani ni lazima mtu awe ameoa/kuolewa

4. Na saizi wapo wanao oa kwasababu kesho ni mfungo, kundi hili la watu wamejiwekea udhaifu kwamba ni ngumu kuishi katika hicho kipindi bila kufanya ngono, na kufanya ngono ya bila ndoa katika kipindi hicho ni dhambi hivyo inamlazimu aoe ili kuhalalisha ngono

5. Wapo walio oa kwasababu ya uvivu wa kazi ndogo ndogo za nyumbani, hili ni kundi lenye watu wengi sana mpaka sasa. Hii inamaana kwamba watu hawa hawakuingia kwa nia madhubuti ya kifamilia/kindoa changamoto za kufua, kuisha vyombo, usafi kiujumla zimepelekea kufunga ndoa. Hapo utaona nafasi ya mke ni kama beki tatu

6. Lipo kundi la watu walioingia kwenye ndoa kutokana na "HOFU". Hili ni kundi ambalo ukiwauliza kwanini umeoa watakuambia "maisha bila mke ni risk sana kwasababu unaweza ukaumwa usiku ukakosa nguvu hata kushika simu ukashindwa hivyo bila mke waweza kufa"

7. Hawa ni wale walio oa baada ya kukutwa na hatia ya kuzini eidha alimpa mimba mwanamke kwa bahati mbaya hivyo ikamlazimu amuoe. Wapo pia wanawake watukutu waliogomea kwenye mageto ya masela kwa kuforce kuolewa

Siku ambayo watu watajua sababu ya msingi kwanini wanaoa kuna uwezekano tukadhibiti kwa kiasi fulani hii migogoro ya ndoa na idadi ya talaka
 
Kuna sababu mbili tu za ndoa nazo ni Ustaarabu wa kujamiiana na kuendeleza kizazi chenye maadili.(utunzaji sahihi wa watoto)

Kuna sababu mbili tu za ndoa kutokuvunjia ambazo ni hofu ya MUNGU na utii wa kiapo cha ndoa.
 
Kabisa mkuuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…